NA HAMZA TEMBA - WMU-DODOMA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Ngailonga Hasunga leo tarehe 18 Oktoba, 2017 ameripoti rasmi Makao Makuu ya Wizara hiyo yaliyopo Mtaa wa Kilimani, Makao Makuu ya Nchi, Mjini Dodoma.

Mhe. Hasunga amepokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi na kuingia ofisini kwake kwa mara ya kwanza ambapo amesaini kitabu cha wageni na baadaye akapata fursa ya kuzungumza na watumishi wa Wizara hiyo waliopo Dodoma.

Akizungumza na watumishi hao baada ya kutambulishwa, Mhe. Hasunga aliwaomba ushirikiano katika kufanikisha majukumu ya Wizara ambayo ni kuhifadhi na kusimamia matumizi endelevu ya maliasili na malikale, na kuendeleza ufugaji nyuki na utalii.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akikaribishwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (katikati) alipowasili kwa mara ya kwanza katika ofisi ya makao makuu ya wizara hiyo zilizopo mtaa wa Kilimani mjini Dodoma leo. Kulia anaeshuhudia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Tutubi Mangazeni.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akimtambulisha Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) kwa watumishi wa Wizara hiyo kabla ya kuzungumza nao leo mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na baadhi ya watumishi wa wizara hiyo baada ya kuwasili kwa mara ya kwanza katika ofisi ya makao makuu ya wizara hiyo zilizopo mtaa wa Kilimani mjini Dodoma leo. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...