Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii
DIWANI wa Kijichi, Eliasa  Mtarawanje amesema kuwa kazi kubwa ni kuwatumikia wananchi  wa kijichi bila kujali itikadi za vyama.

Mtarawanje ameyasema hayo mara baada ya kuapishwa udiwani wake katika Baraza la Madiwani la Manispaa ya Temeke, amesema  uchaguzi umeisha Novemba 26 kilichobaki ni kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi wa kijiji.

Mtarawanje amesema kuwa Kijichi kuna miradi ya mingi kilichobaki ni kusimamia ili kuweza wananchi kupata huduma bora zinazotokana na miradi hiyo.

“Mimi kama kiongozi nimeamua kuwatumikia wananchi wangu wa kijichi hivyo nilazima nitumike katika kuwasaidia wananchi wenzangu kwa kuniamini kutoa kura zao na kuweza kupata ushindi” amesema Mtarawanje.

Amesema katika kipindi hiki cha serikali ya awamu ya tano ni kufanya kazi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na si vinginevyo .
 Diwani  wa Kijichi, Eliasa  Mtarawanje akilakiapo cha udiwani katika baraza la madiwani la Manispaa ya Teemeke leo jijini Dar es Salaam.
 Diwani  wa Kijichi, Eliasa  Mtarawanje akizungumza katika baraza hilo mara baada ya kuapishwa leo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke, Alimishi Hazali akizungumza juu ya ushindi wa diwani Diwani wa Kijichi, Eliasa  Mtarawanje katika baraza la madiwani la Manispaa ya Teemeke leo jijini Dar es Salaam.
 Diwani  wa Kijichi, Eliasa  Mtarawanje akiwa katika picha ya pamoja na madiwani wenzake mara baada ya kuapishwa leo jijini Dar es Salaam .
Diwani  wa Kijichi, Eliasa  Mtarawanje akiwa katika picha ya pamoja na vongozi wa CCM mara baada ya kuapishwa leo jijini Dar es Salaam .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...