Mjane wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere akizungumza na washiriki wa msafara wa waendesha baiskeli wa Twende Butiama na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi rasmi wa kuanza kwa safari yao ya kutoka Dar es Salaam, Oktoba mosi, kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo wanatarajia kufika Oktoba 14. Wakimsikiliza wa kwanza kushoto ni Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha aliyemwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Bw. Philip Besiimire, pamoja na Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare (wa kwanza kulia). Waendesha baiskeli takribani 200 watasafiri kwa kilometa zaidi ya 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere kwa kujihusisha na shughuli za elimu, afya, na mazingira wakiwa njiani.






Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare akizungumza na washiriki wa msafara wa waendesha baiskeli wa Twende Butiama na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi rasmi wa kuanza kwa safari yao ya kutoka Dar es Salaam, Oktoba mosi, kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo wanatarajia kufika Oktoba 14. Wakimsikiliza kutoka kulia ni Mjane wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, pamoja na Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha aliyemwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro. Waendesha baiskeli takribani 200 watasafiri kwa kilometa zaidi ya 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere kwa kujihusisha na shughuli za elimu, afya, na mazingira wakiwa njiani.




Msemaji wa familia ya Mwalimu Nyerere, Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Sinde Warioba akizungumza na washiriki wa msafara wa waendesha baiskeli wa Twende Butiama na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi rasmi wa kuanza kwa safari yao ya kutoka Dar es Salaam, Oktoba mosi, kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo wanatarajia kufika Oktoba 14. Wakimsikiliza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare, Mjane wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, pamoja na Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha aliyemwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro. Waendesha baiskeli takribani 200 watasafiri kwa kilometa zaidi ya 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere kwa kujihusisha na shughuli za elimu, afya, na mazingira wakiwa njiani.

Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha, aliyemwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, akizungumza na washiriki wa msafara wa waendesha baiskeli wa Twende Butiama na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi rasmi wa kuanza kwa safari yao ya kutoka Dar es Salaam, Oktoba mosi, kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo wanatarajia kufika Oktoba 14. Wakimsikiliza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare, Mjane wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire. Waendesha baiskeli takribani 200 watasafiri kwa kilometa zaidi ya 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere kwa kujihusisha na shughuli za elimu, afya, na mazingira wakiwa njiani.

Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation, Zuweina Farah akizungumza na washiriki wa msafara wa waendesha baiskeli wa Twende Butiama na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi rasmi wa kuanza kwa safari yao ya kutoka Dar es Salaam, Oktoba mosi, kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo wanatarajia kufika Oktoba 14. Wakimsikiliza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare, Mjane wa Hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, pamoja na Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha, aliyemwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro. Waendesha baiskeli takribani 200 watasafiri kwa kilometa zaidi ya 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere kwa kujihusisha na shughuli za elimu, afya, na mazingira wakiwa njiani.

Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha, aliyemwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire (kushoto) na Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare (kulia), mbele ya waendesha baiskeli takribani 200 wa msafara wa Twende Butiama kuashiria kuanza kwa safari yao ya kutoka Dar es Salaam, Oktoba mosi, kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo wanatarajia kufika Oktoba 14. Waendesha baiskeli hawa watasafiri kwa kilometa zaidi ya 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere kwa kujihusisha na shughuli za elimu, afya, na mazingira wakiwa njiani.


Kuelekea kumbukumbu ya kumuenzi baba wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alifariki Oktoba 14, 1999, msafara wa waendesha baiskeli unaojulikana kama Twende Butiama umeanza rasmi safari leo katika makazi yake Msasani jijini Dar es Salaam ambapo unatarajiwa kufikia tamati Oktoba 14, Wilayani Butiama.


Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, Meneja Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa, Bw. Benson Chacha aliwapongeza waandaaji wa Twende Butiama pamoja na wadhamini wa msafara huo, taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation kwa jitihada za kufanikisha tukio hili ambalo linahamasisha Watanzania kupenda michezo, kutunza mazingira na kujali afya zao.

“Nichukue fursa hii kuwapongeza kwa dhati waandaji na washiriki wote wa msafara wa Twende Butiama ambao wana dhamira ya dhati ya kumuenzi baba wa taifa. Tukio hili sio tu linachagiza shughuli mbalimbali ambazo Mwalimu Nyerere alikuwa anazipa kipaumbele lakini pia zitahamasisha Watanzania kupenda michezo. Michezo ni sekta muhimu ambayo ukiachana na kuimarisha afya lakini pia huleta umoja na mshikamano miongoni mwa watu. Pia, niwapongeze Vodacom kwa kudhamini ziara hii ambayo itapita mikoa tofauti ukihamasisha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Mchango wenu kwenye kudhamini sekta ya michezo tunaufahamu na tungependa kuona mkifanya hivyo kwenye michezo mingine kama vile riadha, masumbwi, na kadhalika,” alimalizia Bw. Chacha.

