Maurel & Prom (M&P) was among the sponsors of this 5th edition of the Tanzania Energy Congress, themed: ‘Investing in Tanzania’s sustainable energy economy’ held on 20-21st September 2023, under the patronage of the honourable Dr. Dotto Mashaka Biteko (MP), Deputy Prime Minister and Minister of Energy. 

M&P Tanzania’s operations began in Tanzania almost twenty years ago. The company is essentially known for its work in the Mnazi Bay natural gas field located at the south of the country next to Mtwara, and also owns a 60% stake in BRM licence and the Mkuranga discovery.

The recent years have seen M&P together with its partners Wentworth and TPDC upgrade the capacity of the Mnazi Bay field by more than 60% in response to the increasing Tanzanian demand, thanks to significant projects and well interventions implemented successfully; this was carried out with an excellent track record of no LTIs (lost time injury) in 7 years and an overall reliability of our operation above 99.9%.

As a further illustration of M&P’s story and commitment to Tanzania’s growth and development, the company announced on 5 December 2022 a proposed amicable takeover of Wentworth Resources PLC, an operation which still needs to obtain approvals from government authorities.

Reflecting on the Energy Congress, Nicolas Engel, M&P General Manager, highlighted the significance of such platforms, enabling stakeholders to come together with a shared vision and actively contribute to the advancement of Tanzania's energy sector. 

Speaking about the company's nearly 20-year history as a pioneer and leader in gas development in Tanzania, he stated, “Tanzania holds a good position in some of M&P's most impactful projects. 

With a contribution of around 35% to the Tanzanian energy demand, our operation is key to the country and we take our role of operator and all associated responsibilities very seriously. Our ongoing projects and growing strategy further illustrates M&P’s wish to commit on the long-term and to continue providing gas supply in support of the electrification and industrialization of the country"  

Last but not least, M&P Tanzania strives to procure goods and services locally wherever possible, highlighting their commitment to boosting the economy, creating job opportunities and stimulating the various industries in Tanzania. 

Through CSR initiatives, M&P Tanzania also supports local economic activity, investing in education and providing access to quality education and skill development programs. The organization also works towards improving access to clean water, promoting health care, supporting sports engagement for youth, and creating awareness campaigns for environmental conservation. 

M&P continues to support the growth and development of Tanzania through its commitment to providing a reliable and cost-effective gas supply and sustaining economic growth.







Baadhi ya  vijana wakiwa katika picha ya pamoja kuadhimisha siku ya Amani duniani
Naibu meya wa Jiji la Dar es Salaam,Ojambi Masaburi Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya siku ya Amani duniani yaliyofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja kushirikisha vijana wa nchi za maziwa makuu.
Vijana wa nchi za maziwa makuu wakiwa katika matembezi ya Amani katika viwanja vya mnazi mmoja ikiwa ni Maadhimisho ya siku ya Amani duniani.

Na Mwandishi wetu
VIJANA katika nchi zinazozungukwa na maziwa makuu wamewataka kuacha kutumika katika vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani ambavyo kwa kiasi kikubwa vina athari kwao na nchi zao kwa ujumla.

Akizungumza Jana jijini Dar es Salaam ,Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam Ojambi Masaburi wakati akipokea matembezi ya kuadhimisha siku ya amani dunia yaliyofanywa na vijana kutoka nchi za maziwa makuu ambazo ni Demokrasia ya Congo(DRC), Uganda, Tanzania, Rwanda na Burundi.

Masaburi amesema ni muhimu vijana kuacha kushabikia mambo yasiyokuwa ya msingi ambayo yanaweza kuleta machafuko na uvunjifu wa amani huku akiwataka wayasema yale mema ya serikali na kutoa ushauri pale unapohitajika kufanya hivyo.

“Bila kuwa na amani hatuwezi kuwa na maendeleo, amani inapotea tunapoteza ndugu, baba, mama na watoto pamoja na watu wenye mahitaji maalum kwa maana ya walemavu,” amesema Masaburi na kuongeza.

“Kwa mujibu wa takwimu za dunia zinaonesha kuwa zaidi ya vijana Bilioni 1.4 duniani wanaishi katika maeneo au nchi zenye mchafuko na wanawake 600,000 ambao nao wanaishi kwenye nchi zenye machafuko, hizi zi takwimu nzuri,” amesema

Naye Ofisa Maendeleo ya Vijana wa jiji la Dar es Salaam, Happness Joackim amesema kupitia maadhimisho hayo wanawahimiza vijana hususani waliopo katika nchi ambazo zinazungukwa na maziwa makuu kulinda na kutunza amani za nchi zao.

