Bw. Michuzi na wadau wa soka,
Nina maoni marefu ila naomba mnivumilie kwani nafikiri ninahitji kuwa objective kwenye hili. Naomba niwashirikishe ninyi pia kutafuta ufumbuzi wa pamoja.
Mimi ni mdau wa soka hapo Tanzania lakini kwa sasa niko hapa Ujerumani. Nimekuwa nikifuatilia maendeleo ya nchi yetu kwa ujumla, lakini soka kwa namna ya pekee.
Kwa ujumla, hali si nzuri kabisa kwenye nyanja nyingi - kuanzia uchumi na siasa zake hadi soka. Nikijikita kwenye mada yangu, nimekuwa nikifuatilia timu yetu ya Taifa kwa ukaribu na mabadiliko ndani ya TFF. Naweza kusema Maximo kama kocha amejitahidi.
Pia, kukua kwa kiwango cha soka nchini kinaweza kuwa kumesababishwa na yafuatayo:
1. mwamko mkubwa wa wadau,
2. jitihada za vilabu kujibadilisha,
3. nia ya wachezaji kupata exposure (hata tamaa ya kucheza nje),
4. kuongezeka kwa wachezaji ambao pia wamepitia shule,
5. kuongezeka kwa thamani ya wachezaji nje hivyo vituo vya kukuza wachezaji kuongezeka,
6. kuongezeka kwa udhamini (modern marketing strategy ya makampuni mengi), na
7. nia za serikali - kuanzia wakati wa Mkapa aliposafisha FAT na kujenga "Old Trafford" (New and modern Stadium) yetu hadi wakati huu wa Kikwete kumleta Maximo na ku-support timu moja kwa moja.
Wadau, tatizo langu ni kubadilika badilika kwa timu ya Taifa kila kukicha. Sababu kubwa inayotolewa na Maximo ni nidhamu, uzalendo na lengo la kuleta mafanikio. Lakini wakati huo huo tukipoteza michezo Maximo anasema sababu wachezaji hawana uzoefu na bado anawajenga.
Wadau tusisahau kuwa kikosi ambacho Maximo alienda nacho Brazil sio hiki sasa. Kile ambacho kilishiriki qualifiers za Afrika na World Cup kwa kiasi kikubwa si hiki.
Pia, kikosi kinachocheza mechi nyingi za kirafiki ambazo zinaigharimu TFF na sisi tunaoingia uwanjani kwa mechi zilizo kwenye FIFA calendar si hiki. Yaani, huwezi kusema marekebisho mangapi kayafanya kwenye kikosi hiki.
Kwa ujumla, Maximo hana timu ya Taifa ambayo anarekebisha kidogo labda sababu ya majeruhi na kuporomoka kwa kiwango kwa wachezaji. Kila siku ni kikosi kipya ila ikitokea mchezaji wa kikosi kilichopita kajumuishwa, basi hiyo ni bahati yake.
Wakati makocha wengine, mchezaji mpya akiitwa kikosini, basi ndiyo ana bahati. Kwa Maximo, ni kinyume chake. Kwa ufupi, hakuna wachezaji muhimu na permanent kwenye Taifa Stars. Si kama akina Ronadinho, Kaka, Adriano, Robinho kwa Brazil; Mesi, Tevez, Mascherano, Aguiero, Zaneti kwa Argentina; Terry, Ferdinand, Cole(s), Rooney, Gerrard, James kwa England, n.k.
Kwa hali hii tusitegemee kuona timu ikikuwa na kukomaa. Kwa Maximo kila siku ni kuzaa timu changa. Hatoi nafasi kwa timu kukua na kukomaa. Hii inasababisha wadau kuhisi kama anabahatisha na kutafuta visingizio (timu ikifanya vibaya) kwa wadau ili wa-sympathy nae kwa kuwa wachezaji ni vijana na hawana uzoefu.