Madhumuni ya msafara huu utakaokuwa na waendesha baiskeli takribani 200 watakaoendesha baiskeli kwa kilometa 1,500 na kupita kwenye wilaya 20 ndani ya mikoa 10, ni kuenzi maisha na urithi aliotuachia Mwalimu Nyerere ambapo alikuwa akipambania kuhusu elimu bora, upatikanaji wa huduma za afya ili kuondokana na maradhi pamoja na ukuaji wa uchumi miongoni mwa Watanzania wote.


Kwa upande wake msemaji wa familia ya Mwalimu Nyerere, Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Sinde Warioba alizungumza kwa uchache wakati wa kuanza rasmi kwa msafara wa waendesha baiskeli nyumbani kwa Mwalimu, Msasani jijini Dar es Salaam kwa kusema, “nimefurahi kuona tukio hili limeweza kukusanya nchi tofauti zikiwemo zote za Afrika ya Mashariki kitu ambacho kinaonyesha mshikamano wetu.

 Njiani mtakapopita mtaweza kujionea nchi yetu ya Tanzania kwa upana wake na kupitia shughuli mtakazozifanya njiani zitawanufaisha Watanzania. Ni matumaini yangu kuwa kupitia msafara wenu mtaweza kuhamasisha mabadiliko kwenye sekta ambazo mtaziangazia kama yalivyokuwa malengo ya Mwalimu. Bado sekta za elimu, mazingira na afya zina mchango mkubwa kwa manufaa ya umma na nimefurahi kuona mmejikita kwenye maeneo haya. Niwatakie kila la kheri muwapo njiani na bila shaka tutajumuika pamoja kuwapokea mtakapofika Butiama.”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Harriet Lwakatare, ambao ndio wadhamini wakuu wa msafara huo kwa 2023, ameongezea kuwa, “kama tulivyoeleza wakati wa uzinduzi wa ushirikiano wetu, tuna imani kubwa na Twende Butiama hususani kwa kile wanachokifanya katika kuenzi maisha na urithi wa Mwalimu. Elimu, afya, na mazingira ni vipaumbele vikubwa vya taasisi yetu na siku zote tupo mstari wa mbele kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha maeneo haya yanaboreshwa ili kuwanufaisha Watanzania sehemu tofauti nchini kote. Ningependa kutoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kuunga mkono kampeni ya kuchangia dawati inayoendelea kupitia LIPA NAMBA 5483454, na kujumuika nasi katika shughuli za upandaji miti, na kushiriki kwenye kambi ya bure ya matibabu tutakayoiendesha.”

Kwa kumalizia Mwenyekiti wa Twende Butiama, Bw. Gabriel Landa amesema kuwa, “baada ya kuwatangazia Watanzania uwepo wa msafara wa Twende Butiama takribani wiki mbili zilizopita, hatimaye ile siku tuliyokuwa tunaisubiria kwa hamu imefika. Leo Oktoba mosi tukiwa hapa na washiriki takribani 200, tumeanza safari yetu kutokea nyumbani kwa Mwalimu, Msasani jijini Dar es Salaam na tunatarajia kufika Wilayani Butiama Oktoba 14. Tunawashukuru wadhamini wakuu wa mwaka huu, taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation, wadau, na Watanzania kwa ujumla wanaozidi kutuonyesha ushirikiano wao. Tukiwa njiani tutajihusisha na shughuli za kupanda miti, kuchangia madawati kwa shule za msingi za umma kwenye mikoa tofauti. Pia, tunawaomba watu wajitokeze kwa wingi kutuunga mkono njiani katika njia tutakazopita na kututia moyo.”

 

Na. Damian Kunambi, Njombe

Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe Caludia Kitta amewataka viongozi wa sekta ya elimu pamoja na viongozi wa dini wilayani humo kuhakikisha watoto wanajifunza mila na desturi za kitanzania na kupewa kipaumbele ili kuepusha watoto hao kujifunza tamaduni zilizo potofu na hasa za mataifa ya Magharibi.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa Rai hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika shule ya sekondari Elly's iliyopo katika kata ya Ilembila wilayani humo na kuhusisha viongozi wa kidiasa, wataalam mbalimbali, wazazi pamoja na wadau wa elimu wa wilaya hiyo.

Yohana Gwihaya ni mwalimu wa shule ya sekondari Elly's na Yaledi Mlyuka ni mdau wa maendeleo ya elimu wilayani humo wamesema kuwa watoto wanapolelewa katika misingi ya kiimani na kiroho husaidia kuwa na maadili yaliyo mazuri kwakuwa wanakuwa na hofu ya Mungu.

Aidha kwa upande wao baadhi ya wazazi walio huzuria mkutano huo wamesema kwa karne ya watoto wamekuwa wakiharibika na kuharibiwa na walezi wasio waaminifu hivyo ni vyema kujenga utaratibu wa kuzungumza na watoto mara kwa mara pamoja na kuwaasa kuwa na maadili yaliyo mema.