Amesema vijana wasikubali kujiingiza katika machafuko ya kikabila, kisiasa au ya nchi na nchi kwa sababu kuingia katika migogoro hiyo kutaleta matatizo mengi ikiwemo kupoteza ndugu, jamaa na marafiki huku kundi kubwa linaloathirika ni watoto, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake Mratibu wa Taifa wa Mtandao wa vijana wa nchi za maziwa makuu kuhusu Amani na Utulivu .Jimmy Luhende amesema kongamano hilo la siku tatu limeweza kuwakusanya vijana hao na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kupanga mijadala ya kumaliza migogoro mbalimbali katika nchi zao na kudumisha amani.

Amesema tofauti zinapotokea ikiwemo kupeleka majeshi,kutunishiana misuli katika nchi hizo za maziwa makuu haziwezi kuleta amani na wala kuwa suluhisho.

Aidha Katibu wa Asasi ya Vijana Youth VDT,Nicholus Luhende amesema kwa mara ya kwanza kuanza kwa kongamano hilo lilianza nchini Congo,Kigali,Uganda na sasa Tanzania lengo ikiwa ni kuwakutanisha vijana kutoka nchi hizo kujadili masuala ya amani.

''Nchi ambazo zinatuzunguka Tanzania zimekuwa na changamoto mbalimbali katika masuala ya amani hivyo kongamano hili limetupa nafasi ya kukaa pamoja na kujadili kwani kupitia maongezi itaweza kutatua matatizo yaliyopo,''amesema.
Kaimu Mkurugenzi Uzingatiaji na utekelezaji wa sheria Baraza la uhifadhi na utunzaji Mazingira Dk. Thobias Mwesiga akimpa maagizo meneja wa Kiwanda Cha Chanzi kinachozalisha Funza
Meneja wa Kiwanda Cha Chanzi kilichopo mkoani Arusha Mayasa Mhina akieleza shughuli zinazofanyika Kiwandani hapo ikiwa ni pamoja na uzalishaji wa funza kwa ajili ya chakula Cha mifugo
Taka ozo zilizoandaliwa Kwa ajili ya kuanza mchakato wa uzalishaji Funza.

Na Jane Edward, Arusha
NEMC yampa siku Saba mmiliki wa Kiwanda Cha Kuzalisha chakula Cha mifugo Kwa kutumia taka laini kudhibiti harufu Kali itokanayo na taka hizo jambo ambalo limekuwa kero Kwa wakazi waishio eneo linalozunguka Kiwanda hicho.

Agizo hilo limeitolewa na Kaimu Mkurugenzi Uzingatiaji na utekelezaji wa sheria NEMC Dk. Thobias Mwesiga alipotembelea Kiwanda hicho kilichopo mkoani Arusha ambapo amemtaka mwekezaji huyo kuhakikisha wanatafuta mbinu mbadala wa kuzuia harufu kusambaa na kusababisha kero Kwa wakazi wanaoishi maeneo yanayozunguka Kiwanda hicho.

"Hatuna nia ya kufungia Kiwanda hiki lakini lengo letu tunapaswa kutoa elimu na hivyo basi tulipokea malalamiko kutoka kwa wananchi wanaoishi maeneo haya kwamba harufu kali inayosababishwa na shughuli zinazotekelezwa hapa imekuwa kero kwao, hivyo tukatumwa na Waziri anayesimamia Shughuli za Mazingira Ili kuja kutembelea na kukagua shughuli hizo, tumejionea Sasa natoa siku Saba kudhibitiwa Kwa harufu hii"

Lengo la NEMC siyo kuwakwamisha Wawekezaji bali ni kuona mwekezaji ana
tekeleza shughuli zake Kwa kufuata sheria na tumeona kwamba kiwanda hiki kinafanya kazi ya kubadilisha taka laini (muozo) kuwa bidhaa hili ni jambo jema, lakini hatutaki kuona mnatoa tatizo moja sehemu flani na kulihamishia mahali pengine Kuzalisha tatizo jingine, kama mmehamua kufanya hivyo maana yake mje na mbinu mbadala ya kudhibi hii harufu" alisema.

Dk. Mwesiga alisema endapo siku Saba zitatimia Kiwanda hicho kikiwa bado kinalalamikiwa au kushindwa kutimiza sheria na kanuni za Mazingira ni dhahiri kuwa kitachukuliwa hatua Kali ikiwemo kupigwa faini pamoja na kufungiwa kufanya uzalishaji.

Aliitaka halmashauri ya Jiji la Arusha kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa eneo la Mwekezaji huyo Ili aweze kuhamisha Kiwanda hicho na kukipeleka mbali na Makazi ya binadamu Ili kuweza kufanya shughuli zake Kwa uhuru.

