Aliyekuwa
kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Samson Mwigamba Ametangaza kuachana na Chama hicho leo na kuamua kijunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) .
Mwigamba
amewaeleza Waandishi wa Habari kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo bila
kulazimishwa na mtu yoyote, hivyo yeye na
baadhi ya wanachama wa ACT wametangaza rasmi kujivua uanachama wa ACT-Wazalendo
na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“nimefikia
uamuzi huo baada ya viongozi wa ACT-Wazalendo kuwa na maamuzi ambayo ni tofauti
na lengo la kuanzishwa kwa chama akitolea mfano kuipinga serikali hata katika
shughuli za maendeleo hivyo Uongozi wa sasa wa chama hiki unachepuka kwa kasi
kubwa mno nje ya misingi ya chama na sasa chama kimebaki kuwa jahazi ambalo
tanga lake limechanika”amesema Mwigamba.
ameongeza kuwa baada ya kutangaza kujivua uongozi baadhi ya viongozi wa ndani ya
chama waligeuka vichaa wakinitukana kila aina ya matusi na cha ajabu hata wale
wanaofahamu na kuitetea misingi ya chama walitukanwa na viongozi wakiwepo na
wamekaa kimya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...