Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani Mhe. Filberto H. Sanga akizungumza katika hafla ya kukabidhi zawadi ya sikukuu ya Idd
El Fitri kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt.
John Pombe Magufuli kwa Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira
magumu cha Malaika Kids kilichopo Mkuranga leo.Kutoka kushoto ni Katibu Tawala
Msaidizi anayeshughulikia Utawala na Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
wa Pwani, Abdullrahaman Mdimu na Afisa Tarafa ya Mkuranga Clement Muya.
Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na
Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bw. Abdullrahaman Mdimu akizungumza
katika hafla ya kukabidhi zawadi ya sikukuu ya Idd El Fitri kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe
Magufuli kwa Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha
Malaika Kids kilichopo Mkuranga leo. Mhe. Rais ametoa zawadi ya mchele kilo
150, mbuzi pamoja na mafuta ya kupikia lita ndoo mbili.Kutoka kushoto ni Mkuu
wa Kitengo cha Sheria kutoka Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Mohamed
Magati, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto H.Sanga na Afisa Tarafa ya Mkuranga
Clement Muya.
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani,
Filberto H. Sanga akimkabidhi zawadi ya shilingi elfu kumi mmoja wa watoto
wanaolelea katika Kituo cha Malaika Kids wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi ya
sikukuu ya Idd El Fitri kwa niaba ya
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kilichopo Mkuranga leo. Mtoto huyo
amepewa zawadi hiyo kufuatia kujibu swali la Mkuu wa Wilaya huyo lililotaka
kufahamu watoto hao wanataka kuwa wakina nani katika maisha yao ambapo mtoto
huyo alisema anataka kuwa Rais. Anayeshuhudia ni Meneja maarufu kama Baba Mlezi
wa Kituo hicho James Kallinga.
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani,
Filberto H. Sanga akiwakabidhi watoto wa Kituo cha Malaika Kids kilichopo
Mkuranga zawadi ya sikukuu ya Idd El Fitri
kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli leo. Mhe. Rais ametoa
zawadi ya mchele kilo 150, mbuzi pamoja na mafuta ya kupikia lita ndoo mbili.
Mkuu wa Kituo cha Kulelea watoto cha Malaika
Kids kilichopo Mkuranga, Pwani James Kallinga akitoa neon la shukrani kwa niaba
ya watoto wa kituo hiyo mara baada ya kukabidhiwa zawadi za Idd El Fitri
zilizotolewa na na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya kituo hicho
leo. Kutoka kulia ni Katibu Tawala
Msaidizi anayeshughulikia Utawala na Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya Mkuu wa
Mkoa wa Pwani, Bw. Abdullrahaman Mdimu, Afisa Tarafa ya Mkuranga Clement Muya
na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani, Filberto H. Sanga. Picha zote na Frank Shija – MAELEZO, Mkuranga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...