Zaidi ya wananchi 1200 wa kata ya Kirando inayojumuisha vijiji vinne vya Mtakuja, Mpata, Kichangani na Kamwanda, Wilayani nkasi Mkoani Rukwa, wajitokeza katika kuhakikisha uchimbaji na uwekaji wa msingi wa kituo cha afya cha kirando unakamilika ili kuweza kuanza upanuzi na ujenzi wa kituo hicho kitakachohudumia kata zaidi ya nne katika tarafa ya Kirando.  

Wananchi hao wamejitokeza kwa wingi kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Pombe Magufuli katika kuhakikisha huduma hizo za kiafya zinasogezwa karibu na wananchi yao ili kuokoa maisha ya kina mama wajawazito, watoto na wahitaji wengine wa huduma hizo ambao wanaishi karibu na kituo hicho na kuongeza kuwa umbali wa kutoka Kirando hadi hospitali ya Wilaya iliyopo Namanyere ni Kilometa 61.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo aliyeongoza harambee hiyo amesema kuwa wameamua kuungana na wananchi pamoja na kuwashirikisha ili kuwajulisha wananchi juhudi zinazofanya na wananchi na kuonyesha mshikamano kuwa maendeleo hayaji bila ya mshikamano.

“Kila mtu anaguswa na afya, mtoto, mzee na kijana wote, serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dk. John Pombe Magufuli imeamua kuboresha na kupanua vituo vya afya ili huduma zisogee karibu kuliko kutegemea hospitali za wilaya, kwa hali hiyo ndio maana serikali inapanua vituo vya afya ili tuupunguze msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali zetu pamoja na kwenye vijiji na tarafa huduma ziwe bora zaidi.” Alifafanua.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akiongea na kinamama walioshiriki kwenye Songambele ya Ujenzi wa upanuzi wa kituo cha Afya Kirando muda mfupi kabla ya kinamama hao kuruhusiwa na kuwaachia wanaume kuendelea na kazi.
  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa pili kutoka kushoto) akipokezana na wananchi mawe ya msingi yanayojengewa msingi wa kituo cha afya cha kirando siku ya uzinduzi wa songambele ya upanuzi wa ujenzi wa kituo hicho.
 Wanananchi wa Kirando waliojitokeza kushiriki katika Songambele ya ujenzi wa Kituo cha afya Kirando. 

 Wanananchi wa Kirando waliojitokeza kushiriki katika Songambele ya ujenzi wa Kituo cha afya Kirando.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...