Na Tiganya Vincent-RS-Tabora

Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Dkt. Thea Ntara ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kuhakikisha wanakarabati upya Jengo la utoaji wa huduma ya Upasuaji katika Zahanati ya Ilolanguru lilojengwa chini ya kiwango na Mradi wa Mbola Melenia.Hatua hiyo inalenga kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza kwa mgongwa wakati anapata huduma ya upasuaji kutoka madaktari.

Dkt. Ntara ametoa agizo hilo jana Wilayani Uyui wakati alipokwenda kukagua vifaa vya kisasa vya upasuaji ambavyo vipo katika Zahanati hiyo toka mwaka 2013 lakini havijaanza kutumika kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubovu wa jengo lililojengwa na Mradi wa Mbola na ambalo halina ubora kwa mujibu wa Madaktari.

Alisema kuwa wajenzi wa jengo hilo waliamua kujenga hata bila kuwashirikisha Wataalamu wa Afya na Wahandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wala Mkurugenzi wa Wilaya ya Tabora na hivyo majengo yao mengi kuwa mabovu na ambayo yana nyufa kabla hayajaanza kutumika.

Dkt. Ntara aliongeza kuwa haiwezekani kwa muda mfupi baada ya kujengwa jengo liwe limeshapasuka na madirisha kuruhusu vumbi kuingia katika Chumba cha upasuaji , jambo ambalo ni hatari kwa mgongwa kupata maambukizi mengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...