Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dkt.Hamisi Kigwangalla amesema Tanzania na Nchi ya Oman zimefanya mazungumzo katika kuimalisha sekta ya Utalii hasa kwenye Utalii wa kukuza Utamaduni na ule wa Kihistoria uliokuwepo miaka mingi kwa Mataifa hayo.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Kigwangalla amebainisha hayo jioni ya jana Oktoba 18,2017, wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya nyimbo na ngoma za Taifa la Oman yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam ambapo pia tukio lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri na viongozi wa Taifa hilo la Oman ambao wapo Nchini kwa ziara ya kusambaza Ujumbe wa Amani na Upendo kupitia meli ya kifahari ya Mfalme wa Oman Mhe. Qaboos bin Said ‘Fulk Al Salamah’.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dkt.Hamisi Kigwangalla akisalimiana na Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman Dkt. Mohamed Hamad Al Rumhy alipokuwa akiwasili kwenye tukio la Ngoma na nyimbo za Taifa la Oman, Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dkt.Hamisi Kigwangalla akiongea na Waziri wa Uwekezaji wa Oman Mhe. Salem Ben Nasser Al Ismaily, wakati akishuhudia tukio la Ngoma na nyimbo za Taifa la Oman, Jijini Dar es salaam
Bendi ya Jeshi la Taifa la Oman wakipiga nyimbo za Taifa hilo zinazofanyika wakati wa vita na ukombozi
Baadhi ya wananchi wakiwa na bendera za Taifa la Oman na Tanzania wakishuhudia tukio hilo
Baadhi ya Askari wa kikosi Maji cha Oman wakiwa katika tukio hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...