 

Na. WAF - Dar es Salaam

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka wananchi kufanya uchunguzi wa awali wa kupima Saratani ya Matiti ili kujua hali zao na kupata matibabu mapema kwa wenye changamoto hiyo
Waziri Ummy ameyasema hayo leo Octoba Mosi, 2023 wakati akimuwakilisha Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kwenye Maadhimisho ya Mwezi wa Saratani ya Matiti yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Saratani Ocean Road Jijini Dar es Salaam.

“Wataalamu wanatueleza kwamba mtu anaweza kujichunguza mwenyewe na akiona mabadiliko ya uvimbe katika titi, basi anashauriwa kuwahi katika kituo cha kutolea huduma za Afya kwa uchunguzi zaidi”. Amesema Waziri Ummy

Aidha, Waziri Ummy amesema Tanzania inakadiriwa kuwa na wagonjwa wapya wa Saratani takribani Elfu Arobaini na Mbili (42,000) kila Mwaka ndio wanafika katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

“Wakati Tanzania tunakadiriwa kuwa na wagoniwa wapya wa Saratani takribani Elfu Arobaini na Mbili (42,000) kila Mwaka, wagonjwa asilimia 38 tu ndio wanafika Hospitali, maana yake katika kila wagonjwa 100 wa Saratani, wagonjwa 38 tu ndio wanafika katika vituo vya kutolea huduma za Afya". Amesema Waziri Ummy

Pia, Waziri Ummy amesema taarifa ya mwaka 2022/2023, inaonesha kuwa Taasisi ya Saratani Ocean Road ilihudumia wagonjwa wapya takriban 8,779 na asilimia 13 ya wagonjwa hao sawa na wagonjwa 1,141 walikuwa na Saratani ya Matiti.

Sambamba na hayo, Waziri Ummy amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara ya Afya kufunga mashine za CT-Scan katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na mashine za Ultrasound katika Hospitali zote za Halmashauri nchini.

“Hii inamaanisha uchunguzi na ugunduzi wa Saratani ya Matiti ambapo unaweza kupima katika Hospitali ambazo zipo karibu na mahali tunapoishi ikiwemo Hospitali za Rufaa za Mikoa na Hospitali za Halmashauri”. Amesema Waziri Ummy

Hivyo, Waziri Ummy ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanafanya vipimo katika Hospitali angalau mara moja kwa mwaka hasa kwa wanawake endapo ikigundulika una tatizo basi matibabu yaanze mapema.

“Lakini hata wanaume wanatakiwa kupima kwakuwa, katika kila wagonjwa wa Saratani ya Matiti 100, wagonjwa 99 ni wanawake na Mmoja ni mwanaume hivyo tunawaomba wananchi wawahi katika vituo vya kutolewa huduma za Afya ili kupima na kupata matibabu mapema kwa wenye changamoto hiyo”. Amesema Waziri Ummy.


Na Beatus Maganja, ARUSHA.

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) inaandaa mkakati mpya wa ukusanyaji mapato utakaolenga kuongeza mapato ya Taasisi hiyo mara dufu ya makisio yake ya Mwaka wa fedha 2023/2024.

Hayo yamesemwa Leo Oktoba 1, 2023 na Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mabula Misungwi Nyanda katika kikao kazi na wakuu wa Kanda na wakuu wa mapori wa TAWA chenye lengo la kuboresha utendaji kazi katika nyanja za kuongeza mapato na Uhifadhi kwa ujumla, kilichofanyika  ukumbi wa Ngorongoro Crater Hall, Jijini Arusha.

Kamishna Mabula amesema suala la kuongeza Kasi ya ukusanyaji mapato ni maelekezo mahsusi kutoka kwa Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki na hivyo utekelezaji wake unapaswa kuanza haraka iwezekanavyo

"Hili suala la ukusanyaji mapato lisisubiri huo mkakati unaoandaliwa lianze Kuanzia Sasa hivi, Kila kitu unachokiona kwenye eneo lako ni rasilimali hakikisha unakitumia kuingiza mapato" amesisitiza Kamishna Mabula

Kamishna Mabula pia ametoa msisitizo katika suala zima la udhibiti wa Wanyamapori wakali na waharibifu na kuwataka maofisa hao kutafuta mbinu mbadala za kuhakikisha Wanyamapori hao hawaendelei kuleta madhara kwa maisha na mali za binadamu.

