Mwanamuziki mashuhuri wa kimataifa wa Afrika Kusini Hugh Masekela amefariki dunia leo jijini Johannesburg baada ya kushindwa vita dhidi ya tezi dume aliyopigana kishujaa kwa miaka kadhaa. 

Bendi yake imetoa taarifa ikisema kwamba marehemu Hugh Masekela amekuwa akipambana na ugnjwa huo tangia mwaka 2008, na kwamba mnamo Machi 2016 alifanyiwa upasuaji wa jicho baada ya saratani kusambaa ikabidi akafanyiwa upasuaji mwingine mwezi Septemba mwaka huo huo. 
 Hugh Masekela, aliyezaliwa mji wa KwaGuga huko Witbank, alianza kuimba na kucheza piano tangia akiwa mtoto. Na baada ya kuona filamu ya ‘Young Man with a Horn’ akiwa na umri wa miaka 14, Masekela akaanza kupuliza tarumbeta, ambapo Archbishop Trevor Huddleston ndiye alimpa tarumbeta yake ya kwanza. 
 Haukuchukua muda Masekela aliweza kuitawala trumpet hiyo na mwaka 1956 akajiunga na kundi lz jazz la Herbert’s African Jazz revue. Enzi za uhai wake alisema alitumia muziki kama silaha ya kusambaza mageuzi ya kisiasa enzi hizo za ubaguzi wa rangi, na alifanikiwa sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...