Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV
Klabu ya Soka ya Simba imekamilisha usajili wa aliyekuwa Mshambuliaji wa FC Platinum ya Zimbabwe, Perfect Chikwende usiku wa leo, Januari 15, 2021.
Chikwende ametajwa mara nyingi katika Mitandao ya Kijamii akihusishwa kusajili kati ya Simba SC na Azam FC, lakini Simba SC wamefanikiwa kufika makubaliano na FC Platinum kwa kumsajili Mshambuliaji huyo kwa uhamisho wa moja kwa moja (Permanent Transfer).
Chikwende anakumbukwa kuwafunga Simba SC katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Hatua za awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League).
Kupitia Mitandao yake ya Kijamii, Simba SC imesema kwa majigambo. “Tunasajili kwa ajili ya malengo makubwa ya Klabu hii kubwa na hiyo ndio maana ya NEXT LEVEL”, wamesema Simba SC.
Waziri wa Viwanda na Biashara Geoffrey Mwambe ameiagiza Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) kujikita katika ujenzi wa maeneo mapya ya viwanda kulingana na biashara iliyopo katika mkoa husika ikianza na Mikoa ya Lindi, Mtwara na Pwani kwa ajili ya kuwawezesha wajasiliamali wadodo kuchakata korosho ikifuatiwa na maeneo mengine yayozalisha pamba kwa wingi pamoja na uchenjuaji madini
Waziri Mwambe ameyasema hayo alipokuwa akiongea na menejimenti na wafanyakazi wa EPZA alipofanya ziara katika taasisi hiyo akiambatana na Naibu Waziri wa Viwanda Exaud Kigahe pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa Wizara ya Viwanda na Biashara.
Aidha Waziri Mwambe pia ameiagiza EPZA kuyaendeleza na kuyatunza maeneo yote inayoyamiliki ambayo imeshayalipia kwa ajili ya ujenzi wa viwanda pamoja na kufuatilia madeni yote inayowadai wapangaji wake ili fedha hiyo itumike katika kuendeleza maeneo ya viwanda na kufikia malengo iliyojiwekea ambayo hayajafikiwa hadi sasa.
Vilevile Waziri Mwambe amewaasa watumishi wa EPZA kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kuepuka vitendo vya rushwa wanapowahudumia wafanyabiashara pamoja na kujieendeleza katika taauma zao ili kuendana na wakati, kuweza kutoa huduma bora katika uwigo mpana wa biashara na kuongeza idadi ya wafanyabiashara wanaowahudumia.
Naye Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara amesisitiza EPZA kuyaendeleza maeneo inayoyamiliki ili kuepusha migogoro ya ardhi na wananchi wanaovamia maeneo hayo pamoja na kutunza maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda kwa kizazi kijacho.
Aidha, Naibu Waziri ameiasa EPZA kushirikiana na TAMISEMI katika kuelimisha wananchi faida za maeneo ya EPZA yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda huku akiishauri kutumia fursa zinazojitokeza katika kuendeleza miundombinu katika maeneo hayo hususani barabara, maji na umeme.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo
Bw. Gerald Kusaya (aliyevaa fulana ya blu kushoto) akiwa ameshika kizuia
maji wakati alipokagua mradi wa skimu ya umwagiliaji kijiji cha Msolwa
Ujamaa iliyopo Kilombero leo. Mradi huo umetekelezwa chini ya Wizara ya
Kilimo kupitia mradi wa ERPP. Wizara ya Kilimo kupitia mradi wa kuongeza tija
na uzalishaji wa zao la mpunga (ERPP) imefanikiwa kukamilisha miradi
kumi na moja iliyopo mkoani Morogoro na itakabidhiwa kwa wakulima mwisho
wa mwezi huu.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo
Bw. Gerald Kusaya (aliyevaa fulana ya blu kushoto) akikagua mfereji mkuu
wa umwagiliaji uwenye urefu wa kilometa 2.5 uliokamilika kujengwa
kijiji cha Msolwa Ujamaa wilaya ya Kilombero chini ya mradi wa ERPP leo.
Mratibu wa Mradi wa Kuongeza
Tija na Uzalishaji zao la Mpunga( ERPP) Mhandisi January Kayumbe
akiongea na waandishi wa habari wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa
skimu ya umwagiliaji ya kijiji cha Msolwa Ujamaa leo wilayani
Kilombero.Mfereji mkuu unaureu wa kilometa 2.5 ukisambaza maji kwenye
mashamba ya wakulima.
Wizara ya Kilimo imefanikiwa kupitia mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga (ERPP) imefanikiwa kukamilisha miradi kumi na moja iliyopo mkoani Morogoro na itakabidhiwa kwa wakulima mwisho wa mwezi huu.
Hayo yamebainishwa leo (15.01.2021) na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya wakati alipoongea na wakulima wa kijiji cha Msolwa Ujamaa Halmashauri ya Mji wa Ifakara Morogoro wakati alipokagua utekelezaji wa mradi (Expanding Rice Production Project-ERPP) wa ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao na skimu ya umwagiliaji .