Aidha, amewataka maofisa hao kuzingatia maelekezo aliyoyatoa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili Kamishna Benedict Wakulyamba wakati wa semina elekezi kuhusiana na Wanyama Wakali na Waharibifu

Kwa Upande wake Kaimu Naibu Kamishna wa Uhifadhi Mlage Kabange amesema mtaji namba moja wa TAWA ni  ulinzi wa maeneo yote waliyopewa kuyasimamia kwani maeneo yanapokuwa salama ndipo uzalishaji mapato unaongezeka ikizingatiwa kuwa asilimia 70 ya mapato ya TAWA yanatokana na shughuli za Uwindaji wa Kitalii

Sanjari na hilo, amesisitiza kuongeza Kasi ya utekelezaji wa zoezi la kuweka alama za mipaka katika maeneo yote yaliyo chini ya Usimamizi wa Taasisi  huku wakifuata miongozo na maelekezo yote yaliyotolewa na Serikali.















Na Victor Masangu,Kibaha

Katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta ya michezo mke wa Mbunge la Jimbo la Kibaha mjini Selina Koka ameanzisha  rasmi mashindano ya mchezo wa netiboli kwa wanawake wa jumuiya ya umoja wanawake (UWT) kata ya Misugusugu.

Mama Koka amezindua michuano hiyo ikiwa ni moja ya ahadi yake kubwa ambayo aliitoa ya kukuza na kuinua vipaji vya mchezo huo kwa wanawake wa kata zote 14 zilizopo katika Jimbo la Kibaha mjini ili kuweza kupata fursa ya wanawake kushiriki kikamilifu katika kukuza vipaji vyao.

Alibainisha kwamba hivi karibuni aliweza kufanya ziara yake katika kata mbali mbali akiwa Kama mlezi wa UWT Kibaha mji na alitoa na kukabidhi vifaa mbali mbali kwa timu husika ikiwemo mipira pamoja na jezi lengo ikiwa ni kila kata kuweza kuunda timu yao ya netiboli.

"Kwa kweli nimefarijika sana leo kuwepo hapa katika kata ya Misugusugu ikiwa nimekuja kuonana na wanawake wenzangu sambamba na kuzindua mashandano haya ambayo tumeyapa jina la Selina Cup na mm lengo langu ni kukuza vipaji zaidi katika mchezo huu wa netiboli,"alisema Mama Koka.

Kadhalika aliwahimiza wanawake wote wa UWT kuwa na mshikamano katika kushiriki katika mambo mbali mbali ikiwemo suala zima la michezo pamoja na  kukiimarisha chama Cha mapinduzi kuanzia ngazi za chini kabisa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mji Elina Mgonja alimpongeza Mke wa Mbunge kwa ushirikiano wake wa kujitolea na kuwa karibu na jamii katika nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya michezo hususan netiboli kwa wanawake.

Hivi karibuni Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mji alipokuwa katika ziara ya Mwenyekiti wa UWT Kibaha mji aligawa vifaa mbali mbali vya mchezo wa netiboli katika kata 14 kwa lengo la kukuza na kuinua na kukuza vipaji vya wanawake wa Jimbo la Kibaha mjini.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dokta Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuweka Sera na Mipango madhubuti ili kuimarisha Ustawi na Maendeleo ya Wazee wote Nchini.

Dokta Mwinyi ameyasema hayo leo katika Hotuba yake iliyowasilishwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, wakati wa Hafla ya  Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, katika Ukumbi wa Dokta Shein wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema, kama ilivyokuwa dhamira ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Mwaka 1964, chini ya Kiongozi Shupavu, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, iliyohakikisha inapelekea kuandaa Mipango imara ya kuitunza Sehemu na Rika hiyo Muhimu ya Jamii, Serikali inao wajibu wa kusimamia na kuona hayo yanaendelezwa.

Hivyo amesema, ni jukumu la kila mmoja kuungamkono jitihada za Serikali na Wadau wengine ili kuhakikisha hali, ustawi na hadhi ya Wazee Nchini inaimarika.

"Kwa mara nyengine tena, nazihimiza taasisi, mashirika na wadau, zikiwemo Jumuiya za Wazee Nchini, kuendelea kuungamkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha Zanzibar inaendelea kuwa ni mahala bora pa kuishi kwa watu wa rika zote", amehimiza Dokta Mwinyi.

Aidha, ameainisha jitihada mbali mbali za Serikali katika kujenga ustawi wa rika hiyo ikiwemo kuondoa ubaguzi; kuimarisha uwezo na kukuza ushiriki wa kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa makundi yote, bila ya kujali umri, jinsia, hali ya ulemavu, rangi, kabila, dini, mahali mtu anapotoka au hali yake ya kiuchumi.

Sambamba na hayo, Dokta Mwinyi ametaja Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya Mwaka 2050;  na Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar (ZADEP 2021 – 2026), iliyolenga kuimarisha ustawi na maendeleo ya Wazee Nchini; pamoja na kile alichobainisha kuwa katika utekelezaji wake wa vitendo, Serikali imeandaa Sera ya Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2014 ambayo pia imeweka mikakati madhubuti ya kusimamia Maendeleo ya Wazee, hapa Nchini.

