Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Najma Giga, akizungumza wakati wa kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), leo Jumatano 17/03/2021, Dar es salaam.
Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Jenister Mwagama, ambae pia ni Mjumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, akizungumza wakati wa kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), leo Jumatano 17/03/2021, Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), Ndg. William Erio, akiongea mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, katika Ofisi za Bunge jijini Dar es salaam, leo Jumatano 17/03/2021, kabla ya kuelekea kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya shirika hilo.

Meneja miradi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ndg. Helmes Pantaleo, akizungumza mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Kamati hiyo  imekagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), iliopo jijini Dar es Salaam. Leo  17/03/2021
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, ikiwa katika picha ya pamoja baada ya kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), leo Jumatano 17/03/2021, jijini Dar es salaam.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, ikikagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyo chini ya Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), leo Jumatano 17/03/2021, jijini Dar es salaam.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, leo Jumatano 17/03/2021, imekagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), hapa kwenye majengo mawili ya Mzizima Tower, Posta Mpya jijini Dar es salaam.
***************************


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti, Mhe. Najma Giga na Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Jenister Mwagama, leo Jumatano 17/03/2021, imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyo chini ya Shirika la Taifa la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), lipo chini ya Wizara ya nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mujibu wa sheria, huku Mhe. Jenister Mwagama akiwa ni mjumbe wa kamati hiyo.

Miradi iliyokaguliwa leo ni miradi ya hoteli, apartments na nyumba za kawaida za kupanga zilizopo Dar es salaam.

Miradi hiyo ni Mzizima Tower, majengo mawili yaliyopo Posta mpya,
 jijini Dar es salaam, yenye hoteli ya vyumba 90, apartments 44, eneo kwà ajili ya ofisi, yenye eneo la mraba 8502, maegesho ya magari 354, mradi ukitegemea kugharimu bilioni 220 na mpaka sasa ukiwa umegharimu shilingi bilioni 125, na mradi ukiwa umekamilika kwa 85%, ukitarajiwa kukamilika Juni mwaka huu.

Mradi mingine ni ile ya apartments na nyumba za kawaida za kupanga zilizopo Tuangoma, gharama yake ikiwa ni shilingi bilioni 161 mpaka sasa zikiwa zimetumika shilingi bilioni 61.

 Dungu Kigamboni ni nyumba 100, huku nyumba 94 zikiwa zimekamilika na nyumba 25 zikitumiwa na viongozi mbalimbali, wafanyakazi wa Manispaa ya Kigamboni na wananchi wengine.

 Mradi wa Mtoni Kijichi Dar es salaam ni mradi wa nyumba 292 katika awamu ya kwanza (1),  zikitegemewa kujengwa nyumba 820 katika awamu tatu (3), mradi ukikamilika utagharimu shilingi bilioni 159 na hadi sasa mradi umegharimu shilingi bilioni 125.5.

Mradi wa Dungu Kigamboni, umegharimu shilingi bilioni 64 ukiwa ni mradi wa nyumba 134.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Najma Giga, amesema, miradi hii ni mikubwa na ina manufaa  kwa uchumi wa Taifa na tija kwa maisha ya Watanzania waliopo katika uchumi wa kati, akiwataka NSSF kutumia mbinu mbalimbali kuhakikisha miradi hii inaleta tija kwa Taifa.

Nae Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ambae nae ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Jenister Mwagama, akiongea kwa niaba ya Serikali ameitaka Kamati hiyo kuishauri Serikali vizuri, huku akisisitiza kwa kuwa NSSF kupewa kushughulika na sekta binafsi.

Amesema NSSF ikijipanga zaidi Shirika linaweza kufanya vizuri, Serikali imeingilia kati kwa mradi wa Mtoni Kijichi, ikitaka mradi uanze kufanya kazi, huku nyumba hizo zikianza kutumika kama hostels za vyuo mbalimbali hapa Dar es salaam.

Akizungumza Mkurugenzi wa Shirika la Taifa la mfuko wa hifadhi ya jamii, Ndg. William Erio, ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwa ushauri mbalimbali, huku akisema baada ya miradi ya nyumba, sasa Shirika tayari lina ajenda ya kuwekeza katika sekta ya viwanda, ili kuhakikisha linatoa ajira kwa Watanzania walio wengi, kwa sasa tayari wameanza na kiwanda cha sukari.