Naye Ofisa Mazingira Jiji la Arusha Sigfrid Mbuya alisema tayari mwekezaji huyo alishapeleka Mapendekezo (Proposal) ya kuomba eneo la kujenga Kiwanda kikubwa Kwa kuwa eneo walililopo Kwa Sasa limekuwa dogo na Ili kuondoa kero kwa wakazi wa maeneo hayo ambapo alisema wataalamu wa Jiji walishapitia mapendekezo hayo na kilichobaki ni kupitishwa kwenye vikao vya Jiji Ili kupatiwa Eneo hilo.

" Waliomba Eneo lililotengwa kwa ajili ya dampo Ili kuendesha shughuli zao Kwa uhuru hivyo tulishapitia mapendekezo hayo na imebaki kupita kwenye vikao vya halmashauri waweze kupatiwa maeneo hayo, lakini pia hiki Kiwanda kinafanya kazi ya kubadili taka jambo ambalo ni teknolojia ya maana, kama Kwa siku zinakusanywa taka zaidi ya tani 100 lakini hapa wanauwezo wa kuchukua taka tani 30 maana yake ni teknolojia ya maana ,hivyo ni namna tu ya kuweza kukamilisha taratibu zinazotakiwa na kuendelea na uzalishaji " alisema.

Naye meneja shamba wa Kiwanda hicho Mayasa Mhina alisema walishafanikiwa kudhibiti harufu hiyo lakini tatizo limejitokeza pindi umeme ulivyoanza kuwa wa mgao.

"Tumefanikiwa Kwa kiwango kikubwa kudhibiti harufu Katika uzalishaji wetu lakini tangu umeme uanze kukatika mara Kwa mara ndipo tatizo lilipoanzia hapo, lakini umeme ukirudi tu kazi ya kuondoa hizi taka inaanza lakini pia Huwa tunatumia vumbi la mkaa kudhibiti harufu"alisema Mhina.

Kiwanda hicho huchakata taka laini na Kuzalisha funza kwa ajili ya kutengeneza chakula Cha mifugo (protein ya mifugo) pamoja na mbolea.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh. Kisare Makori Akiongea na Timu ya Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu waliofika katika Wilaya yake kwaajili yakutoa elimu ya Kodi kwa  Wafanyabiashara wa Mkoa wa Kilimanjaro.Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mh. Kisare Makori Akiongea na Timu ya Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu waliofika katika ofisi zake kwa ajili ya kujitambulisha kabla ya kuanza kwa kwa zoezi la kutoa Elimu ya Kodi ya Mlango kwa mlango kwa Wafanyabiashara wa Mkoa wa Kilimanjaro


Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kisare Makori amesema kuwa anakumbuka kauli ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo amewataka maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kukusanya kodi bila vitisho na hilo linajidhihirisha kwa kusema kuwa siku hizi TRA ni rafiki sana na wafanyabiashara na hilo ni jambo jema na lenye kudumisha uzalendo wa ulipaji kodi wa hiari.

Ameyasema hayo mwanzoni mwa wiki katika ofisi yake iyopo Moshi wakati alipotembelewa na maafisa kutoka TRA Makao makuu walipofika katika ofisi yake kwa ajili ya kujitambulisha kabla ya kuanza ya zoezi la Elimu ya kodi Mlango kwa Mlango kwa wafanyabiashara wa Moshi sambamba na kusikiliza changamoto zao ili waweze kuzifanyia kazi.

Makori amesema kuwa anafurahia kuwepo kwa elimu ambayo itawafikia wafanyabiashara moja kwa moja katika maeneo yao ya biashara na kuwataka wafanyabiashara hao kushirikiana na maafisa wa TRA ili kufikia lengo lilokusudiwa.

“Natoa pongezi kwa hatua waliyofikia Maafisa wa TRA ya kukusanya kodi bila Mitulinga kama maagizo ya Mh. Rais yalivosema kwaajili ya faida ya Nchi yetu na maendeleo ya Taifa letu, pia kama tujuavyo Serikali haina biashara yoyote isipokua kodi, hivyo utoaji wa elimu ni hatua kubwa sana na itaongeza “sovereignty” na uwezo wakulipakodi utaongezeka.”

Nae kiongozi wa zoezi hilo, Afisa Mkuu Elimu kwa Walipakodi na Mawasiliano Lydia Shio kutoka TRA Makao Makuu amesema uwepo wa maafisa ni kutoa elimu ya kodi na kusikiliza changamoto zao ambazo hata wao wanashindwa kuzileta katika ofisi zao hivyo wameamua kuwafata katika maeneo yao ili kujua uhalisia wa biashara zao na kuwakumbusha malipo ya kodi kwa hiari.