Kwa kweli alikuwa na nafasi kubwa ya kufanikiwa kama kocha kutokana na mazingira mazuri ya soka la Tanzania kwa sasa (kama sababu zinavyoonesha hapo juu) katika ukanda wetu hapo. Kwa nini anabadili timu kila kukicha? Maximo anasema nidhamu, uzalendo na lengo la kupata mafanikio ni vigezo muhimu kwake. Mimi naungana nae mkono moja kwa moja kwenye hili.
Ila natofautiana nae namna ya kuyapima na kuya-manage hayo. Yeye kama kocha ndiye mzazi wa mchezaji. Hivyo, jukumu la kumlea mchezaji ni lake. Pia, kama mzazi unakuwa karibu na wachezaji ili wa-feel uzazi wako. Lakini haingii akilini kuona kila siku anawaacha wachezaji kisa nidhamu, kakosa uzalendo na hajitumi. Hiangii akilini akina Chuji, Bobani, Abdi Kassim, Maftah, Farouk ambao amekuwa nao kwa miaka kadhaa ingawa wakati mwingine ni On and Off wamekosa hizo sifa leo.
Hatujasahau ya akina Machuppa, Abdallah Juma, Admini Bantu, Mwaikimba, Kaseja, Costa, Mussa Kipao, nk. Hao wachezaji wanajuhudi kubwa na wanajituma na ni tegemeo kwenye vilabu vyao. Iweje kwake tu tena baada ya kuwa nao kwa nyakati tofauti tofauti?
Inawezekana kweli mchezaji akakosea (hata Ulaya na Brazil kwake hutokea sana tu) utaifa unawekwa mbele. Alitakiwa aongee na meneja na TFF. Pale TFF, akina Kayuni/Madadi/Mwalusako/Mziray ndio wanafaa kuitwa na kushughulikia hayo na si nafasi za kisiasa za akina Rais na Katibu.
Walitakiwa kumwita mchezaji ambaye Maximo anamuona ana kasoro za kinidhamu, wanaongea naye na ikiwezekana kumtafutia wanasaikolojia na hivyo kumrudisha kwenye mstari. Akina Stephen Mapunda waliambiwa hawatavaa tena jezi ya Taifa hadi Ndolanga aondoke madarakani.
Hii si nzuri kwa soka letu na haitafikia tukakua na kukomaa. Naamini tungekuwa na wachezaji wengi walianza wakati wa kwenda Brazil na kucheza mechi zote za kirafiki na mashindani ambayo Maximo amesimamia, wangekuwa na uzoefu wa kutosha na hata kule CHAN Ivory Coast tungefanya vizuri zaidi.
Pia asikilize ushauri wa wadau. Kwa sasa anajivunia Tegete na Ngasa ambao alikuwa amewapuuzia wakati wadau walikuwa wanamlilia awajumuishe Taifa Stars. Boban pia aliwekwa kando hadi wadau walipolalamika sana na mwenyewe alimkubali kwenye mechi zetu na Bukina Faso, Senegal, nk.
Abdi Kassim alifunga goli bora na la rekodi Uwanja mpya na mwenye uwezo wa kubadili mchezo leo hana nidhamu. Sasa anataka wachezaji gani? Si vizuri kusikiliza wadau lakini haingii akilini kuwa na mchezaji wa kiwango cha juu halafu humtumii kwa taifa - mfano wa hili pia ni Kaseja.
Naomba wadau tujadili hili na TFF na Maximo wapate ujumbe ili tuzidi kuboresha si timu tu bali mkakati mzima wa kukuza soka Tanzania. La sivyo tutakuwa tunapiga "mark-time" miaka nenda rudi.
Hakuna haja ya TFF na Maximo kuanza kujitetea na kutoa sababu za hapa na pale ku-justify what is happening now!!
Wakubali kujifunza (kwani wasifikiri wako 100% perfect) ili tupige hatua mbele.
There's always a room for improvement.
Ni mdau mwenzenu
Geoff. I. Mwambe
Mannheim,
Germany