 

 Na Mwandishi wetu, Kiteto


WAKAZI wawili wa Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, Leshoni Moita na Muunjuri Tepeno, wamehukumiwa kwenda jela miezi sita kila mmoja kwa kushindwa kulipa shilingi laki tano ya dhamana baada ya mtuhumiwa wa kesi ya rushwa Moita Tepeno kuruka dhamana.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Kiteto, Mossy Sasi baada ya washtakiwa hao kushindwa kulipa faini ya shilingi laki tano kila mmoja, baada ya kumdhamini mtuhumiwa Tepeno kisha akatoroka.

Hakimu Sasi amesema washtakiwa hao walimdhamini Tepeno kwenye kesi ya jinai namba 22/2020 iliyopo mahakamani ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Amesema Tepeno alijipatia fedha hizo kwa udanganyifu kuwa ametumwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Kanali Patrick Songea ili mtu ambaye binti yake mwanafunzi alipata ujauzito asichukuliwe hatua.

Amesema baada ya Tepeno kuruka dhamana mahakama iliamuru wadhamini wakamatwe na kutakiwa kutoa fungu la dhamana sh500,000 kila mmoja na kukamatwa Machi 10 mwaka huu wakashindwa kulipa kisha wakapelekwa mahabusu.

Washtakiwa hao walirudishwa tena mahakamani Machi 16 na kutakiwa kulipa fedha za dhamana kila mmoja shilingi laki tano wakashindwa, ndipo wakahukumiwa kwenda jela miezi kila mmoja na kisha wakapelekwa gereza la wilaya ya Kiteto kuanza kifungo.

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Manyara, Holle Joseph Makungu ametoa onyo kali kwa wana Manyara wote wenye mtindo wa kuwadhamini washtakiwa mahakamani na kisha kuwatorosha waache mara moja.

Makungu amesema kwa watakaoshupaza shingo zao wafahamu kwamba yatawapata kama yaliyowapata Tepeno na Leshoni kwani sheria ni msumeno hukata mbele na nyuma.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoani Manyara, Holle Joseph Makungu, akizungumza na waandishi wa habari
 

Na Mohamed Saif

Hatimaye kero ya ukosefu wa majisafi na salama iliyokuwa ikiwasumbua wananchi wa vijiji vya Nduguti na Maziliga wilayani Mkalama, mkoani Singida imepatiwa ufumbuzi.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida, Mhandisi Jackson Masaka aliyasema hayo Machi 17, 2021 kijijini Nduguti alipokuwa akizindua mradi wa maji wa thamani ya shilingi milioni 980 unaonufaisha zaidi ya wakazi 7,000.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi, Mhandisi Masaka aliipongeza Wizara ya Maji kwa utatuzi wa changamoto hiyo ambayo alisema ilichangia kuzorotesha maendeleo kwa wananchi wa Nduguti.

“Mradi huu ninaozindua leo ni ufumbuzi wa changamoto iliyokuwa ikitukwamisha kujiletea maendeo. Sasa hatuna kikwazo, tuchape kazi,” alisema Mhandisi Masaka

Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa Mkuu wa Wilaya, Meneja wa Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Mkalama, Mhandisi Antidius Muchunguzi alisema uligharamiwa na Serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Taifa wa Maji.

Mhandisi Muchunguzi alisema umejengwa na Mkandarasi Nyakire Investment Ltd na alibainisha kwamba ulianza kutekelezwa mwezi Juni 2018 na ulikamilika rasmi Desemba, 2020.

Aliongeza kwamba tayari mradi umeanza kutoa maji na wananchi wanapata maji yanayotosheleza, hata hivyo alisema wanaendelea na utoaji wa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji wa miundombinu.

Hafla hiyo ya uzinduzi wa mradi wa maji wa Nduguti inakwenda sambamba na uzinduzi wa miradi na uwekaji wa jiwe la msingi maeneo mbalimbali kote nchini ikiwa ni kuadhimisha Wiki ya Maji mwaka 2021.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhandisi Jackson Masaka akizindua mradi wa maji wa kijiji cha Nduguti.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhandisi Jackson Masaka katika picha ya pamoja na wananchi wa kijiji cha Nduguti wakifurahia uzinduzi wa mradi wa maji.



 

 

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Karolius Misungwi (kuhoto) akiweka Jiwe la Msingi la mradi wa maji wa maji wa mserereko wa kijiji cha Katete.

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Katete na watendaji watendaji wa Sekta ya Maji waliofika kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa maji wa Katete.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kalambo, Mhandisi Patrick Ndimbo akiwasilisha taarifa ya mradi wa maji wa Katete kwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi.