“Tumekuja kwa lengo la kutoa elimu kwa Walipakodi na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kilimanjaro tukianzia na Wilaya ya Moshi Mjini ili kuwakumbusha walipakodi waweze kujua wajibu wao wa kulipa kodi kwa wakati kwaajili ya kuongeza pato la Taifa, wafanyabiashara wengi wamesema kua huko nyuma walikua wakiwaona maafisa kutoka TRA wanawakimbia na hawajui wanakimbia kwa kosa gani ila kwa sasa hawana haja ya kukimbia maana tukifika wanatusikiliza na kufanya kilichotuleta na wao wanauliza maswali na kuwasilisha changamoto zao kwa ufafanuzi Zaidi ili aweze kulipakodi inavotakiwa”

Mmoja wa wafanyabiashara wa mtumba katika eneo la soko kuu la Memorial Betty Urono ameeleza kuwa yeye anatumia machine ya risiti na inamsaidia sana na angependa kuwaona wafanyabiashara wenzake wanatumia pia ili kulipakodi kwa usahihi na kujenga taifa letu na maendeleo ya nchi.

“mimi natumia machine ya risiti EFD ni nzuri na inasaidia sana katika kutunza kumbukumbu zetu ni nzuri katika bishara yangu, mimi natoa risiti na nawaomba wengine pia watoe risiti kwa faida yao na ya Nchi yetu pia.”

Mkoa wa Kilimanjaro umekua ni moja wapo ya mkoa wenye historia nzuri katika ulipaji na ukusanyaji kodi na kufikia malengo na muendelezo wa gurudumu la kuongeza pato la Taifa na maendeleo kiujumla hii ni kutokana na ushirikiano unaopatikana kutoka kwa wafanyabiashara na taasisi ya TRA ya Mkoa wa Kilimanjaro katika kutimiza malengo ya Serikali yetu katika kuendeleza maendeleo ya Mkoa na Nchi kiujumla.

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV

KATIBU Mkuu Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla amesema, Serikali imetoa kipaumbele kwa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kuendeleza uchumi wa kidigitali.

Uchumi wa Kidijitali serikali imewekeza fedha nyingi kwenye mkongo wa Taifa wa Mawasiliano hivyo wananchi wanahitaji huduma kwenye mkongo huo na kuona shirika hilo likifanya kazi yake kwa ufanisi unaotakiwa ili kutekeleza majukumu waliyonayo.

Abdulla ameyasema hayo jijini Dar es Salaam, mara baada ya kukagua vifaa vya mradi vitakavyotumika katika upanuzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano awamu ya tatu sehenu ya pili.

Amesema Serikali imemwamini Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Mhandisi Peter Ulanga na ndio maana imemkabidhi kituo cha data na mkongo wa taifa kwa lengo la kuvifanyia kazi.

Katibu Mkuu huyo amesema mradi huo unatakiwa kumalizika kwa wakati kwa lengo la kuleta tija kwa wananchi kwa sababu fedha zinazotumika ni za watanzania.

Hata hivyo amesema taasisi za serikali ambazo hazijaingia Kituo cha Data ziingie kwani nafasi zipo za kutosha

“ Sitaki stori nyingi kwenye mradi huu nataka utekelezaji wa kazi na kazi lazima ifanyike kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa na mkandarasi ,”amesema Abdulla.

Hata hivyo katika ziara hiyo Katibu Mkuu alizihimiza Wizara na taasisi zingine ziweke taarifa zake katika kituo cha data cha TTCL.

Aidha aliwataka wakandarasi wa mradi huo wafanye wajibu wao kama mkataba wao ulivyotaja ili wananchi waweze kuanza kupata huduma hiyo kwa kutumia mkongo wa taifa

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Mhandisi Ulanga alisema Shirika hilo linaunga mkono juhudi za Serikali katika kuhakikisha wilaya zote nchini zinaunganishwa na mkongo wa Taifa.

Mhandisi Ulanga alisema mradi wa awamu ya tatu unakwenda kutekeleza Wilaya 32, ambapo Wilaya 23 ziko chini ya Mkandarasi na Wilaya nyingine Tisa (9) ziko chini ya TTCL.

“Magari 44 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi yameshapatikana na tayari yanatumika kwenye shughuli hizi ili kuongeza ufanisi zaidi katika mradi huo”,alisema

Mhandisi Ulanga alimuakikishia Katibu Mkuu kuwa, Menejimenti yake itasimamia miradi hiyo kwa ukamilifu,kwa weledi,pamoja na kukamilika kwa wakati .

“ Wasimamizi wa Mradi hakikisheni mnasimamia mradi kwa ukamilifu na kwa weledi. Changamoto zitakazojitokeza tafadhali ziwasilisheni mapema katika Menejimenti ili tuweze kuzifanyia kazi kwa ukaribu na haraka”,amesema.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari  Mohammed Khamis Abdulla  akipata maelezo kutoka Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Mhandisi Peter Ulanga wakati Katibu  Mkuu huyo alipitembelea na Kukagua vifaa  kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano  wa awamu ya tatu sehemu ya pili , jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari  Mohammed Khamis Abdulla akizungumza mara baada ya  Kukagua vifaa  kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano  wa awamu ya tatu sehemu ya pili , jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Mameneja wa kusimamia ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano
Sehemu picha ya mkandarasi wa kujenga sehemu ya mradi wa ujenzi Mkongo wa Taifa wa Mawsiliano jijini Dar es Salaam.
 