 

Akitoa ufafanuzi juu ya Posho la Wazee, Dokta Mwinyi amefahamisha kwa kusema, "Kwa kuthamini mchango mkubwa wa Wazee wetu katika kuleta maendeleo ya Nchi, Serikali imeongeza Kiwango cha Pencheni Jamii kutoka Shilingi Elfu Ishirini (20,000/=) hadi Elfu Khamsini (50,000/=) sawa na asilimi Mia na Khamsini (150%) kwa Wazee wote wenye umri wa miaka Sabiini (70) na kuendelea ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa Sera ya Hifadhi yaJamii ya Mwaka 2014 ambayo imeeleza changamoto kubwa inayowakabili Wazee ni ukosefu wa usalama wa kipato; Na kwamba mpaka kufikia Septemba 2023, jumla ya Wazee 29,307 wamesajiliwa, ambapo kwa Unguja ni 17,482 sawa na asilimia 59.6; na 11,825 kwa Pemba, sawa na asilimia 40.3 ambao wanapokea Pencheni kila Mwezi; na kati ya hao Wanawake ni 16,889 sawa na asilimia 57.6, na kwa Wanaumeni 12,418 sawa na asilimia 42.4".

 

"Napenda kuchukua nafasi hii kuwaagiza watendaji wote wanaoshughulikia suala hili la Pencheni-Jamii kuzidisha ushirikiano, ili kuhakikisha lengo la Serikali linafikiwa, pamoja na kuondosha changamoto zote zinazojitokeza wakati wa usajili hadi kupokea Pencheni- Jamii; Aidha, katika kuhakikisha Mpango huu wa Pencheni-Jamii unaimarika zaidi, Serikali imeandaa Sheria ya Kusimamia Masuala ya Wazee, Namba 2 ya Mwaka 2020 ambayo imeweka Miongozo imara inayohakikisha Wazee wetu wanapatiwa pencheni kwa kuzingatia Vigezo vilivyowekwa".

 

Rais Dokta Mwinyi, katika Hotuba yake hiyo, amefahamisha kwamba, Serikali inaendeleza jitihada zake za kuwahudumia na kuwatunza Wazee wasiokuwa na Ndugu wala Jamaa, katika Makao Maalum ya Wazee, yaliyopo Sebleni na Welezo kwa Unguja, na Limbani kwa Pemba, ambapo kwa sasa Jumla ya Wazee 63 wanatunzwa katika Makao hayo, huku wakiendelea kupatiwa huduma muhimu zikiwemo Chakula, Malazi, Mavazi, Matibabu na Posho.

 

Ametoa wito kwa familia na wanajamii kutokwepa majukumu ya kuwalea Wazee na kuwacha tabia ya kuwapeleka kulelewa katika Vituo vya Wazee, kwani  wanahitaji huruma na mapenzi kutoka kwa watoto na jamii inayowazunguka, kama ambavyo Vitabu Vitukufu vimehimiza.

 

Aidha, Dokta Mwinyi ametumia fursa hiyo kuwakumbusha Wazee juu ya Wajibu wao wa kuendelea kutoa maelekezo mema na mawaidha juu ya ustawi mzuri kwa jamii, hasa wakati huu ambao panashuhudiwa mporomoko mkubwa wa maadili.

 

Akiwa Mgeni Rasmi wa Hafla hiyo, Mheshimiwa Othman ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib.

 

Naye, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Zanzibar, Mhe  Riziki Pembe Juma amesema Serikaki imefanikisha kuwepo kwa harakati mbali mbali zikiwemo za kuwafikia Wazee wa Hali tofauti katika jamii, sambamba na kuandaa Makongamano ya kujenga uelewa, ili kuhakikisha Maadhimisho ya Mwaka huu yanafana zaidi na kugusa ngazi zote.

 

Amehimiza pia haja ya kuwathamini na kuwatunza Wazee, bila ya bughudha wala kuwapa usumbufu, huku akifafanua kwamba tayari Serikali ya Zanzibar imetoa Vitambulisho kwa Wazee waliotiimiza umri wa Miaka 70, ambavyo vitasaidia upatikanaji wa huduma muhimu zikiwemo za usafiri wa umma, afya, Viwanja vya Michezo vya Serikali na Pencheni-Jamii, ambapo hadi sasa takriban Wazee 28,668 wamepatiwa.

 

Katika Risala yao, iliyowasilishwa na Mwalimu Issa Kidali, sambamba na Wakuu wa Jumuiya za JUWAZA (Jumuiya ya Wazee  Zanzibar) JUWAMAZA (Jumuiya ya Wazee Wenye kuishi katika Mazingira Magumu Zanzibar), Bi Salma Saleh na Bw. Hashim Bakar Kondo, Wazee wameeleza changamoto kadhaa zinazowakabili, zikiwemo  za ukosefu wa masoko ya kuuzia bidhaa zao, hali inayozidi kudhoofisha matumaini ya uhakika wa kupata mahitaji yao ya msingi ya kila siku.