Meneja wa RUWASA Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Boaz Pius akipanda mti wakati wa hafla ya utiaji saini mradi wa maji wa Katete Wilayani Kalambo, Mkoa wa Rukwa.

**************************************

Na Mohamed Saif

Zaidi ya wananchi 3,000 kutoka kijiji cha Katete Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa watanufaika na mradi wa maji wa mserereko unaotekelezwa na Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira  Vijijini (RUWASA) Wilaya Kalambo.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kalambo Mhandisi Patrick Ndimbo amesema hayo kijijini Katete alipokuwa akiwasilisha taarifa ya mradi kwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Karolius Misungwi wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi Machi 16, 2021,

Mhandisi Ndimbo alisema mradi unatekelezwa na Kampuni ya Safari General Business ya Sumbawanga kwa ufadhili wa fedha za Mfuko wa Taifa wa Maji (NWF) kwa gharama ya shilingi milioni 382.

Alibainisha kwamba kijiji hicho hakikuwa na huduma ya maji na badala yake wananchi walilazimika kutumia muda mwingi kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji.

Akizungumza na wananchi wakati wa hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Karolius Misungwi aliipongeza Wizara ya Maji kwa kutambua kero iliyokuwa ikiwasumbua wakazi wa kijiji hicho na kuitafutia ufumbuzi.

“Wizara ya Maji inafanya kazi kubwa sana, tumeshuhudia miradi mingi ikijengwa, ninaamini maeneo mengine pia ya jirani nayo yatapata huduma ya maji ni suala la muda tu,” alisema Misungwi.

Aliwasihi wananchi kuhakikisha wanatumia vyema fursa zitokanazo na mradi ili kujiletea maendeleo na pia aliwataka kuhakikisha wanatunza mradi na wanalinda miundombinu.

“Huu mradi unajengwa kwa fedha nyingi, mmeteseka kwa muda mrefu kufuata huduma mbali na hapa hivyo ni lazima muwe na uchungu wa kuhakikisha mradi unadumu, msikubali mtu auchezee,” alisisitiza Misungwi.

Aliitaka Jumuiya ya Watumiaji Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO) ambayo inasimamia shughuli za uendeshaji na matengenezo ya mradi wa Katete kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa weledi.

Hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa maji wa Katete unakwenda sambamba na uzinduzi wa miradi na uwekaji wa jiwe la msingi maeneo mbalimbali kote nchini ikiwa ni kuadhimisha Wiki ya Maji mwaka 2021.

 MAHAKAMA ya Mwanzo Buguruni, Dar es Salaam, imevunja ndoa Magreth Silaeli (37) na mume wake, Raymond Kulaya (44) baada ya kujiridhisha kuwa ndoa hiyo imeshindwa kurekebishika kufuatia kuishi mbali mbali kwa miaka 10.

Ndoa hiyo imevunjwa chini ya kifungu cha 107 (2) (f) cha sheria ya ndoa na mahakama imepewa Mamlaka ya kufanya hivyo chini ya kifungu cha 110 cha sheria hiyo ya ndoa.

Aidha,  Silaeli ambaye ndio mdai katika kesi hiyo talaka namba 82 ya mwaka huu, ameieleza mahakama kuwa yeye na mzazi mwenzake wa sasa, wanatarajia kufunga ndoa Novemba mwaka huu jambo ambalo liliungwa mkono na mdaiwa ambaye ameeleza kushirikiana naye kufanikisha ndoa hiyo mpya.

Katika hukumu hiyo iliyosomwa na Hakimu Matrona Luanda leo Machi 17, 2021 imeeleza kuwa, licha ya ndoa hiyo kipitia kwenye baraza la usuluhishi lakini ilishindikana  kurekebishika.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Luanda  Silaeli (mdai) aliieleza mahakama kuwa alifunga ndoa na Kulaya Machi 18, 2006 lakini hawakubarikiwa kupata watoto na wala kuchuma mali yoyote pamoja isipokuwa mdaiwa Kulaya) alikasirishwa na kitendo cha wao kutopata watoto n ku wa apelekea kufikia uamuzi wa kutengana, mwaka 2011.

Baada ya kutengana, Silaeli alipata mwanaume mwingine na kufanikiwa kuzaa naye watoto wanne huku mwanaume akipata watoto watatu na mwanamke mwingine.

Amesema kufuati hayo, Silaeli alifika mahakamani na kuomba talaka kwa sababu hawaishi pamoja na mdaiwa kwa zaidi ya miaka 10.