 

Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imesaini kandarasi ya mfumo wa usimamizi wa taarifa za anga na Kampuni ya Indra Avitech GmbH kwa ajili ya kuboresha usalama wa safari angani katika anga ya Tanzania kupitia utoaji wa taarifa za anga zenye ubora wa hali ya juu, salama na muhimu kwa wakati sahihi kwa wadau mbalimbali wa usafiri wa anga.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari leo Mamlaka hiyo imesaini mkataba wenye thamani ya Shilingi Bilioni Tisa kwa ajili ya kubuni, kusambaza, kusanikisha, kuunganisha, na kuzindua Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Anga ambapo Mradi huu utatekelezwa kwa miezi 18.

Amesema sehemu ya mpango thabiti wa Usimamizi wa Taarifa za Anga (AIM) wa kuboresha mfumo wake wa taarifa za anga kwa kutoa usimamizi wa taarifa za anga kwa njia ya kisasa zaidi kwa kutoa na kubadilishana taarifa za anga za dijitali zenye ubora na kushirikiana na pande zote hivyo kuhakikisha usalama, utaratibu, na ufanisi wa urambazaji wa anga wa kitaifa na kimataifa.

“Lengo la utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Anga ni kuboresha mfumo wa AIM katika kuboresha usahihi wa data, upatikanaji, na ufanisi kwa kuzingatia mahitaji ya Upandishaji wa Mfumo wa Anga wa Usafiri (ASBU), na kufuata viwango vya kitaifa na kimataifa.” Alisema Johari
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Hamza Johari (katikati) akisaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9. Bw. Simon Masike alisaini kwa upande wa kampuni ya Indra Avitech. Hafla hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya TCAASeptemba 22, 2023.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Hamza Johari (katikati), Mkurugenzi Huduma za Sheria TCAA,  Maria Makala (wa pili kulia), Mwakilishi wa Kampuni ya Indra Avitech , Bw. Simon Masike(wa pili kushoto) wakisani Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9 iliyofanyika Makao Makuu ya TCAA Septemba 22, 2023.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Hamza Johari (wa pili kushoto) akikabidhiana mkataba na Mwakilishi wa Kampuni ya Indra Avitech, Bw. Simon Masike mara baada ya kusaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9 iliyofanyika Makao Makuu ya TCAA Septemba 22, 2023. Mkurugenzi Huduma za Sheria TCAA,  Maria Makala (wa pili kulia).

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Hamza Johari (katikati) pamoja na Mwakilishi wa Kampuni ya Indra Avitech, Bw. Simon Masike ( wa pili kushoto) wakionesha mkataba mara  baada ya kusaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9 iliyofanyika Makao Makuu ya TCAA Septemba 22, 2023.Wa pili kulia ni Mkurugenzi Huduma za Sheria TCAA,  Maria Makala 

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Hamza Johari (katikati) akizungumza wakati wa kusaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9 iliyofanyika Makao Makuu ya TCAA Septemba 22, 2023. 


Mwakilishi wa Kampuni ya Indra Avitech, Bw. Simon Masike  akizungumza wakati Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) waliposaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9 iliyofanyika Makao Makuu ya TCAA Septemba 22, 2023. 


Kaimu Mkurugenzi Wa Huduma Za Uongozaji Ndege TCAA, Hamis Kisesa akizungumza wakati Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) waliposaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga na Kampuni ya Indra Avitech wenye thamani ya Tsh. Bilioni 9 iliyofanyika Makao Makuu ya TCAA Septemba 22, 2023.

Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti Uchumi TCAA,Bw. Daniel Malanga(katikati), Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka Bw. Teophory Mbilinyi (kushoto) na Mkurugenzi Huduma za Sheria TCAA,  Maria Makala wakiwa kwenye hafla ya kusaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga. 

Meneja Uhusiano na Mawasiliano TCAA, Yessaya Mwakifulefule(kushoto), Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) kinachomilikiwa na TCAA, Aristid Kanje (katikati) na Afisa Mtoa Taarifa za Anga Mwandamizi (TCAA) wakiwa kwenye hafla ya kusaini Kandarasi ya Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga. 

