Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala akikagua Mpaka wa Tanzania na Uganda katika Kituo cha Mpakani cha Mtukula mkoa wa Kagera, Katikati ni Kamishna wa Udhibiti wa Mipaka Samuel Magweiga ambaye ameambatana na Dk. Makakala katika ziara hiyo inayolenga kufanya ukaguzi katika Mpaka wa Tanzania na Uganda ili kujionea utekelezaji wa majukumu ya Idara yake katika Mpaka huo.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala akisalimiana na baadhi ya Maofisa wa Uhamiaji wanaofanya kazi katika Kituo cha Uhamiaji cha Mtukula mkoa wa Kagera alipofanya ziara kukagua Mpaka wa Tanzania na Uganda ili kujionea utekelezaji wa majukumu ya Idara yake katika Mpaka huo.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa pili kushoto akimsikiliza mmoja kati ya wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera alipotembelea kiwanda hicho ili kujionea shughuli za uzalishaji wa sukari ambapo alisisitiza dhana ya Uhamiaji na Maendeleo. Dk. Makakala ameambatana na Maafisa mbalimbali wa Idara ya Uhamiaji Makao Makuu.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala akimsikiliza Meneja Msaidizi wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera Bw. REO B.M alipotembelea Kiwanda hicho. Dk Makakala amewasisitiza Watendaji Wakuu wa Kiwanda hicho kuhakikisha wanafuata Sheria za Uhamiaji mara wanapoajiri wageni kutoka nje ya nchi. Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Makakala yupo Mkoani Kagera kwa ajili ya kufanya Ukaguzi katika Mpaka wa Tanzania na Uganda ili kujionea utekelezaji wa majukumu ya Idara ya Uhamiaji. 
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala akimkabidhi kipeperushi chenye taarifa mbalimbali za huduma zinazotolewa na Idara ya Uhamiaji Nchini, Mkuu wa wilaya ya Bukoba aliyepokea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mara baada ya Kamishna Jenerali Dk. Makakala kutembelea Ofisi hiyo akiwa ziarani Mkoa wa Kagera kukagua mpaka wa Tanzania na Uganda.(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...