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 37 mpaka sasa

  1. Mdau Mwambe,kwanza hongera kwa mada hii.u got some gud points.personally,sikuwahi kuiona Staz ikicheza chini ya Maximo hadi ktk haya mashindano ya CHAN(which overall performance as a team na hata individual haikuwa ya kuridhisha).lkn kwa kiasi kikubwa nimekuwa nikifuatilia uteuzi wa timu yetu ya taifa na hata matokeo ya games kupitia vyombo vya habari.na ni kweli kama ulivyosema Maximo amekuwa akitapatapa kwa kutokuwa na msimamo juu ya wachezaji wa kudumu ktk timu ya taifa.

    ni vigumu kupata maendeleo kwa kutaka kujenga upya kile ulichoanza kukijenga.hivyo inakuwa unaenda hatua chache mbele then hatua nyingi nyuma.najua ana baadhi ya wachezaji walio wa kudumu lkn idadi yao mara zote huwa ni ndogo kulinganishwa na ile ya wapya.hivyo hata ktk ufundishaji inakuwa kama mara zote uanze upya badala ya kuendeleza kile ambacho wachezaji(wengi wa mwanzo) wameshajifunza.na hilo litasaidia kwa wale wapya kuelewa kwa urahisi.

    nakubadiliana na wale wanaosema Maximo kabadili mtazamo wa soka bongo.lkn je,kufuzu ni mafanikio kweli tunayoyataka ama tunataka kujivunia matunda ya kufuzu huko????
    hivi tangu achukue timu,ni mamilioni mangapi yamesogezwa ktk timu yetu na tumejivunia nini haswa?me ningejivunia zaidi kama tungechukua kombe la Chalenji kuliko hata kuifunga timu kama Cameroun.kwani wadau wengi wanaona mafanikio ya kocha ni kuzifunga timu vigogo wa soka barani Afrika.

    Ukiangalia viwango vilivyoonyeshwa na timu zilizoshiriki hiyo CHAN, STAZ ilikuwa na kila nafasi ya kufanya vizuri kama isingekuwa ubabaishaji wa huyu Maximo.

    Ukichukulia mshahara anaolipwa kocha,sapoti ya kifedha ktk maandalizi ya timu na huduma zingine muhimu huwezi kukubali kwamba eti kaleta mafanikio.Je ni mafanikio gani?mafanikio ya Kocha yanakuja ktk Vikombe na sio eti tumefuzu kucheza mashindano haya au yale.TUMECHOKA KUWA WASHIRIKI!!!!!!

    sisemi kwamba ni kocha mbaya,but he needs to change himself first before he can change Staz na kupata mafanikio.HIS APPROACH FOR SUCCESS inakatisha tamaa.

    ReplyDelete
  2. mdau,

    nakubaliana na wewe moja kwa moja. maximo kajitahidi, ila sidhani kama anaweza kutufikisha zaidi ya hapa. na kiwango hakijakua kiivyo sana, ni kwamba wachezaji wamepata exposure, na ukiangalia dunia yote mpira unakua, kwa hiyo in perspective bado tupo pale pale.

    nadhani muda wa maximo kuondoka umefika. sasa hivi wachezajii hawataki kuchezea timu ya taifa kisa maximo. hata kama wana makosa, kama hawezi kuwaonyesha makosa yao nao wakakiri basi hafai. kumu-alienate mchezaji si suluhisho. sasa leo kuna machupa, kaseja, boban, chuji, maftah, costa na wengineo ambao ndo hivy hawatachezea tena timu ya taifa so long as maximo ni kocha. na katika timu kuna wengine ambao kwa mwenendo huu watakuwa wameonywa kuwa waangalifu - yondani, jabu etc. sasa kocha aina hii ndo tunayemtaka kweli?

    mi nadhani kazi imemshinda aondoke. TFF iwe pro-active wamuachishe kazi aishie zake. yan pamoja na mazuri yote yanayofanywa na wadau kuhakikisha kwamba mazingira ya soka bongo ni pro-active bado hatujaweza hata kushinda kikombe chochote! nadhani uwezo wake umefika kikomo, aishie tu....

    ni hayo tu........

