Na David John -Mwanza.
KATIBU wa Chama cha Michezo wilaya ya Nyamagana Daddy
Gilbert amewataka wanasiasa kuacha tabia ya kuitumia michezo pindi
wanapotafuta nafasi za uongozi na wakishapata hawana habari.
Amesema wanasiasa wengi wamekuwa wakitumia michezo kama
tiketi yao ya kutaka uongozi na wakifanikiwa hawanahabari na michezo
jambo ambalo halipendezi.
Kiongozi huyo wa michezo ametoa dukuduku lake hilo wakati
akizungumza na waandishi wa habari ambapo walifika katika ofisi za chama
cha soka wilaya hiyo kutaka kujua namna walivyojipanga kuendeleza
michezo.
Daddy amesema anakerwa na baadhi ya wanasiasa ambao wanatumia michezo kupata uongozi na pindi wanapofanikiwa hawajari tena.
"unajuwa kama wenzetu wanasiasa wangekuwa wanatuunga mkono
naamini hata kwa hapa Mwamza tungefika mbali ,lakini bahati mbaya
wakishapata wanachokipata hawana muda tena na sisi". amesema Daddy.
Pia bosi huyo wa chama wilaya ametoa rai kwa wananchi wa
mkoa wa mwanza kujitokeza katika viwanja vya michezo hususani uwanja wa
Nyamagana ambapo ligi ya Willya kutafuta timu zitakazo cheza ligi ngazi
ya mkoa.
"kama mmavyoona hapa kuna ligi ya Wilaya ambayo
imeshirikisha timu 25 inaendelea lakini mwamko wa mashabiki Kama
mnavyoona."amesema Daddy.
Mwenyekiti
wa Chama cha Soka wilaya ya Nyamagana Daddy Girbat( kushoto) akiwa
katika picha ya pamoja na Mwandishi wa Habari hizi David John leo mara
baada ya kumtembelea ofisini kwake ulipo uwanja wa michezo wa Nyamagana.
Mkoani mwanza
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...