Baadhi ya wadau mbalimbali wa uSafiri wa anga wakiwa kwenye hafla ya kusaini Kandarasi ya Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Utoaji wa Taarifa za Anga. 
Picha za pamoja 

 

BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza kuhusu dhamira yake ya kufanikisha ustawi wa biashara baina ya Tanzania na Afrika kusini kwa kuwawezesha wafanyabiashara wa mataifa hayo mawili ili waweze kupanua zaidi biashara zao sambamba na kuchangamkia fursa zaidi nje ya mipaka ya nchi hizo kufuatia hatua ya Umoja wa Africa kujumuishwa kuwa mwanachama wa kudumu katika muungano wa Umoja wa bara Ulaya G-20.

Dhamira hiyo imewekwa bayana na Mkurugenzi wa Hazina na Masoko ya Fedha wa Benki ya NBC Bw Peter Nalitolela wakati akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw Theobald Sabi kwenye Mkutano wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania uliofanyika jijini Dar es Salaam jana jioni ukihudhuriwa pia Balozi wa Afrika Kusini hapa Tanzania Bi Noluthando Malepe.

Kwa mujibu wa Bw Nalitolela, kupitia huduma zake mbalimbali za kifedha ikiwemo mikopo ya ukuzaji mitaji, dhamana, huduma ya fedha za kigeni sambamba na huduma ya malipo kwa njia ya mtandao inayofahamika kama ‘NBC Connect’ benki hiyo imedhamiria kurahisisha zaidi ufanisi wa biashara kwa wafanyabiashara wa mataifa hayo ili waweze kushiriki kwa ushindani zaidi kwenye fursa hiyo mpya ya kimataifa.

“Tumefurahi kuona kwamba Mheshimiwa Balozi wa Afrika Kusini hapa Tanzania Bi Noluthando Malepe nae amewasisitiza wafanyabiashara kuchangamkia soko hili jipya la G -20 nasi NBC pia tunawathibitishia kuwa tupo tayari Kwenda nao bega kwa bega kufanikisha hili kupitia huduma zetu muhimu za kifedha ambazo zimebuniwa mahususi kurahisha mahitaji yao ikiwemo mikopo, dhamana, upatikanaji wa fedha za kigeni na zaidi huduma yetu ya malipo kwa njia ya mtandano yaani NBC Connect itakayowawezesha kufanya mihamala mbalimbali yakiwemo malipo ya serikali na tozo mbalimbali’’ alitaja.

Alisema kwa muda mrefu sasa benki hiyo imekuwa mdau mkubwa wa wafanyabiashara kati ya Afrika Kusini na Tanzania ambapo kupitia mkutano huo uliodhaminiwa na benki ya NBC, alitaja baadhi ya sekta zinazotazamwa zaidi na benki hiyo kuwa ni pamoja na sekta za kilimo, usafirishaji, mawasiliano, biashara na madini.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo Balozi Noluthando Malepe aliitaja Tanzania kama moja ya nchi bora zaidi kwa uwekezaji kutokana na uwepo wa fursa nyingi za kibiashara huku akitaja uwepo wa amani nchini Tanzania pamoja na ushirikiano wa kihistoria uliodumu kwa muda mrefu baina ya Tanzania na Afrika Kusini kama nguzo muhimu katika kufanikisha ustawi wa biashara baina ya mataifa hayo mawili.

“Hivyo nawaomba sana muitumie vema fursa hii ya amani na ushirikiano tuliona nao na wenzetu wa Tanzania kustawisha biashara zenu. Popote mnapohisi kuna changamoto tunawakaribisha ofisi za ubalozi ili tuweze kujadili namna bora ya kuzitatua huku pia tukijadili fursa nyingine zaidi,’’ aliomba Balozi Malepe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania, Bw Manish Thakrar alisema pamoja na mambo mengine, nia ya jukwaa hilo ni kuunga mkono jitihada za serikali katika kuvutia wawekezaji wengi zaidi kutoka nje ya nchi kuja kuwekeza nchini Tanzania, huku akitaja suala la upatikanaji wa huduma za kifedha za uhakika kama moja nguzzo muhimu katika kufanikisha agenda hiyo.

“Hata hivyo Habari njema ni kwamba ushirikiano wetu na benki ya NBC uliodumu kwa muda mrefu sasa umeendelea kutuhakikishia upatikanaji wa huduma bora za kifedha. Tumefarijika zaidi kusikia kwamba NBC wanaendelea kutuhamasisha kuhusu ushiriki wetu kwenye soko la G-20 huku wakituhakikisha ufanisi zaidi kwenye upatikanaji wa mitaji zaidi na huduma nyingine nyingi za kifedha,’’ alisema Bw Thakrar ambae pia lionyesha kuvutiwa zaidi na huduma ya malipo ya mtandao ya NBC Connect.

Mkurugenzi wa Hazina na Masoko ya Fedha wa Benki ya NBC Bw Peter Nalitolela akizungumza na wajumbe wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania wakati wa mkutano wa jukwaa hilo ulifanyika jijini dar es salaam jana.

Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania Bi Noluthando Malepe (alieshika kipaza sauti) akizungumza na wajumbe wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania wakati wa mkutano wa jukwaa hilo ulifanyika jijini dar es salaam jana. Wanaomsikiliza ni Pamoja na Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bw Manish Thakrar (kushoto kwa balozi) pamoja na Mkurugenzi wa Hazina na Masoko ya Fedha wa Benki ya NBC Bw Peter Nalitolela (kushoto kwa Mwenyekiti)

Mkurugenzi wa Hazina na Masoko ya Fedha wa Benki ya NBC Bw Peter Nalitolela (Kushoto) akibadilishana mawazo na baadhi ya viongozi waandamizi  wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania wakati wa mkutano wa jukwaa hilo ulifanyika jijini dar es salaam jana.

Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania Bi Noluthando Malepe (wa tatu kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo  Bw Manish Thakrar pamoja na  maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa Hazina na Masoko ya Fedha wa Benki ya NBC Bw Peter Nalitolela (wa tatu kushoto) wakati wa mkutano wa jukwaa hilo ulifanyika jijini dar es salaam jana.


Na Mwandishi Wetu-Kilosa

Zaidi ya shilingi Bilioni 11 zimeongezwa na Serikali kuanzia mwaka wa fedha 2021/22 kutoka Bilioni 1.097 hadi kufikia Bilioni 12 kwa ajili ya matengenezo na ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja.

Fedha hizo ni sehemu ya kuhudumia mtandao wa barabara zenye urefu wa Km 913.67 zinazosimamiwa na Wakala ya Barabara ya Vijijini na Mijini (TARURA) Wilayani Kilosa.

Hayo yamesemwa na Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilosa Mhandisi Harold Sawaki wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa daraja la Ruhembe lenye urefu wa mita 40 itakayogharimu Shilingi Bilioni 1.28 pamoja na kufungua barabara yenye urefu wa Km 2 inayoingia darajani hapo kuunganisha Kata ya Ruhembe na barabara kuu ya Mikumi - Ifakara itakayogharimu Shilingi Milioni 203.

Miradi hii ikikamilika itaenda kuondoa kero ambazo walikuwa wakizipata hapo awali ikiwemo kuwafikisha kwenye barabara pamoja na mahitaji ya kijamii.

“Daraja hili ni kubwa na litaenda kuondoa kabisa kero za wananchi wa kata ya Ruhembe na kuongeza Wakazi hao hawakuwa na njia ya kuwafikisha barabara kuu na hivyo kukosa mahitaji muhimu ya kijamii.

"Wananchi hao ambao ni wakulima wa miwa walikuwa wanapata shida ya kuuza miwa yao na hivyo kupata hasara kubwa “.

Aidha, amesema kwa upande wa ujenzi wa daraja la Berega lenye urefu wa mita 140 linalogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 7.9 kwamba mradi huo unaendelea vizuri na upo katika hatua za mwisho za umaliziaji .

"Tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuweza kuongeza bajeti ya fedha na hivyo tunaenda kukamilisha mradi wa daraja kubwa la Berega.

Mhandisi Sawaki ameongeza kusema kuwa kufunguliwa kwa barabara yenye Km 42 ambayo inaunganisha Kata ya Ulaya na Kisanga ambapo kuna kituo cha bomba kuu la kusukuma mafuta kutoka Tanzania kwenda Zambia na hivyo kuwa msaada mkubwa na kuwezesha kuungana na barabara kuu inayoanzia Dumila, Kilosa hadi Mikumi.

“Hii tunaona dhamira kuu ya Serikali ya Awamu ya Sita namna ilivyodhamiria kuondoa kero za wananchi kwa kufungua barabara mbalimbali ambazo zilikuwa zimefungika na kukata mawasiliano katika pande mbili”.

Hata hivyo amesema TARURA wana mpango mkakati watakayoendelea nayo ya kutekeleza miradi mikubwa na midogo kwa mwaka wa fedha 2023/24 ambapo kuna barabara ya kwenda Kisanga kupitia mbuga ya Mikumi yenye urefu wa Km 30 Serikali imetenga fedha kiasi cha Shilingi Milioni 500 ambapo watajenga boksi Kalvati kubwa na kwenda kuondoa tatizo la kuzidiwa na maji na kupelekea kukata mawasiliano.

Kwa upande wa jimbo la Kilosa Mhandisi Sawaki amesema upo mradi mkubwa wa ujenzi na ukarabati wa barabara ya Ilonga kwenda Mfuluni yenye urefu wa Km 8.9 ambayo imetengewa kiasi cha shilingi Milioni 950 na ni barabara ambayo haijawahi kufanyiwa matengenezo makubwa kwa takribani zaidi ya miaka 30 iliyopita.

