Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akikabidhi sehemu ya mifuko 10 ya Saruji katika kivuko cha karavati ili kuweza kujenga kingo katika kivuko hicho. picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega amesema kuwa maendeleo yoyote  yanapatikana kwa wananchi kujitoa kwa fedha pamoja na nguvu.
Ulega aliyasema hayo jana katika kijiji cha Chanungu wakati alipopeleka mifuko kumi kwa ajili kusaidia miundombinu ya barabara ya kijiji hicho ambao wamejitoa kufanya upanuzi kwa kungoa mimea yao.

Amesema kuwa kama viongozi kazi yake ni kusukuma maendeleo pamoja na kuangalia sehemu ambayo inatatizo na kuweka nguvu.

Ulega amesema kuwa kijiji hicho kiweke mkakati wa kuwa na ukusanyaji mapato yanayotokana na mauzo ya ardhi na fedha hiyo kuweza kutumika katika maendeleo .


Aidha amesema kuwa maendeleo ya kuwa na Shule na Zahanati katika kijiji hicho kuanza mchakato wa kutafuta maeneo.
 Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Chanungu juu ya maendeleo ya kijiji hicho.
 .Mwenyekiti wa Chadema katika kijiji jirani cha Chanungu akimpongeza Mbunge, Abdallah Ulega kwa kazi anayoifanya Mbunge wa jimbo hilo. Picha na Emanuel Masaka, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...