"Mdaiwa alipoitwa aliieleza mahakama kuwa ni kweli walifunga ndoa ya kikristu mwaka 2006 lakini walifikia uamuzi wa kutengana ili kila mmoja akatafute watoto," amesema Hakimu Luanda.

"Baada ya mahakama kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili ilijiuliza maswali matatu, je mdai na mdaiwa walioana kwa ndoa, je, ndoa imevunjika na imeshindwa kurekebishika na nani mshindi katika shauri hilo?

Ameeleza ushahidi unaonyesha kuwa ni kweli mdai na mdaiwa walifunga ndoa ya kikristo Machi 18,2006 lakini hawakuishi pamoja kwa miaka 10 huku kila mmoja akiishi kwake licha ya baraza la usuluhishi kujaribu kurekebisha ndo hiyo bila ya mafanikio

"Nimeridhika na maelezo ya mdai na ndio ameibuka mshindi katika shauri hili na kwa Mamlaka niliyonayo ndoa hii imevunjwa hivyo, mdai apate talaka yake ndani ya siku 45 na haki ya rufaa kwa asiyeridhika ipo wazi." Amesema Luanda.

Akizungumza nje ya mahakama, Silaeli amesema waliishi kwa miaka mdaiwa kwa mitano bila kupata watoto na kwa sababu matamanio yao yalikuwa ni kupata watoto waliamua watengane mpaka sasa ambapo ameamua kuja ahakamani kudai talaka ili kila mmoja abariki ndoa yake maana kila mmoja anafamilia yake.

"Nimefurahia hukumu hii, Novemba Mwaka huu  natarajia kubariki ndoa yangu na mtu ambaye naishi naye sasa ili tuishi maisha ya kumpendeza Mungu kama mahakama ingeamua vinginevyo tungevumilia mpaka mwakani," amesema Silaeli.

Ameongeza kuwa,  yeye na aliyekuwa mume wake hawana tatizo lolote kwani wanaishi vizuri na wanaendelea kuwasiliana kama marafiki wa kawaida.

Kwa upande wake,  Kulaya amesema hakuna mtu aliyewahi kuwaingilia katika ndoa yao kuuliza kwa nini hawapati mtoto, walikaa wenyewe na kuamua kila mmoja akatafute mtoto ili kuepusha kugombana endapo  mmoja wapo angepeleka  mtoto wa nje ya ndoa yao.

"Tunaishi kwa amani, mwenzangu amejaliwa watoto wanne na mimi ninao watoto watatu na kabla ya ndoa nilikuwa nao wawili. Nimekubaliana na maamuzi ya mahakama wote tumeshinda katika kesi hii hatukuwa na mali hivyo, tusingweza kugawana vyumba vya kupanga" amesema.

Aliongeza wangeweza kusubiri huenda Mungu angewapatia zawadi hiyo ya watoto lakini ndiye anayejua na tayari yameshatokea hivyo, hawezi kumnyang'anya mwanaume mwenzake watoto wake eti kwa sababu amelima kwenye shamba lake.



 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (katikati) akizungumza wakati Kamati hiyo ilipotembelea Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Morogoro kukagua ujenzi Maabara Mtambuka. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Othman Chande na kulia ni Makamu Mweyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Japhet Hasunga leo Machi, 17, 2021.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Prof. Raphael Chibunda  (wa kwanza kushoto) akifafanua jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakati Kamati hiyo ikikagua ujenzi wa Maabara Mtambuka inayojengwa chuoni hapo  leo Machi, 17, 2021.

Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Othman Chande (kushoto) akizungumza mbele na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakati Kamati hiyo ilipotembelea Chuo hicho kukagua ujenzi wa Maabara Mtambuka inayojengwa chuoni hapo leo Machi 17, 2021. Katikati ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka na kulia ni Makamu Mweyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Japhet Hasunga.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Menejimenti ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Morogoro wakimsikiliza Mshauri Mwelekezi kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi, Rweyemamu Vedasto akifafanua kuhusu Mradi wa ujenzi wa Maabara Mtambuka katika Chuo hicho wakati Kamati hiyo ilipotembelea Chuoni hapo na kukagua ujenzi huo leo Machi 17, 2021.

