Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii. 

KAMANDA wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Muslimu amesema hakuna sheria inayoruhusu askari polisi kupiga wanaotumia vyombo vya usafiri barabarani wakiwamo waendesha bodaboda huku akielezea kuwa atafuatilia ili kubaini iwapo kuna askari wenye tabia ya kupiga waendesha bodaboda. 

Muslimu ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana kwenye kupunguza ajali za barabarani ambapo Baraza la Taifa la Usalama Barabarani limetoa tathmini ya mpango mkakati wa awamu ya kwanza na awamu ya pili unaonesha ajali za barabarani zimepungua kwa kiasi kikubwa nchini. 

Hivyo ameelezea pia umuhimu wa watumiaji wa barabara wakiwamo waendesha pikipiki maarufu bodaboda kuzingatia sheria za usalama na kuelezea kuwa wanapaswa kufuata sheria bila shuruti. Hata hivyo waandishi wa habari waliokuwa kwenye mkutano huo walitaka kufahamu ni kwanini baadhi ya askari polisi hasa maeneo ya makutano ya Tazara, Ubungo, Mwenye na Daraja la Salenda wamekuwa wakiwapiga waendesha bodaboda na kusababisha hali ya sintofahamu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...