Kusaya alisema ameridhishwa na hatua ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa maghala matano yalipo kwenye wilaya za Mvomero, Kilombero na Kilosa kufuatia wakandarasi wake kukamilisha kazi kwa asilimia 99.
“Mradi wa ERPP ulilenga kujenga maghala matano, skimu za umwagiliaji tano na maabara moja ya kilimo kwenye wilaya za Mvomero, Kilombero na Kilosa ambapo wizara inatarajia kukabidhi miradi hiyo kwa wakulima ifikapo mwisho wa mwezi huu.Nimefarijika kuona miradi yote ipo tayari isipokuwa mmoja wa skimu ya Kilangali wilaya ya Kilosa uliofikia asilimia 77 chini ya mkandarasi Lukolo Construction Ltd. ” alisisitiza Kusaya.
Katibu Mkuu huyo aliyefanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa maghala ya kuhifadhia mazao ya Kigugu (Mvomero), Msolwa Ujamaa (Ifakara) pia skimu za umwagiliaji za Kigugu (Mvomero), Kilangali (Kilosa) na Msolwa Ujamaa (Ifakara) kwa nyakati tofauti.
Kusaya alitoa wito kwa wakulima mkoa wa Morogoro ambao mradi wa ERPP umetekelezwa kuitunza miradi hiyi iliyogharimu fedha nyingi za serikali ili idumu na kunufaisha vizazi vijavyo.
“Miradi yote hii kumi na moja ni zawadi iliyotolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa wakulima wa mkoa wa Morogoro ili waongeze uhakika wa upatikanaji chakula na kipato cha kaya , hivyo wizara ya kilimo itapenda kuona ikitumika kuchangia kukuza uchumi wa wakulima wa zao la mpunga” alisema Kusaya.
Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Kuongeza Tija na Uzalishaji wa Zao la Mpunga (ERPP) Mhandisi January Kayumbe alisema mradi huo uliotekelezwa kwa miaka mitano uulianza mwaka 2016 kwa upande wa Tanzania Bara na Zanzibar.
Mhandisi Kayumbe alisema mradi wa ERPP ulikuwa na malengo manne,kwanza kupeleka mbegu bora za mpunga kwa wakulima zilizofanyiwa utafiti ambapo walifanikiwa kupata mbegu 13 kupitia mashamba darasa ambapo baada ya utafiti wakulima wengi walichagua mbegu aina ya SARO 5 iliyotoa mavuno mengi.
Litaja lengo la pili la mradi ilikuwa ni kuboresha skimu za umwagiliaji katika wilaya tatu za Mvomero,Kilosa na Kilombero ambapo jumla ya skimu tano zimejengwa tayari na tatu mradi umefanikiwa kujenga maghala matano ya kuhifadhia nafaka kwenye wilaya hizo tatu.
Mhandisi Kayumbe aliongeza kusema anaishukuru serikali ya Awamu ya Tano kwakushirikana na Benki ya Dunia kwa kutoa fedha Dola za Kimarekani Milioni 22 ( milioni 16.9 Bara na milioni 6.4 Zanzibar) zilizofanikisha kukamilisha mradi huu wa mfano kwenye sekta ya umwagiliaji nchini.
“ Mradi umekamilika kwa asilimi 97 na wizara yetu ya Kilimo imepanga ifikapo tarehe 31 mwezi huu itakabidhi miradi yote hii 11 kwa wakulima na wananchi wa mkoa wa Morogoro.
Kuhusu tija kwenye uzalishaji wa mpunga Mhandisi Kayumbe alisema mradi umefanikiwa kuongeza uzalishaji wa mpunga toka tani 2 kwa hekata mwaka 2016 hadi tani 5 kwa hekta mwaka 2019 na baadhi ya wakulima mmoja mmoja walifikia tani 10 kwa hekta ndani ya kipindi cha mika mitano ya utekelezaji wa mradi huu wa ERPP mkoani Morogoro.
“ Mradi umefanikiwa kufanya wakulima wa Morogoro kuwa na uhakika wa chakula kwa familia na sasa ziada inatumika kuuza kwenye masoko na kuwapatia kipacho cha uhakika “ alisema Mhandisi Kayumbe.
Mhandisj Kayumbe alitaja changamoto ya mvua nyingi katika miaka miwili iliyopita kuwa ilikwamisha mradi kukamilika kwa wakati hivyo kupelekea kuongezwa kwa miezi tisa kufikia mwezi huu .
Naye Mwenyekiti wa skimu ya umwagiliaji kijiji cha Msolwa Ujamaa Asumini Mwinyi alitoa pongezi kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uongozi wake unaojali wakulima hata kutoa fedha kugharimia mradi huo.
Mwenyekiti huyo alitoa ombi kwa Wizara ya Kilimo kabla ya kukabidhi mradi huo isaidie kuondoa kasoro ndogo ndogo kama maeneo ya vivuko na kukarabati barabara ya kwenda mashambani iliyoharibiwa wakati wa utekelezaji wa mradi.
