Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu Tamasha la Usalama Barabarani linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi wa nane, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam,ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi,Fortunatus Musilimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Fortunatus Musilimu, akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu Tamasha la Usalama Barabarani linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi wa nane, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli. Kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,Mhandisi Hamad Masauni.
Waandishi wa Habari wakimisikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa Mkutano uliohusu Tamasha la Usalama Barabarani linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi wa nane,mwaka huu katika Uwanja wa Taifa,Jijini Dar es Salaam, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk. John Magufuli.Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi,Fortunatus Musilimu.
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...