Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart-SACH) ya nchini Israel ambao walifika katika mkoa huo kwa ajili ya kumjulia hali na kufuatilia maendeleo ya elimu ya mtoto Julius Kaijage ambaye mwaka 2013 alifanyiwa upasuaji wa Moyo nchini humo.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akiwa katika kikao na wafanyakazi wa Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart-SACH) ya nchini Israel ambao walifika katika mkoa huo kwa ajili ya kumjulia hali na kufuatilia maendeleo ya elimu ya mtoto Julius Kaijage ambaye mwaka 2013 alifanyiwa upasuaji wa Moyo nchini humo.
Mama Judy Shore kutoka Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart-SACH) ya nchini Israel ambaye anaishi nchini Marekani wakizungumza jambo na mtoto Julius Kaijage ambaye mwaka 2013 alifanyiwa upasuaji wa moyo nchini Israel. Mama Shore aliamua kuja nchini kumjulia hali mtoto Julius baada ya kupata taarifa za kupona kwake ugonjwa wa moyo.
Mama Judy Shore na Tamar Shapira kutoka Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart-SACH) ya nchini Israel wakizungumza jambo na mtoto Julius Kaijage ambaye mwaka 2013 alifanyiwa upasuaji wa moyo nchini humo. Wafanyakazi wa SACH walitembelea mkoa wa Kagera kwa ajili ya kumjulia hali mtoto huyo.
Tamar Shapira kutoka Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart-SACH) ya nchini Israel akipokea zawadi ya kitenge kutoka kwa mtoto Julius Kaijage ambaye mwaka 2013 alifanyiwa upasuaji wa moyo nchini humo. Wafanyakazi wa SACH walitembelea mkoa wa Kagera kwa ajili ya kumjulia hali mtoto huyo.Picha na JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...