Naye msimamizi wa mradi waujenzi wa skimu ya Msolwa Ujamaa Abdulamid Mbaga alisema wamekamilisha ujenzi wa mfereji mkuu wenye urefu wa kilometa 2.5 pamoja na mifereji ya upili yenye urefu wa kilometa 7.5 hivyo kuyafikia mashamba ya wakulima wengi.
Mbaga aliongeza kusema kwa sasa wanakamilisha marekebisho madogo hususan ujenzi wa matuta kuongeza udongo,ujenzi wa vivuko,eneo la kupumzikia wakulima na vyoo vya shambani kabla hawajakabidhi mradi .

<
Na. Catherine Sungura, WAMJW-Dodoma
Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipomwakilisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe Innocent Bashungwa, katika ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la TBC.
"Serikali imetimiza na itaendelea kutumiza wajibu wake kwenu; miaka mitano iliyopita hamkuwa mnapata fedha za uendeshaji na zile za miradi, leo serikali imewongezea na juzi tu mmeletewa hela zote za maendeleo kwa bajeti ya mwaka huu, kikao hiki lazima kisiwe cha malalamiko tena, kiwe sasa cha kufanya dhukuru kuhusu TBC inapaa kwenda wapi huko tuendako," alisema Dkt. Abbasi.
Alitumia fursa hiyo pia kuwapa maagizo sita wajumbe wa Baraza hilo ikiwemo kutaka kuona mipango mikubwa na yenye ubunifu katika Shirika hilo kuhakikisha linatimiza wajibu wake na kusisitiza mipango hiyo kila mfanyakazi ashiriki kuitekeleza.
Alisisitiza: "Mwanafalsafa mmoja amewahi kusema inachukua muda na kiasi kile kile cha nguvu yako kuwaza mambo makubwa au kuwaza mambo madogo yasiyo na tija. Kwa sababu hiyo nawaomba msipoteze muda kuwaza mambo madogo madogo na kuendekeza ulalamishi na majungu. Leteni mipango mikubwa na sisi Serikali tutashirikiana nanyi kuitekeleza."
Awali Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba alieleza kuwa mkutano huo unalenga kuwapatia wajumbe hao, pamoja na mambo mengine, mada kuhusu uboreshaji wa ufanisi na kuleta mabadiliko katika taasisi hiyo kongwe ya Serikali.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dkt. Agness Kijazi, akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (katikati), namna mamlaka hiyo inavyofanya kazi.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, akizungumza na uongozi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dkt. Agness Kijazi, wakati alipotembelea Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (wa nne kutoka kulia), akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), wakati alipotembelea Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, akizungumza na uongozi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), wakati alipotembelea Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Bw. Hamza Johari, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (hayupo pichani), wakati alipotembelea Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), wakati alipotembelea Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
***********************************
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), imetakiwa kutangaza taarifa zake kwa vyombo vya habari vingi kadri iwezekanavyo ili zisaidie wananchi kupanga mipango yao ya kimaendeleo na kujiepusha na majanga yanayoweza kuepukika.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, alipokagua shughuli zinazofanywa na Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
“Tafuteni vyombo vingi vya habari ili vitangaze taarifa zenu kwa kuwa ni taarifa muhimu kwa mustakabali wa Taifa na watu wake”, amesema Naibu Waziri huyo.
Amesisitiza umuhimu wa TMA kuweka taarifa zake zote katika mifumo ya kieletroniki ili ziweze kupatikana kwa urahisi kwa watu wengi na mahali popote.
Awali akitoa taarifa ya kiutendaji, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agness Kijazi, amesema Mamlaka yake imejipanga kushirikiana na vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi kutangaza taarifa za utabiri kwa wakati.
Amesema usahihi wa utabiri unaotolewa na TMA kwa sasa ni kati ya asilimia 84 hadi 96 hivyo kuifanya Tanzania kupata fursa mbalimbali za wataalamu wake kushiriki katika masuala muhimu ya Shirika la Kimataifa la Hali ya Hewa (WMO).
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kasekenya ametembelea na kuzungumza na Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), na kuwapongeza kwa uwekezaji mkubwa wa vifaa na utalaamu walioufanya na kuwezesha mamlaka hiyo kupiga hatua katika kuboresha huduma zake toka asilimia 37 mwaka 2013 hadi asilimia 69.5 mwaka 2020.
Mhandisi Kasekenya, amewataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kufanya kazi kwa uzalendo na bidii na kuhakikisha usalama wa anga la Tanzania kuwa ndio kipaumbele chao namba moja.
Aidha, amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa TCAA kutoa motisha kwa wafanyakazi ili kuwajengea ari ya kufanya kazi na kukuza uzalendo miongoni mwao.
Naibu Waziri Kasekenya yupo mkoani Dar es Salaam katika ziara ya kukagua taasisi zilizo chini ya Wizara yake ambapo ametembelea na kuzungumza na uongozi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) na Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA).