Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania Dkt Raphael Chegeni (katikati) akiongoza kikao wakati Wajumbe wa Kamati hiyo walipokutana na Wajumbe wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada Mhe. Yasmin Ratansi (wa kwanza kushoto) akisisitiza jambo wakati Wajumbe wa Chama hicho kutoka Canada walipokutana na Wajumbe wa Kamati Tendaji ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada ambae pia ni Mbunge, Mhe. Yasmin Ratansi akimkabidhi zawadi Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania Dkt Raphael Chegeni mara baada ya Wajumbe wa pande zote mbili kuzungumza mapema leo katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa Kamati Tendaji ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada mara baada ya mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Ofisi ya Bunge)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...