 

Wazee hao, ambao miongoni mwao wamekabidhiwa Vitambulisho kwaniaba ya wenzao kwaajili ya kupata huduma mbalimbali, wamemtunukia Mheshimiwa Rais zawadi, kikiwemo Cheti cha Shukran.

 

Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Mwaka huu ni UTHABITI WA WAZEE KWENYE DUNIA YENYE MABADILIKO, ujumbe unaokwenda sambamba na Lengo Nambari 10 la Maendeleo Endelevu, linalohusu kupunguza tofauti miongoni mwa Nchi na linalolenga kuhakikisha unakuwepo usawa katika upatikanaji wa fursa na kupunguza tofauti ya kipato kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo ya maendeleo na ustawi wa Wazee.

 

Viongozi mbalimbali wamehudhuria Hafla hiyo wakiwemo Mawaziri; Manaibu Waziri; Makatibu na Manaibu Katibu Wakuu wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Mheshimiwa Zena Ahmed Said; Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya; Mabalozi na Wanadiplomasia,; Wakuu wa Mashirika ya Kitaifa na Kimataifa; Watendaji wa Serikali; Viongozi wa Vyama vya Siasa;  Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Wabunge; Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama; Washirika wa Maendeleo; Mabaraza ya Wazee; Wasomi na Wanataaluma;  na Asasi za Kiraia.

 

Hafla hiyo imeambatana na Dua, Utenzi kutoka kwa Bi Amina Mkombe;  Ngoma ya Mwanandege ya Kikundi cha Sanaa cha Jeshi la Polisi Zanzibar, pamoja na Tumbuizo za Bendi za Vikosi vya Ulinzi Nchini,  baada ya Kukagua Maonyesho ya Bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Wazee, kupitia Jumuiya zao.

 

Siku hii inayoadhimishwa ifikapo Tarehe 1 Oktoba ya Kila Mwaka, ilianza kuadhimishwa rasmi mnamo Mwaka 1991, baada ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la Mwaka 1990 kuketi na Kupitisha Azimio  Nambari 45/106 ambalo liliitenga Siku hii Maalum, ili kutambua na kuthamini Mchango wa Wazee Duniani.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, akihutubia wakati wa Hafla ya  Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, katika Ukumbi wa Dokta Shein wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja, Mhe. Othman akimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Mwandishi wetu. Babati 

MICHUANO ya 16 ya Chemchem CUP 2023 ambayo inalenga kupiga vita ujangili wa Twiga imezinduliwa katika eneo la hifadhi ya jamii ya Burunge WMA wilayani Babati mkoa Manyara.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa wilaya ya Babati.Lazaro Twange kwa niaba ya Mkuu wa mkoa, amesema michuano hiyo licha ya kuinua vipaji vya michezo lakini inaendeleza uhifadhi.

Twange amesema vijiji 10 ambavyo vinaunda Burunge WMA,vinapaswa kushirikiana na Taasisi ya chem chem ambayo imeweza shughuli za utalii na uhifadhi katika eneo hilo.

"Tunatarajia nyie muwe mabalozi wazuri wa uhifadhi ,mtowe taarifa za wanaojihusisha na ujangili lakini pia muendelee kunufaika na uhifadhi"alisema

Awali Mkurugenzi wa chemchem association Fabia Bausch alisema michuano hiyo tangu imeanzishwa imejuwa na faida kubwa kushirikisha jamii katika uhifadhi kupitia uhifadhi.

Fabia alisema mwaka huu kwa mara ya kwanza kutakuwa na timu 10 za wasichana na za mchezo wa soka, timu 16 za wanaume na timu 7 za vijana.

Amesema taasisi hiyo imetenga kutimia zaidi ya sh 99.2 million kufanikisha michuano ya mwaka huu.

Awali Mwenyekiti wa michuano hiyo,Elasto Belela amesema maandalizi ya michuano hiyo yamekamilika ambapo timu.zote shiriki tayari zimepewa seti za jezi na mipira kwa maandalizi.

Amesema mshindi wa kwanza atapewa zawadi ya sh 2.5 milioniwa pili 1.5 milioni wa tatu 1 milioni .kwa upande wa wasichana mabingwa watapata 1.5 milioni,mahindi wa pili million Moja na mshindi wa tatu 500,000.

Kwa michezo kwa vijana chini ya miaka 18 mshindi atapata milioni Moja wa pili 600,000 na WA tatu 400,000.


