Na Honorius Mpangala.

Wakati kipenga cha ufunguzi wa kigi kikipigwa agosti 20 mwaka 2016 kwa mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Azam na Yanga ilikua ni kitu kilichokua kikisubiliwa na wapenzi wengi kutokana na wadau kushuhudia usajili kabambe wa vilabu vyao.

Kuanza kwa ligi kuliweza kutoa harufu ya msisimko na ushindani katika msimu huo,mfano mechi ya kwanza kati ya Azam Fc dhidi ya African Lyon ilikua mechi ambayo iliwaduwaza sana mashabiki na benchi la ufundi la azam kutokana na shughuli waliyokutana nayo toka kwa vijana wa African lyon.

Azam katika mchezo huo ilisawazisha dakika za mwisho baada ya Lyon kutangulia kwa mpira wa kona ulioingia moja kwa moja na kumshinda kipa Aishi manula.

Kwa upande wa ratiba wadau wengi ambao wengi wao ni wanazi wa simba na yanga walilalamikia kwa kuona timu moja wapo ina pendelewa.

Changamoto ya ratiba imekua ni mfupa ulioshindikana kabisa kutokana ligi kusimama Mara kwa Mara au kutoa viporo kwa baadhi ya timu kutokana na kuwajibika kimataifa .

Mapendekezo yanayoweza kuwa bora ni uandaaji wa ratiba wa ligi kuu utazame kalenda ya FIFA  pamoja na ile ya CAF  ili wanapopanga wasiweze kuleta mkanganganyiko na kusababisha viporo.

Kwa upande wa usajili uliozua zengwe na kuleta mkanganyiko ni ule wa mchezaji Said mkopi aliyekuja kufungiwa baada ya Tanzania Prisons kupeleka pingamizi na kuonekana mkopi ana mkataba na klabu yake ya zamani huku akisajiliwa tena Mbeya City.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...