Serikali Wilaya ya Kilolo  mkoani  Iringa  imetangaza  kuwachukulia  hatua kali  wazazi na  viongozi  wa  serikali  za   vijiji na vitongiji aambao  watasaidia kutorosha wanaume  wanaowapa mimba  wanafunzi katika maeneo  yao .
Agizo hilo  limetolewa na mkuu wa  wilaya ya  Kilolo Mhe. Asia Abdallah  wakati wa ziara  yake ya  kutembelea  shule  za msingi na  sekondari  katika kata ya  Ilula wilayani  humo  leo. Amesema kuwa  imekuwa ni kawaida ya  wazazi  kwa kushirikiana na baadhi ya  viongozi wa serikali za  vijiji na vitongoji  kupokea  pesa  kutoka kwa  wanaume  wanaowapa  mimba  wanafunzi  kisha kuwatorosha.
Mkuu  huyo wa  wilaya  alisema kuanzia  sasa mzazi ama kiongozi atakayebainika  kushiriki kupokea  pesa au  kumtorosha mtuhumiwa wa mimba   kwa  wanafunzi atakamatwa na kufikishwa mahakamani pasipo  huruma.
Hivyo alitaka  kila mzazi  na  kila mwananchi kuhakikisha  wanakuwa  sehemu ya  ulinzi wa watoto  hao wa kike na pale inapobainika  kuwa mwanaume ana mahusiano na  wanafunzi kuchukua hatua haraka ya kumfikisha kwenye  vyombo vya  sheria .Aidha  alisema kazi ya  viongozi wa  serikali  za  vitongoji na vijiji ni kuwalinda  watoto hao  wa  kike  dhidi ya  wabakaji kwa  kuwakamata na  kuwafikisha  polisi huku wazazi  hawana sababu ya  kukaa chini ya  watuhumiwa hao  wa mimba kwa lengo la  kumalizana nje ya vyombo  vya  sheria .
Mkuu wa  wilaya ya  Kilolo  mkoa wa Iringa Mhe. Asia  Abdallah akizungumza na wanafunzi wa kidato cha kwanza  shule ya  sekondari  Ilula leo
Walimu wa  shule ya  sekondari Ilula na  wanahabari  wakiwa katika kikao cha mkuu wa wilaya  ya Kilolo  leo
Mkuu wa  wilaya ya  Kilolo  mkoa wa Iringa Mhe. Asia  Abdallah akifurahia jambo na wanafunzi wa kidato cha kwanza  shule ya  sekondari  Ilula leo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...