Na Said Mwishehe, Michuzi TV

NI Shanwe tu, !Ndivyo unavyoweza  kuelezea baada ya timu ya Soka ya Simba jijini Dar es Salaam kufanikiwa kuingia hatua ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika kwa kuibuka na matokeo ya jumla ya bao tatu kwa tatu dhidi ya timu y Power Dynamos FC

Simba imecheza na  Power Dynamos FC ya Zambia  katika Uwanja wa Chamazi jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na maelfu ya mashabiki wa soka ndani na nje ya uwanja huo.

Timu ya Power Dynamos FC katika mchezo huo ulioanza saa 10 jioni kwa saa za Afrika Mashariki ilikuwa ya kwanza kupata bao la kuongoza na bao hili lilidumu katika dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili mchezo ulianza kwa kasi na kila timu ikiisoma timu pinzani na kwa upande wa Simba Kocha alimtoa Jean Baleke na kumuingiza John Boco.

Kuingi kwa Boco kuliifanya Simba kuongeza mashambulizi dhidi ya wapinzani wake Power Dynamos FC lakini walinzi wake walikuwa makini kuzuia mashambulizi.

Hata hivyo kadri muda ulivyokuwa ikienda ndivyo Simba walivyoonesha kuwa wanatafuta angalau bao la kusawazisha  na hatimaye mshambuliaji wake John Boco alifanikiwa kupiga mpira ulioingia wavuni baada ya moja ya walinzi wa Power Dynamos kuugusia mpira huo na kuingia wavuni.

Baada ya Simba kupata bao la kusawazisha kila timu ikawa makini kuhakikisha hairuhusu bao lakini wakati huo huo kuangalia uwezo wa kupata bao la kuongeza.

Hata hivyo hadi dakika 90 za mchezo huo zinamalizika matokeo ikawa bao moja kwa moja na Simba imekwenda hatua ya makundi kutokana na matokeo ya jumla .

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Zambia Simba waliifanikiwa kupata mabao mawili akiwa ugenini na Power Dynamos nayo ikipata bao mbili na katika mchezo wa marudiano uliochezaa leo timu hizo zimefungana bao 1-1 na kuifanya Simba kuingia hatua ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa.

Kwa matokeo hayo Simba  inaungana na watani wake wa jadi Yanga ambao tayari wameingia hatua ya makundi baada ya kupita miaka 25 kwani mara ya mwisho iliingia hatua hiyo mwaka 1998.

Hata hivyo katika mchezo wa Simba na Power Dynamos  ulikuwa umetawaliwa na mbinu nyingi za mchezo na hivyo kusababisha makocha wa timu zote mbilii kuusoma mchezo huku wakibadilsha wachezaji kulingana na mbinu  za kupata matokeo kadri muda ulivyokuwa ukisonga mbele.





Iringa

Timu ya Mpira wa miguu ya TARURA yaendeleza ubabe kwa siku tatu mfululizo ambapo Leo imefanikiwa kuipiga Ardhi goli 1-0 kwenye mashindano ya SHIMIWI.

Katika mchezo wa Leo uliochezwa kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Mkwawa,TARURA ilifanikiwa kuona goli la ardhi katika kipindi cha kwanza dakika ya 28 ambapo mchezaji Erick Tegamaisho aliipatia goli la ushindi.

Hadi mwisho wa mchezo huo timu ya Ardhi haikufanikiwa kuliona goli la TARURA licha la mchezaji wa TARURA Makunge Mwera kupewa kadi nyekundu.

Hadi Leo TARURA inaongoza kwa kuwa na point 9 na magoli  8 ambapo katika mechi ya kwanza dhidi ya Wakili Mkuu iliibuka kidedea kwa magoli 4-0 na katika mechi ya pili dhidi ya Wizara ya Elimu ilitoka mshindi kwa 3-2.









Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow, akizungumza na waandishi wa habari katika Mgodi wa North Mara juzi kuhusu athari chanya za ubia wa kimageuzi katika uchimbaji madini kwa kushirikiana na Serikali kupitia kampuni ya Twiga. Kushoto ni Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido.

Mkuu wa Wilaya, Tarime, Michael Mtenjele, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari katika Mgodi wa North Mara kuhusu mipango ya kuimarisha ulinzi na usalama katika Mgodi wa North Mara baada ya kukutana na Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow.

Mbunge wa Tarime vijijini, Mwita Waitara akiongea katika mkutano huu.

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow, akimkabidhi ufunguo wa gari Mkuu wa Wilaya Mara, Michael Mtenjele (kulia) lililotolewa na Barrick kwa ajili ya kusaidia ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa kwa fedha za CSR za mgodi wa North Mara katika Halmashauri ya Wilaya hiyo wakati wa hafla hiyo.

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick,Mark Bristow, akizindua Kamati mpya ya Maendeleo ya Jamii (CDC) ya Halmashaurin ya wilaya ya Tarime ambayo kwa sasa Mwenyekiti wake mpya ni Diwani wa Kata ya Matongo, Godfrey Kigoye.

