Na Mathias Canal, Kaskazini Pemba


Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesema kuwa Jukumu la kuleta maendeleo ya kiuchumi katika jamii ni la kila mwananchi sio jukumu la serikali pekee.


UVCCM imesema kuwa jukumu la serikali ni kuwaonyesha wananchi fursa zilipo na namna bora ya kuzichanganua ikiwa ni pamoja na kufanya kazi ili kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla wake sambamba na kuwezeshwa kupata mikopo katika vikundi vyao vya ujasiriamali.


Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 16, 2017 alipokuwa akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake katika mkutano wa ndani uliofanyika katika ukumbi wa Jamhuri Wilayani Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.


Alisema kuwa vijana ni nguvu kazi ya Taifa hivyo wanapaswa kutumia nguvu zao vizuri kwa kufanya kazi ili kujikwamua kiuchumi katika familia zao badala ya kukaa maskani kujadili mambo yasiyokuwa na tija kwao.


Aliongeza kuwa UVCCM inaunga mkono vijana kukaa maskani kwa maslahi mapana ya mjadala wa Maendeleo yatakayopelekea kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kujiunga katika vikundi mbalimbali vya ujasiriamali.
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akizungumza jambo pamoja na mwl,Ally khatibu Hassan Mkuu wa shule ya msingi Michekweni wakati akikagua jengo la Ujenzi wa maktaba pamoja na madarasa ya Shule ya Msingi Micheweni. wakati wa ziara ya kikazi  visiwani pemba.
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akiwa Shumba mjini akikagua sehemu itakayo jengwa jeti
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akigagua ujenzi wa ofisi ya ccm tawi la njuguni inayojengwa na mwakilishi Jimbo
 Afisa mipango wa halmashauri ya konde (pili kushoto)akitolea ufafanuzi juu ya ujenzi wa soko la mboga mboga la samaki pamoja na mbogamboga kwa Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akiwa katika ziara ya kikazi  visiwani pemba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...