MBUNGE wa Dodoma mjini Anthony Mavunde ameendelea kutatua kero katika sekta ya Afya jimboni humo ambapo leo amezindua matumizi ya mfumo wa Biometrics na kamera za CCTV katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma,kufuatia hali hiyo wagonjwa wengi waliokuwepo hospital hapo walionekana wenye furaha na kuunga mkono jitihada za mbunge wao katika kusaidia kuboresha huduma za Afya katika hospital hiyo.

Akizungumza katika uzinduzi wa matumizi ya vifaa hivyo, Mavunde amesema ufungaji wa mifumo hiyo ni miongoni mwa jitihada zake za kuhakikisha huduma za afya katika jimbo hilo zinatolewa ipasavyo.

Mavunde ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Ajira na Vijana amesema mfumo huo umefungwa na Ofisi ya Mbunge wa Dodoma na amelazimika kufunga vifaa hivyo kutokana na malalamiko ya muda mrefu ya wagonjwa kuwa wamekuwa wakitolewa lugha chafu na wauguzi.

Amesema pamoja na kamera hizo, pia umefungwa mfumo wa Biometrics(uchukuaji alama za dole gumba) ili kudhibiti watumishi ambao wamekuwa wakiondoka kabla ya muda na kuchelewa kuingia kazini.

“Kamera hizi zinarekodi sauti na kuchukua video ili kuondokana na malalamiko yaliyotolewa na wananchi na itakuwa ni rahisi kumbaini mtu atakayelalamikiwa na mgonjwa,”amesema Mavunde
Mbunge wa Dodoma Mjini Anthony Mavunde,akizungumza na wafanyakazi wa Hospital ya Mkoa wa Dodoma hii leo.
Mbunge wa Dodoma Mjini Anthony Mavunde,akizungumza na wafanyakazi wa Hospital ya Mkoa wa Dodoma hii leo,wakati wa uzinduzi mfumo wa Biometrics na kamera za CCTV katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo.
Mbunge wa Dodoma Mjini Anthony Mavunde,akibonyeza kitufe wakati wa kuzindua matumizi ya mfumo wa Biometrics na kamera za CCTV katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...