Viongozi wa mila kutoka koo zote za kabila la Wakurya wakimpatia Rais na CEO wa Barrick, Mark Bristow, zawadi ya beberu la mbuzi ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa kampuni hiyo kwa maendeleo ya wananchi wa Tarime.


Kampuni ya Dhahabu ya Barrick na serikali ya Tanzania zimedhihirisha jinsi uchimbaji madini unavyoweza kuwa na manufaa makubwa pale wachimbaji madini na serikali wenyeji wanaposhirikiana katika kuleta thamani endelevu kwa wadau wote, anasema Rais na Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Mark Bristow.


Akizungumza na vyombo vya habari mwishoni mwa wiki , Bristow alisema ubia ulioanzishwa na Barrick na Serikali uliyoiunda Kampuni ya Twiga ambamo pande zote mbili zinagawana kwa usawa faida za kiuchumi zinazotokana na migodi ya North Mara na Bulyanhulu, unapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa ni ubia wenye mafanikio makubwa, hasa katika nchi zinazoendelea. Aidha, si tu kwamba Barrick sasa ndiyo mchangiaji mkubwa zaidi katika uchumi wa Tanzania kupitia kodi, mishahara, gawio, malipo kwa wasambazaji wa ndani, na uwekezaji katika miradi ya jamii, bali pia kampuni hiyo imethibitisha kwa makampuni mengine ya kimataifa ya madini kuwa nchini humu kunawekezeka.


Tangu mwaka 2019 ilipoichukua migodi hiyo miwili iliyokuwa imekufa, Barrick imeibadilisha na kuifanya kuwa ya kiwango cha kimataifa na hivyo, kutoa mchango mkubwa katika faida halisi ya kampuni. Aidha, katika kipindi hicho, kampuni hiyo imechangia zaidi ya dola bilioni 3 katika uchumi wa Tanzania, huku mwaka huu Twiga ikitambuliwa kuwa mlipaji mkubwa wa gawio kuliko makampuni yote ambayo serikali ina maslahi nayo. Migodi ya Barrick hutumia asilimia 84 ya bajeti yake ya manunuzi kwa makampuni ya ndani huku asilimia 96 ya nguvukazi yao ikiwa ni wananchi wa Tanzania.


Kwa moyo huo huo wa ushirikiano, Barrick imetoa dola milioni 40 kwenye mpango wa ujenzi wa barabara na dola milioni 30 zaidi katika uboreshaji wa suhula za elimu ya juu nchini.






Migodi yote miwili iko katika mwelekeo mzuri wa kuufikia mwongozo wake wa uzalishaji wa mwaka 2023 na utafutaji wa madini pia. Kwa sasa, utafutaji madini katika maeneo yote ya Barrick yaliyopewa leseni umeonesha fursa mpya za maendeleo katika maeneo hayo, ikiwa ni pamoja na uwezekano wa mgodi mpya wa chini ya ardhi huko North Mara.


“Ubia wetu wa Twiga si tu kwamba unaongeza thamani katika uchumi wa Tanzania bali pia katika ubora wa maisha ya jamii zinazoizunguka migodi yetu na ambayo iaendelea kustawi. Kuendelea kwetu kujihusisha na jamii hizi na viongozi wao wa vijiji, AZISE za maeneo hayo pamoja na mashirika ya haki za binadamu kunaonesha falsafa ya Barrick ya ubia na dhamira yetu ya dhati ya kuzingatia haki za binadamu katika maeneo tunayofanyia kazi,” alisema Bristow.


Bristow pia alikabidhi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime (Vijijini) gari aina ya Toyota Land Cruiser lililotolewa na Barrick kwa ajili ya ufuatiliaji wa miradi ya kijamii inayotekelezwa kutokana na fedha za katika Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) zinazotolewa na Mgodi wa Barrick North Mara. Mgodi wa North Mara kwa sasa unatekeleza miradi zaidi ya 100 ya CSR mkoani Mara.


Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kanali Michael Mntenjele, alisema gari hilo ni muhimu katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya CSR kutoka Barrick unaenda vizuri.


Tunashukuru Barrick kwa gari hili, litasaidia wataalamu wetu kufika kwenye miradi kwa wakati na miradi kutekelezeka kwa wakati, ili iweze kunufaisha wananchi wetu,” alisema Kanali Mntenjele.


Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara umetumia zaidi ya shilingi bilioni saba kugharimia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kijami kupitia mpango huo wa CSR katika vijiji vyote 88 vya halmashauri ya Wilaya ya Tarime, ambapo asilimia 70 ya kiasi hicho cha fedha kikienda kwenye vijiji vinavyouzunguka.


Katika hafla hiyo, viongozi wa mila kutoka koo zote za kabila la Wakurya walimpatia Rais na CEO wa Barrick, Bristow, zawadi ya beberu la mbuzi ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa kampuni hiyo kwa maendeleo ya wananchi wa Tarime.

Top News