 


PICHA NA BUNGE


 

 

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea  akizungumza katika Ukumbi wa mkutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora alipotembelea kwa ajili ya kufanya ziara katika Mkoa huo kuangalia hali ya mawasiliano.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akimkabidhi kitabu chenye miradi ya Ujenzi wa minara nchi nzima cha Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Mkuu wa Wilaya ya Urambo Angelina Kingwa alipotembelea wilaya hiyo kuangalia hali ya mawasiliano.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akioneshwa Jengo la Posta Tabora na Meneja wa Posta Mkoa huo Devota Mkude alipofanya ziara katika Posta hiyo.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akipata utambulisho katika Ofisi za TTCL Tabora.

*Minara yote ifanyiwe utafiti kuangalia uwezo.

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV - Urambo

 NAIBU Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea amewataka watoa huduma wa kampuni za simu kuongeza uwezo katika minara yao katika Wilaya ya Urambo.

Uongezaji wa uwezo kutokana na mahitaji ya watumiaji kuongezeka kwani minara hiyo ilijengwa miaka ya mingi na kuwa na watumiaji wachache.

Naibu Waziri Kundo aliyasema hayo alipofanya ziara katika Wilaya ya Urambo na kudai kuwa suala la mawasiliano ni laziama kwa ajili ya kurahisha upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa njia ya mtandao.

Amesema kuwa mawasiliano yanakwenda katika kutoa shuluhisho la Sekta ya afya kwa hospitali zilizo pembezoni kufanya vipimo na Daktari Bingwa wa hospitali ya Taifa Muhimbili.

Ziara katika wilaya ya Urambo na Jimbo ulifanyika katika Kijiji cha Mlangale ,Wema pamoja Nsogoro.

Mhandisi Kundo amesema kuwa minara iliyojengwa kwa miaka ya nyuma haiendani idadi iliyopo sasa na kufanya kuelemewa kutoa huduma.

Mkuu wa Wilaya ya Urambo Angelina Kingwa amesema kuwa Jimbo la Urambo na Wilaya hiyo kuna changamoto ya mawasiliano kwa baadhi ya maeneo .

Katika ziara hiyo alitembelea shirika la Posta (TPC),Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kudai kuwa mashirika hayo kwa Mkoa wa Tabora wamejipanga katika utoaji wa huduma pamoja na kufanya ubunifu wa ushindani wa kibiashara.

 

 

**************************************

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama ameiongoza kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kuukagua mradi wa uzalishaji sukari katika shamba la Mbigiri,  wilayani kilosa mkoani Morogoro.

Akiongea wakati wa kikao na Kamati hiyo aliihakikishia kuwa nia ya serikali ya Awamu ya Tano ni kukamilisha ujenzi wa kiwanda hicho kwa wakati ili kuweza kupunguza naksi ya mahitaji ya sukari nchini pamoja na kuweza kutengeneza ajira za moja kwa moja na ajira zisizokuwa za moja kwa moja kwa watanzania.

Mradi huo kwa sasa umeajiri moja kwa moja wafanyakazi 387. Kati ya hao, 300 ni vibarua katika mashamba. Inakadiriwa kwamba mradi  tayari umetoa ajira ambazo si za moja kwa moja kwa wananchi zaidi ya 2,000.

Uzalishaji wa sukari utakapoanza jumla ya wananchi zaidi ya 1,200 wataajiriwa, kati ya hao 650 watakuwa mashambani. Pia ajira zisizokuwa za moja kwa moja kwa wananchi zaidi ya 5,000 zitapatikana. Aidha, kwa sasa kilimo cha miwa kwa wakulima wa nje zaidi ya 245 wamehamasishwa na wakulima 1, 000 wanatarajiwa kuwa wamehamasishwa kiwanda kitakapoanza uzalishaji sukari.

Mradi huo unaotarajiwa kuzalisha tani 50,000 kwa mwaka, unatarajia kuanza kuzalisha sukari kwenye kiwanda cha Mbigiri katika kipindi cha mwisho  wa msimu wa  mwaka 2021/2022 ambapo maandalizi ya eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda yamefanyika kwa kutenga eneo la ukubwa wa hekta 35.3.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC), Mhe. Naghenjwa Kaboyoka aliwaongoza wajumbe wa kamati hiyo kukagua eneo lililotengwa kwa ajili  ya ujenzi wa kiwanda, mabweni kwa ajili ya mafundi 112 wa awali wa kiwanda, ofisi za kiwanda, ukumbi mdogo wa mikutano, barabara ya kuelekea eneo la kiwanda pamoja na bwawa la kuhifadhi maji ya kumwagilia miwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi ya Mradi Dkt. Hildelitha Msita, ameeleza kuwa mradi umejenga zahanati itakayotumiwa na wafanyakazi pamoja na wananchi wanaoishi jirani na mradi. Aidha, ameeleza kuwa wanaendelea kuboresha kazi za kilimo kwa kununua zana za kilimo na vifaa vya kisasa vya kilimo kulingana na mpango mkakati. Lengo la mradi ni kufikia uzalishaji wa sukari kiwango cha tani 110 kwa hekta ifikapo mwaka 2021/2022  na tani 130 kwa hekta ifikapo mwaka 2023/2024.