“Serikali imeenda kuona tatizo hilo na kuwafikia wanachi wale na kufungua maeneo mbalimbali yenye changamoto ya kufikika. Barabara ile ipo sehemu ya mlimani sana, hivyo mlima ule unaenda kushushwa na kukatwa ili kuwa na mwinuko ambao unaweza kuruhusu vyombo vya usafiri kupita pia kuna kipande kitawekewa zege kwa ajili ya kupaboresha.

Kwa mwaka wa fedha 2023/24 amesema wametengewa kiasi cha Shilingi Bilioni 4.097 ambazo zitaenda kuhudumia maeneo mbalimbali ambayo yana changamoto ya kufikika ili kuendelea kutoa huduma zaidi na kuondoa kero walizo nazo za barabara, kalvati pamoja na madaraja.

Naye, Mtendaji wa Kijiji cha Ruhembe Bw. Coready Luwanda amesema wananchi wa kijiji hicho walikuwa wakitumia muda mrefu kuzunguka zaidi ya Km 20 ili kwenda kupata huduma za kijamii Mikumi na wakati mwingine walikuwa wakipanga magogo kwenye mto huo ambapo iliwasababishia vifo hususani kipindi cha masika.

Amesema kukamilika kwa daraja hilo ambapo urefu wa kufika barabara ya lami itakua Km 1.2 na hivyo kuwarahisishia usafiri na kuwaletea maendeleo katika kijiji chao na wananchi mmoja mmoja na hata gharama za bidhaa zitaenda kupungua na pia magari kufika hadi kijijini.
Muonekano wa daraja la Ruhembe lenye urefu wa mita 40 ambalo litagharimu shilingi Bil.1.28 na hivyo kuwaunganisha wanakijiji wa kata ya Ruhembe na Mikumi
Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Kijiji cha Ruhembe wakiwa na Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilosa wakikagua daraja la Ruhembe ambalo litaenda kuwaondolea Kero ya usafiri na kuwaletea maendeleo
Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilosa Mhandisi Harold Sawaki akiongea namna bajeti ya fedha walizopewa wataweza kuhudumia mtandao wa barabara zenye uteri wa KM 913.67.

Barabara ya kata ya Ruhembe ambayo inaingia darajani yenye urefu wa Kilomita 2 ambayo inaenda kuondoa kero kwa wananchi na kuwaletea maendeleo ya kijiji na ya mtu mmoja mmoja pamoja na kufikiwa na usafiri utakaoweza kusafirisha mazao yao



Na. WAF, Dar Es Salaam

Watalamu wa Afya nchini wametakiwa kuwa wazalendo katika kusimamia fedha zinazotolewa na wadau wa maendeleo, ili kuhakikisha wanatatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi kama ilivyo azma ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wito huo umetolewa Jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel wakati akifunga kikao kazi cha tathmini ya namna Tanzania ilivyoweza kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO-19.

Dkt. Mollel amesema kuwa wadau wengi wamekuwa wakileta fedha nyingi kwenye sekta ya afya, lakini fedha hizo zimekuwa hazitumiki ipasavyo katika kusaidia sekta hiyo, huku nyingine zikiishia kutumika katika semina na makongamano na kupelekea kushindwa kuwanufaisha wananchi ambao ndiyo walengwa.

“Zinakuja fedha nyingi kutoka kwa wadau, lakini tukishuka chini katika ngazi ya msingi hatuoni matokeo chanya, tuige mfano wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan namna alivyotumia fedha za COVID katika kuboresha huduma za afya nchini mfano katika ngazi ya msingi kumejengwa majengo ya dharura na majengo ya wagonjwa mahututi.” Amesisitiza Dkt. Mollel.

Akizungumzia kuhusu zoezi la tathmini baada ya kukabiliana na mlipuko wa UVIKO-19 Dkt. Mollel amesema yapo mengi ya kuzungumzia katika tathmini hiyo, hivyo ni jukumu la wataalamu na wadau walioshiriki kwenye kikao hicho kuhakikisha tathimini yao inakuja na matokeo chanya ya kuleta tija kwa wananchi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa Wizara ya Afya, Dkt. Angela Samwel amesema mapendekezo yote yaliyotolewa na watalaamu pamoja na wadau walioshiriki kwenye tathmini hiyo yatachukuliwa kama sehemu ya kupokea masuala yote mazuri na kuboresha mapungufu yaliyojitokeza wakati wa kukabiliana na mlipuko wa UVIKO-19.

Dkt. Angela ameongeza kuwa Tathmini ya namna nchi ilivyokabiliana na mlipuko wa UVIKO 19 imehusisha wadau mbalimbali kutoka Wizara mbalimbali ikiwemo, Taasisi za Serikali, Hospital za Taifa, Hospital binafsi, Waganga wakuu wa mikoa,wadau wengine kutoka Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Wadau wengine wa Maendeleo.





Top News