Idara ya Uhamiaji katika Kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) imefunga Vifaa vyenye mfumo mpya wa utambuzi na ulinganisho wa sura (Facial Recognition and Matching System) kwa abiria wanaoingia nchini.

Akiongea baada ya kupokea vifaa hivyo, Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka Samwel Rhobby Magweiga, amesema kuwa huo ni muendelezo wa mikakati ya Idara katika kuimarisha na kuhuisha KANZIDATA ya wanaoingia nchini.

“Vifaa na mfumo huu utasaidia sana katika kukusanya taarifa za abiria wote wanaoingia nchini kupitia hapa (JNIA), kama mlivyofahamishwa, mfumo huu unachukua sura ya mtu na kulinganisha na sura nyingine zilizomo kwenye kanzidata ili kuhakikisha taarifa zilizo kwenye pasipoti yake ni za pekee na hakuna mtu mwenye sura kama yake au mtu mwenye sura ingine kuwa na taarifa kama zake.”Alieleza Kamishna Samwel Magweiga.

Awali wakati akabidhiana vifaa hivyo, Mwakilishi mkazi wa Shirika la Uhamiaji la Kimataifa (IOM) Dr. Qasim Sufi alisema kwamba IOM itashirikiana na Idara ya Uhamiaji katika suala zima la udhibiti wa uingiaji na utokaji wa raia na wageni.

Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na shirika hilo, wamefunga vifaa vingine vyenye mfumo huo kwenye vituo vya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) pamoja na mpaka wa Holili kwa pande zote mbili za Tanzania na Kenya.

Kupitia ushirikiano huo na IOM, Idara ya Uhamiaji itaendelea kuimarisha maeneo yote ya mipaka kwa kufunga vifaa na mfumo huu wa kisasa zaidi kutumiwa hapa Afrika Mashariki.
Dr. Qasim Sufi Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji akifanyiwa majaribio katika mfumo wa utambuzi wa sura (Facial Recognition and matching system) katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam
Kamishna wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) Samwl Magweiga (wa kwanza kulia) akisikiliza kwa makini namna mfumo huo unavyofanya kazi wakati wa ufungaji wa vifaa vyenye mfumo huo.
Kamishna wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) akikabidhiwa nyaraka za mfumo huo na Mwakilishi Mkazi wa IOM Dr. Qasim Sufi mara baada ya ufungaji wa vifaa hivyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...