    ReplyDelete
  3. Maximi ni mbabaishaji.juzi kaja na gea mpya kuwa anachukua vijana kwa asilimia 70 swali wakati anaenda Chan kwanini hakuwachukua hao vijana anaodai wanafundishika?

    huko nyuma alimkataa mgosi hadi watu walipolalamika kuwa mgosi kawa mfungaji bora wa Taifa cup vipi unamkataa taifa stars?

    pawasa alimkataaa kwa vile anasema hajawahi kumona. kina wenger wanachukua wachezaji sio kwa kuwaona bali kwa recomendations za ma scout.

    wachezaji kama DROGBA,BECKHAM,BARRACK,JIMMIE GARAGHER,LAMPARD,GALLAS WANA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 30 LAKINI NDIO CHACHU YA USHINDI WA TIMU ZAO.

    HUWEZI KUMUWEKA NJE DROGBA NA UKAMPANGA SHAUN WRIGHT KWA VILE SHAUN NI KIJANA KWA DROGBA.

    HUKO HUKO BRAZIL ALIKOTOKA KUNA WACHEZAJI KAMA ROBERT CARLOS NA CAF WAMECHEZA HADI WAKIWA NA MIAKA 35.

    KAMA KASEJA ANGECHEZA KWENYE KOMBE LA DUNIANI KUNA MAGOLI STARS ISINGEFUNGWA KAMA YALE YA KIJINGA TULIFUNGWA NA CAMEROON KWA KUKOSA KIPA ANAYEJUA KUCHEZA KROSI NA HANA UZOEFU.

    PIA KAMA ASINGEMFUNGIA BOBAN KULE NYUMA BASI MECHI KAMA NA CAPE VERDA,MAURITIUS TUNGESHINDA, KAMA ALIVYOMUWEKA BENCHI CHUJI KWENYE CHAN MATOKEO YAKE KAMUWEKA BOONY ASIYE NA UZOEFU TUMEFUNGWA.

    KAZI YA CHUJI KAIONA KWENYE MECHI NA CAMEROUN VIPI UNAMUWEKA NJE KWA CHUKI KUWA HANA NIDHAMU, BASI ANGEMUACHA TZ kuliko kupoteza pesa za taifa kwenda nae Ivory coast WAKATI HAMTUMII,

    ANGEPELEKA HAO CHIPUKIZI WAKAPATE UZOEFU.

    TIMU ZOTE KUBWA HUWA NA BENCHI LA UFUNDI LAKINI STARS MAXIMO NDIO KILA KITU HUWEZI KUBISHANA NAE, WATU WANAOGOPA KAMA KINA TENGA WANAONA UDHAIFU WAKE LAKINI WANAOGOPA KUMKOSOA KWANI YEYE ANARIPOTI KWA BWANA MKUBA MOJA KWA MOJA.

    HILI LIMEMPA KIBURI KIKUBWA MAXIMO.

    MAXIMO ALIMFUNGIA BOBAN NDANI YA WIKI MOJA AKAMFUNGULIA THEN AKASEMA NIMEMSAMEHE LAKINI SIWEZI KUMRUDISHA TIMU YA TAIFA KWANI HAJAONA KIWANGO CHAKE,SWALI MTU UMEMCHAGUA WIKI MOJA ILIYOPITA UMEMCHAGUA KWA KIWANGO KIPI?

    WAKATI MAPUNDA NA NSAJINGWA WALIFUNGIWA NA TIMU ZAO KWA MIEZI SITA NA WALIPOGUNGULIWA TU AKAWACHUKUA BILA KUWAONA.

    WAKATI TIMU YA TAIFA INAKWENDA KWENYE CHALENJI AKAMUITA MRWANDA LAKINI AKAMWACHA KIPA WAKE MAPUNDA KWA KUSEMA HAJAMOUNA, SWALI MRWANDA YUKO QATAR ALIMUONA WAPI?

    PIA KAMA KOCHA PROFESSIONAL KWANINI USIWE NA REPORT ZA WACHEZAJI WAKO TOKA KWA MAKOCHA WANAOWAFUNDISHA MAPUNDA NA MRWANDA KILA MWEZI?