Kampuni Hodhi ya Mkulanzi ilianzishwa mwaka 2016 kwa lengo la kuanzisha viwanda vyenye uwezo wa kuzalisha jumla 250,000 za sukari kwa mwaka ili kupunguza nakisi ya mahitaji ya sukari nchini. Endapo Mradi wa Mbigiri Estate, ukianza kutekelezwa unatarajia kuzalisha tani 50,000 za sukari kwa mwaka.Uzalishaji huo utasaidia kupunguza naksi ya mahitaji ya sukari nchini. Kampuni hiyo inamilikiwa kwa asilimia tisini na sita na Shirika la Uzalishaji mali Magereza kwa asilimia nne.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt Zainab Chaula akizungumza wakati akifunga kikao cha wadau cha kujadili mapendekezo ya kutungwa kwa Sheria ya TEHAMA kilichofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Lugano Rwetaka na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Godleader Shoo.

Baadhi ya wadau walioshiriki katika kikao cha wadau cha kujadili mapendekezo ya kutungwa kwa Sheria ya TEHAMA kilichofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Lugano Rwetaka akizungumza katika kikao cha wadau cha kujadili mapendekezo ya kutungwa kwa Sheria ya TEHAMA kilichofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo Godleader Shoo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt Zainab Chaula akizungumza wakati akifunga kikao cha wadau cha kujadili mapendekezo ya kutungwa kwa Sheria ya TEHAMA kilichofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

 

***********************************

Na Faraja Mpina – WMTH, Dodoma

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imewakutanisha wadau mbalimbali ambao ni wataalamu wa TEHAMA kutoka katika Wizara, taasisi za Serikali na sekta binafsi ili kujadili mapendekezo ya kutungwa kwa Sheria ya TEHAMA kwa lengo la kupata maoni ya wadau hao na kuyafanyia kazi kabla ya kupeleka mapendekezo hayo katika Sektetarieti ya Baraza la Mawaziri.

Akifungua kikao hicho kilichofanyika tarehe 16.03.2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuwepo kwa Sheria ya TEHAMA nchini kutokana na kukua kwa kasi kwa teknolojia hiyo nchini yenye msukumo mkubwa kibiashara.

Amesema kuwa Serikali imewekeza katika kukuza matumizi ya TEHAMA nchini ili kuendana na mahitaji ya mapinduzi ya nne ya viwanda, hivyo ni muhimu kuwa na Sheria itakayohakikisha inatoa mwongozo wa matumizi sahihi ya mifumo ya TEHAMA na wananchi waweze kushiriki ipasavyo kwenye uchumi wa kidijitali.

“Ili mambo yaende vizuri ni lazima tuwe na Sheria mahsusi ya TEHAMA itakayotoa mwongozo na kusaidia kusimamia na kutambua nani anafanya nini, wapi, muda gani na kwa utaratibu upi”, alizungumza Dkt. Chaula  

Ameongeza kuwa Sheria hiyo itaweka utaratibu wa mifumo rafiki na madhubuti katika uendelezaji na usimamizi wa matumizi ya TEHAMA nchini ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya taasisi za umma kwa maendeleo ya Taifa.

“Kupitia Sheria hii natamani tutoke na dawa ya kumfanya kila mtu awe mtiifu na mzalendo badala ya kuwatafuta wahalifu wa mitandaoni tutengeneze elimu jamii itakayowafanya watu wawe na matumizi sahihi badala ya kutumia mifumo ya TEHAMA badala ya kuitumia kuchafua taswira ya nchi na kudhalilisha wengine”, alizungumza Dkt. Chaula

Aidha, Dkt Chaula ametoa rai kwa wadau hao kupeleka mrejesho kwa taasisi wanazoziwakilisha na kama kuna kitu ambacho kimesahaulika kitumwe katika Wizara hiyo kwa maandishi ili kuondoa sintofahamu ya wadau mbalimbali kuja kusema hawakushirikishwa.

