Wanaume wa jamii ya Kihadzabe wanaoishi kwenye pori la Myembe lililopo ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngogorongoro upande wa Ziwa Eyasi wakipanda mti wa mbuyu kurina asali. Kabila la Wahazabe ni moja ya jamii za wawindaji na wakusanyaji wanaopatikana Tanzania ambao chakula chao kikuu ni nyama, matunda, mizizi na asali. 
HONGERA KIONGOZI: Bwana Julius Indaya (katikakati) kiongozi wa jamii ya Wahadzabe wanaoishi upande wa Ziwa Eyasi akivishwa ngozi ya nyani na wenzake mara baada ya kufanikiwa kumkamata mnyama huyo kwa ajili ya kitoweo cha siku. Kwa utamaduni wa kabila la Wahadzabe kuvishwa ngozi ya mnyama ni ishara ya pongezi kwa mtu aliyefanikisha kukamatwa mnyama wakati wa uwindaji. Picha na Abuu Kimario - Bodi ya Filamu Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...