    SALUM SWEDI NA CANAVARO WANACHEZA MCHEZO MZURI NA WANAJUANA KWA VILE WAKO MUDA MREFU PAMOJA LAKINI KUWEKA WACHEZAJI WAPYA KILA SIKU TIMU HAITOFIKKA POPOTE,

    KUJUA KAMA MAXIMO NI LOOSER ANA KAULI YAKE KUWA KAJA KUWEKA MSINGI WHICH MEANS HANA UWEZO WA KULETA KOMBE, NI MUDA MUAFAKA WA KUONDOKA HIVI SASA.SCHOLARI KAONDOKA CHELSEA MABADILIKO YAMEONEKANA,TOTENHAM KAONDOKA RAMOS MAMBO YAMEONEKANA.

    KWA MATUNZO INAYOPATA STARS HATA KOCHA MBARAKA WA ASHANTI AKIPEWA TUTAKUJA NA KOMBE.

    SAWA NA MWALIMU WA SHULE KILA MWANAFUNZI UNAMFUKUZA KWA KISINGIZIO CHA NIDHAMU WAKATI MOJA YA KAZI YA MWALIMU NI KUMREKEBISHA MCHEZAJI.HIVI BOBAN NI MTOVU WA NIDHAMU KUSHINDA ALIVYOKUWA ROONEY?AU GEORGE BEST AU GAZZA?

    ANACHOTUMIA SASA NI KUWA DIKTETA HIVYO WACHEZAJI WATAKUWA NA KINYONGO NA SIO RAHISI SISI KUPATA KOMBE HATA LA MBUZI.
    PIA MSHAHARA ANAOPATA NI MKUBWA SANA KULINGANA NA CV YAKE NDOGO.

    NA HATA TUKIMWACHA HAKUNA TIMU ITAMCHUKUA UTAMUONA YUKO AZAM AU MBAGALA MARKET.ALISEMA MWAKA HUU ANAONDOKA HIVI SASA ANASEMA KUWA KUNA OFFER NYINGI ANAPATA ILA YEYE ANAIPENDA TANZANIA, JIBU ANAPENDA WALLET-POCHI LETU TU.

    JK TUNAOMBA UMPUNGUZIE NGUVU HUYU MTU WASIKILIZENI NA WACHEZAJI,KOSA KAMA LA KASEJA LINA UKUBWA GANI KIASI ASEME LABDA YEYE AFE NDIO KASEJA ARUDI STARS?MOJA YA SIFA YA MWALIMU NI KUREKEBISHA NA KUSAMEHE.MAXIMO ANAWEZA KUISHI NA MALAIKA TU.
    HATA WABRAZIL WENZAKE WAMEMKIMBIA KWA KERO NA GHUBU ALILONALO MAXIMO.

    TUNATAKA KOMBE SIO MSINGI.MSINGI TUNAO TOKA 1980 BENDARA ALITUWEKEA.

    BY THE WAY HILI KOMBE LA CHAN HATA FIFA HAWALITAMBUI HIVYO HANA CHA KUJIVUNIA MAXIMO.MECHI TULIZO SHINDA NI KWA MOTISHA YA JK NA HAMASA YA WANANCHI.
    MDAU KISIJU.

    ReplyDelete
  4. upande wa ubadilishaji wa wachezaji hata hapa ulaya tunaona makocha wanawabadilisha wachezaji kila siku hayo majina ya wachezaji uliyo wataja ambao wako kwenye timu zao za taifa kwa muda mrefu hao ni wachezaji nyota duniani, bado timu ya tanzania inajengwa kwa hali hiyom lazima ukubali mabadiliko ya kila wakati na hayo mabadiliko ndiyo yameweza kutufikisha GHANA. Toka aje Tanzania unaweza kuona mpangilio na mwelekeo wa soka, tatizo bado lipo wenye vilabu vyetu. Na kuhusu hao wajezaji wasio na nidhamu dawa yake ni hiyo agalia Ngasa anajua anacho taka katika maisha yake unapo anza kuonyesha ubabe na ubishi kwa mwalimu wako unajidanganya tu utasaulika sasa hivi wakiwa ni watu wa busara wakae chini waongee na mwalimu wao badala ya uonyesha ujuaji ambao hautawasaidia hiyo niajira yao wasipo iheshimu kazi kwao na mpira ni kitu cha kupita tu.