Dkt. Chaula ameongeza kuwa mchakato wa kutungwa kwa Sheria hiyo ni wa muda mrefu na tayari maoni ya watu wengi  katika maeneo tofauti tofauti yamekusanywa na kufanyiwa kazi

Naye Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria wa Wizara hiyo Lugano Rwetaka amesema kuwa Sheria ya TEHAMA ni jambo la msingi kwa sababu soko la TEHAMA linakuwa kwa kasi nchini na duniani pote na kuleta uhitaji wa kuwa na matumizi ya TEHAMA kwa mujibu wa Sheria.

Amesema kuwa kuna sheria mbalimbali zinazosaidia kukuza na kuleta ulinzi katika TEHAMA lakini bado kuna vitu vingi ambavyo havijaainishwa katika sheria hizo hivyo kuna umuhimu wa kuwa na Sheria maalumu ya kusimamia TEHAMA nchini ambayo itaenda kubuni mbinu mbalimbali za kuimarisha ulinzi katika mtandao

“Moja ya malengo ya Sheria hii ni kuhakikisha bidhaa za TEHAMA zinatengenezwa hapa hapa nchini kwa matumizi ya nchi lakini hata pia tuweze kuziuza katika nchi nyingine za nje ya Tanzania”, Alizungumza Rwetaka

Naye Dkt. Nkundwe Mwasaga Mhadhiri kutoka Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) amesema kuwa kuna umuhimu wa kuwa na Sheria ya TEHAMA ambayo itatengeneza mazingira ya kuweza kufanya tafiti, ubunifu na uwekezaji katika TEHAMA.

 


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Zanzibar, wakati wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa maagizo yake kwa Mawaziri na Makatibu Wakuu, mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akifuatilia taarifa ya utekelezaji wa maagizo yake aliyoyatoa kwa Mawaziri na Makatibu Wakuu,ikiwasilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Bi. Fatma Hamad Rajab (hayupo pichani)  wakati wa mkutano huo wa Uongozi wa Wizara hiyo uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akifuatilia uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji wa maagizo yake aliyoyatoa kwa Mawaziri na Makatibu Wakuu wakati wa kuapishwa katika viwanja vya Ikulu, ikiwasilishwa na Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita na (kushoto kwake) Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ndg. Khamis Abdalla Said, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha

KATIBU Mkuu Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Bi. Fatma Hamad Rajab akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Rais aliyoyatoa wakati wa kuwaapisha Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali za SMZ katika viwanja vya Ikulu Zanzibar, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

 

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akisisitiza jambo kwa Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akimsikiliza Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Mazungumzo yakiendelea 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke wakiwa katika picha ya pamoja  mara baada ya kuhitimisha mazungumzo yao yaliyofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akisisitiza jambo kwa Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.

************************************

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge mapema leo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke katika ofisi za Wizara jijini Dodoma. 

Wawili hao wamejadili masuala mbalimbali yanayolenga kudumisha zaidi ushirikiano na uhusiano wa kidiplomasia na biashara. Vilevile wamejadili kuhusu ufuatiliaji wa maendeleo ya miradi na programu mbalimbali zinazotekelezwa kwa ushirikiano wa Tanzania na China ili kuhakikisha zinaleta tija kwa manufaa ya pande zote mbili.

Balozi Ibuge kwa upande wake ameeleza kuwa kuwepo kwa uhusiano mzuri wa Kidiplomasia baina ya Tanzania na China kumechagiza kwa kiasi kikubwa kukuwa kwa biashara, utali na uwekezaji baina ya nchi hizi mbilia hivyo urafiki na undugu kati ya Mataifa haya mawili unapaswa kulindwa, kudumisha na kuendelezwa siku zote na katika hali yoyote. “China kwa muda mrefu imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya Taifa letu kupitia sekta mbalimbali kama vile ujenzi wa mundombinu ya usafirishaji na mawasiliano kama vile reli na barabara, hivyo Wizara na Serikali kwa ujumla inadhamini na kulinda undugu huu wa kihistoria” Balozi Brigedia Jenerali Wiibert A. Ibuge

Mheshimiwa Balozi Wang Ke kwa upande wake ameshukuru kwa ushirikiano ambao amekuwa akiendelea kuupata kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Serikali kwa ujumla katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku. Ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano ili kuhakikisha serikali za nchi hizi mbili na watu wake wananufaika kotokana na uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo.



