Ndugu
waandishi wa habari: Nimeshikwa na mshtuko, simanzi baada ya kusambaa
kwa taarifa ambazo naweza kusema kuwa ni za uzushi kwamba
ninampango wa kujiondoa ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
Chadema. naomba taarifa hizo zipuuzwe manahazina ukweli wowote na kwamba
zinampango wa kunichafua mimi pamoja na Chama Changu.
Ndugu wandishi wa habari : Napenda ieleweke kuwa sijawahi kudhani wala kufikiria kuhama Chadema na kwenda kwenye chama chochote kile cha siasa. Chadema ni chama ambacho nimetoka nacho mbali tangu mwaka 2004 hadi leo, nimejenga chama kwa gaharama zangu mwenyewe.
Ndugu waandishi wa habari: Leo nimekuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam kupitia Chama Changu cha Chadema,natambua kuwa chama kimeniheshimu sana kwa kunipa nafasi hii hivyo sina sababu ya kuondoka kwani ninania ya kuwatumikia Wananchi ambao wameniamini na wamenichagua kwa mapenzi yao wakiamini kuwa nitawaletea Maendeleo nikiwa ndani ya Chama Cha Chadema.
.Nafahamu tuhuma hizi zinatokana na aina ya utendaji wangu katika Jiji la Dar es Salaam kwani nimekuwa nikifanya kazi badala ya kupambana na serikali pale ambapo watu wanaamini kuwa mambo hayajaenda sawa.
Ndugu waandishi wa habari: Kukaa kwangu kimya huku ,kutokufanya siasa za kiharakati ndani ya jiji la Dar es Salaam haimanishi kwamba nipo upande wowote ama kukihujumu chama changu. Ila huu ni mfumo ambao nimeuchagua na kujijengea kwa ajili ya kuwatumikia wananchi nasio kufanya harakati za kisiasa kwakuwa nina nia ya kufanya maendeleo ndani ya jiji la Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Ndugu wandishi wa habari : Napenda ieleweke kuwa sijawahi kudhani wala kufikiria kuhama Chadema na kwenda kwenye chama chochote kile cha siasa. Chadema ni chama ambacho nimetoka nacho mbali tangu mwaka 2004 hadi leo, nimejenga chama kwa gaharama zangu mwenyewe.
Ndugu waandishi wa habari: Leo nimekuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam kupitia Chama Changu cha Chadema,natambua kuwa chama kimeniheshimu sana kwa kunipa nafasi hii hivyo sina sababu ya kuondoka kwani ninania ya kuwatumikia Wananchi ambao wameniamini na wamenichagua kwa mapenzi yao wakiamini kuwa nitawaletea Maendeleo nikiwa ndani ya Chama Cha Chadema.
.Nafahamu tuhuma hizi zinatokana na aina ya utendaji wangu katika Jiji la Dar es Salaam kwani nimekuwa nikifanya kazi badala ya kupambana na serikali pale ambapo watu wanaamini kuwa mambo hayajaenda sawa.
Ndugu waandishi wa habari: Kukaa kwangu kimya huku ,kutokufanya siasa za kiharakati ndani ya jiji la Dar es Salaam haimanishi kwamba nipo upande wowote ama kukihujumu chama changu. Ila huu ni mfumo ambao nimeuchagua na kujijengea kwa ajili ya kuwatumikia wananchi nasio kufanya harakati za kisiasa kwakuwa nina nia ya kufanya maendeleo ndani ya jiji la Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...