    ReplyDelete
  5. Da! umenifumbua macho kwa sasa nafikiri huyu kocha ni BOM

    ReplyDelete
  6. Mdau uliyoyasema ni kweli kabisa ila si TFF au mdau yeyote anayeweza kumweleza lolote Maximo na akakubali. Wachezaji wengi wazuri duniani huwa ni watovu wa nidhamu na wengine wanatolewa jela kwenda kutetea nchi na Maximo bila shaka hili analijua, kama wangekuwa wanafukuzwa kama ilivyo kwa Maximo nadhani uingereza wasingekubali kwa Gaza na Argentina wasingekubali kwa Maradona na wengine wengi. Nadhani Maximo haya anayajua ila ninashawishika kuamini kuwa anasikiliza maneno ya "kiswahili"

    ReplyDelete
  7. Huna Hoja ya maana, Geoffrey. Unaleta siasa na chuki dhidi ya Maximo. Tatizo lako kubwa ni kwamba upo one sided. Unaona ni sawa mchezaji akikosa basi aendelee tu kuitwa timu ya taifa. Unatoa mifano ya wachezaji ambao siku zote wanaitwa kwenye timu za taifa brazil, argentina, na uingeleza. Kitu cha msingi ambacho hukizungumzii ni kwamba wachezajhi wa timu hizo wana uwezo wa kumaintain viwango wakati wachezaji wa Tanzania wengi viwango vinapanda na kushuka. Unasema upo objective wakati si kweli. Unataja mifano ya wachezaji ambao wamekuwa wakiachwa kwa sababu ya kushuka kiwango au nidhamu. Lakini upo kimya kutaja wale ambao viwango vyao vipo juu misimu yote na hawajawahi ondolewa kwenye timu, mfano ni Fuso ambaye kiwango chae kipo juu muda wote na hajatemwa hata siku moja kwa sababu za kiwango. Niambie mchezaji gani ambaye amemaintain kiwango muda wote wa maksimo na akaachwa. Acha siasa bwana. Ona timu ya uingeleza sasa. Mtu haitwi na kapelo bila kupandisha kiwango, na matokeo yake uingeleza imeanza kubadilika tofauti na kabla yake ambapo majina ndo ilikuwa kigezo.
    Kaa kimya. Huna hoja. Au ulitaka tujue upo ujerumani nini?

    ReplyDelete
  8. Tatizo ni ngazi ya klabu, ukiangalia wachezaji ktk klabu zao hawadumu ktk kikosi cha kwanza ktk klabu wanazochezea kwa muda mrefu.

    Ndio maana watoto wadogo/wakubwa wa Bongo hawawezi kukutajia kwa uhakika vikosi vya kwanza vya Yanga au Simba au Coastal Union.

    Miaka iliyopita Simba walilkuwa na Mahadhi, Kibadeni, Kajole n.k ktk kikosi cha kwanza cha Simba kwa miaka kadhaa. Pia Yanga kina Kitwana Manara, Omar Kapera, Sunday Manara n.k walikuwa wachezaji wa kikosi cha kwanza cha Yanga kwa miaka kadhaa.

    Sasa turudi kwa Maximo, Maximo yeye anatumia vigezo vya kisasa kuangalia ni mchezaji yupi anapangwa ktk kikosi cha kwanza cha klabu yake. Je mchezaji huyo hudumu ktk kikosi hicho cha klabu au alipata majeruhi yaliyomfanya ashindwe kuwa katika 'hali kamili ya mchezaji bora' n.k

    Ndiyo maana hata David Beckham imebidi atoke Marekani na kuhamia Italy ili kujiwekea nafasi nzuri ya kuchaguliwa timu Ya England. Pia Maximo au kocha yeyote wa Taifa stars anapaswa kupewa tiketi kwenda kuangalia wachezaji wa klabu za Tanzania zinazoshiriki ktk mashindano ya kimataifa, mfano Maximo lazima aende Misri kuangalia wachezaji wa Yanga wata kavyo ikabili Al Ahly huko ugenini Egypt.

