Hizi taa za solar , zinatumia betri yenye kutumia mionzi ya jua , zinatengenzwa na WODSTA , (Women Development for Science and Technology Association ) huko Arusha. Hakuna haja ya giza kijijini jamani .

Hizo bulbu ndogo zinawekwa kwenye mfuniko wa chupa ya plastiki iliokuwa inahifadhi maji .( Recycled water bottles bulb covers ) System nzima ni betri ndogo inayodumu miaka mitatu na taa tatu .

Inagharimu kama $100 za kimarekani . Kwa kweli huwezi kulinganisha na gharama ya kuvuta umeme na bili za kila mwezi . Waliotaka kuwajengea mama zao au ndugu zao yale “majiko ya mama”

tuma email
kwa taarifa zaidi.

Muda umefika jamani wa kuunga mkono bidhaa zetu za kiTanzania zenye kustahili.
Mdau Msafiri SS

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. JAMANI TUACHE USANII, HIVI HAWA AKINAMAMA WANATENGENEZA HIZI TAA AU WANAAGIZA ZIKIWA TAYARI ZIMETENGANEZWA TOKA NJE? NIJUAVYO TANZANIA HATUNA KIWANDA KINACHOTENGENEZA VIFAA VYA SOLAR IKIWA PANEL, BULB NA BETRI YAKE.

    ReplyDelete
  2. mimi nina kibanda changu/boys kota shambani kwangu mlingotini bagamoyo nimevutiwa sana na umeme hu,nitawapataje hao wamama ili wakanifungie kwenye hicho kibanda changu.Transport cost itakuwa juu yangu au? Grama za fundi ni inclusive ua ? Maelezo zaidi pleaseeee!!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...