Waziri wa Mawasiliano Teknolojia ya Habari Dkt.Faustine Ndungulile akimkabidhi hati ya Ardhi Katibu mkuu wa Umoja wa Posts Afrika ,Katibu Mkuu wa umoja wa Posta Afrika (PAPU),Djibrine Younouss,kulia kwake ni Posta masta mkuu Hamisi Mwang'ombe.
Waziri wa Mawasiliano Teknolojia ya Habari Dkt.Faustine Ndungulile akikagua hati ya kiwanja Cha PAPU Mara baada ya kukabidhiwa na kwa niaba ya Katibu mkuu
Kaimu  Katibu mkuu wa Wizara ya  Mawasiliano Injinia Clarence Ichekweleza akimkabidhi Waziri wa Mawasiliano Teknolojia ya Habari Faustine Ndungulile hati ya kiwanja Cha PAPU leo Jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi Victor Nkya akitoa taarifa ya mradi wa makao makuu ya PAPU mbele ya Waziri wa Mawasiliano Teknolojia ya Habari Dkt.Faustine Ndungulile


Na Vero Ignatus,Arusha

Hatimae mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka 25 baina ya (PAPU) na baadhi ya wananchi wa kiwanja cha Makao makuu ya Posta Afrika kilichopo Mkoani Arusha umetatulika baada ya kukabidhiwa hati rasmi kwa umiliki kwa PAPU  kuwa Mmiliki halali wa kiwanja hicho.

Akizungumza katika makabidhiano hayo ya hati Waziri wa Mawasiliano Teknolojia ya Habari Dkt. Faustine Ndungulile alisema hii Ni moja ya mafanikio makubwa ya kukabidhi hati na hatujawahi kutokea katika Jiji la Arusha na utaleta tija .

Amewataka wakandarasi kuongeza kasi ya ujenzi huo kwnai wapo nyuma kwa wiki mbili ambapo amesema anaimani kuwa ifikapo June mwakani jengo hilo litakuwa limekamilika 

"Niwasihi  wakandarasi mnaosimamia mradi huu muhakikishe unamalizika kwa wakati kama ilivyopangwa mwezi wa sita ,2022 hivyo mhakikishe mnafanya kazi usiku na mchana ili umalizike kwa muda uliopangwa na kw wakati sahihi "
amesema Dkt.Ndungulile

Amesema kuwa, kukamilika kwa mradi huo kutaongeza ufanisi mkubwa katika utendaji kazi wao huku ikitoa fursa mbalimbali za ajira pindi jengo hilo litakapokamilika.

Amesema kuwa ,mradi huo hadi kukamilika utagharimu kiasi cha shs 33.6 bilioni , ambapo aliipongeza wizara ya ardhi kwa kufanya kazi nzuri ya kukabithi hati  hiyo kwani kwa muda mrefu walikuwa hawana hati ya kiwanja hicho.

Dkt.Ndungukile amelitaka Shirika la Posta  kuwa kielelezo pekee cha maendeleo ambacho kitakuwa mfano bora wa kuigwa huku akiwataka kwenda na kasi mpya ,na kuhakikisha makao makuu ya posta yanafafana huduma wanazotoa katika kuhakikisha inaendeshwa kidigitali zaidi.

Naye Mwenyekiti wa bodi kutoka TCRA,Dokta Jones Killimbe amesema kuwa,ujenzi wa jengo hilo ambao ndio utakuwa makao makuu ya posta Afrika na ofisi za Kanda ya kaskazini za PAPU ni ushindi  mkubwa Sana kwao kwani unaongeza ajira kwa watanzania walio wengi pia.

Dkt. Kilimbe amesema kuwa,uwepo wa jengo hilo utaongeza tija kubwa kwa mapato ya  fedha za kigeni pamoja na kuwepo kwa mikutano yote ya Kimataifa ambapo  ukumbi utakuwa na uwezo wa kubeba zaidi ya watu Mia tano .

Tunashukuru sana kuongezewa eneo kwani lililokuwepo lilikuwa dogo Sana ila kwa Sasa hivi eneo limepanuliwa  na kuwa kubwa ,hivyo tunashukuru Sana kwa serikali kwa ushirikiano mkubwa katika kukamilika swala hilo.”amesema.

Naye Katibu Mkuu wa umoja wa Posta Afrika (PAPU),Djibrine Younouss amesema kuwa,anashukuru Sana serikali kwa kuwapatia hati hiyo baada ya kuwepo kwa mgogoro kwa takribani miaka 25 Sasa na hivyo hivi Sasa umeweza kufikia mwisho na kuweza kupatiwa hati hiyo.