Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba ametembelea kiwanda cha kubangua Korosho cha Micronix System Limited kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara na kuzungumza na Viongozi wa kiwanda hicho juu ya kupandisha malipo kwa Vibarua wanaofanya kazi Kiwandani hapo.

Kwa Sasa mfanyakazi analipwa Kati ya Shilingi elfu 7 mpaka elfu 8 kwa siku ambapo wanafanya kazi Kwa Siku 5 kwa Wiki.

Tayari uongozi wa kiwanda hicho kwa  kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo wameahidi kulifanyia kazi Suala hilo.

 Waziri wa Kilimo Dr.Tizeba akiongea na Baadhi ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha kubangua Korosho cha  Micronix System ltd kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara ambacho Kimeajiri wafanyakazi 350.
 Waziri wa Kilimo Dr.Tizeba akioneshwa aina za Korosho ambazo Tayari zimebanguliwa na kuwekwa kwenye vibakuli ili kupima Ubora Tayari kwa Kupakia, Kushoto kwake ni mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo pamoja na Meneja Uzalishaji wa ETG Ltd Sunir Mizar.
 Waziri kilimo Dr.Charles Tizeba Akipanda Mche wa Mkorosho katika Kijiji cha Machombe,Kata Ya Marika kama Moja ya kuhamasisha upandaji wa Miche Mipya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...