    Hivyo Maximo ana mtihani mgumu wa kupata kikosi kamili kwani ngazi ya klabu pia wachezaji wanabadilishwa kila mara au kuchomekwa na wajomba zao ktk timu za Yanga/Simba n.k wakati kimchezo viwango vyao viko chini, wachezaji wazuri wasio na wajomba hawapati nafasi ktk vilabu vya madaraja ya juu.

    Hivyo sio Maximo wa kulaumiwa ila mfumo mzima wa kuwatayarisha na kuwalea wachezaji bora, ndio wa kutupiwa lawama. Michezo ya Copa Coca Cola,Shule/Vyuo/majeshi,Ligi za wilaya/mikoa na kombe la taifa inabidi ilenge ktk kukuza vipaji vya wachezaji bora ii waweze kufikia kiwango cha juu cha kusakata kandanda.

    Mdau
    Rocky
    Jijini London.

    ReplyDelete
  9. MDAU NIMEKUELEWA HOFU YAKO,ILA MAJIBU YANGU NI KUWA WENGI WASISI WAPENZI WA SOKA TUKO EMOTIONAL ZAIDI BADALA YA KUFUATILIA TATIZO.KWA KUANZIA KWANINI ANABADILISHA WACHEZAJI,MARA NYINGI KOCHA ANAEBADILISHA WACHEZAJI ANA MAANA WALE ALIOWATUMIA SIO GOOD ENOUGH,NA HIYO SIO TU KIUCHEZAJI TU KUNA MAMBO MENGI YANACHANGIA MCHEZAJI KUONEKANA HAFAI,MFANO NIDHAMU,COMMITMENT,KUSHIRIKIANA,KUSAIDIANA,KUTOKUWA MBINAFSI,ELIMU YA MPIRA,SASA KAMA WACHEZAJI WETU NI KUKIMBIZA MPIRA,VIPAJI WANAVYO LAKINI ,NO NIDHAMU,ELIMU FINYU UNAJITAHIDI KUWAELIMISHA VICHWA NGUMU,NAONA ITABIDI WABADILISHWE,
    HALAFU KUMUONA MCHEZAJI AKIBAHATISHA GOLI MOJA NA KUKAA NAYE KUMFUNDIHA NI VITU TOFAUTI NA UTAONA MAPUNGUFU YAKE,USIONA NIMEVAA SURUALI HUJUI NDANI NIMEVAA CHUPI GANI LABDA IMETOBOKA.KWA UFUPI YEYE NDIO KOCHA NADHANI ANAJITAHIDI KULETA MABADILIKO KWA HIYO ITATAKE TIME,TUNA MAFAZA WENGI SANA WANATAKIWA WABADILIKE,SIO KUCHEZEA SIMBA AU YANGA NDIO UKOO JUU.
    NI KOSA LAO WENYEWE WASILETE MAJUNGU KAMA HUKUCHAGULIWA AU KUPANGWA SUPPORT THE REST ACHENI UBINAFSI,STARS SIO KASEJA,BOBAN,CHUJI N.K.
    NA HAO AKINA KASEJA NA CHUJI HISTORIA YAO TANGU KWENYE VILABU VYAO NI NADHAMU MBOVU SASA KWANINI MSIWALAUMU?


    OCD

    ReplyDelete
  10. Nadhani moja kati ya sheria za mpira wa miguu ni kuwa uamuzi wa refa ni wa mwisho. nadhani hii sheria iliwekwa makusudi ili kulinda heshima na nidhamu ya mchezo unapochezwa. Kama hii sheria isingekuwepo basi tungeona vituko kadha wa kadha kutoka kwa wachezaji, viongozi na hata mashabiki na labda huu mchezo ungelikuwa tofauti na tunavyouona sasa.

    Nia yangu ya kutanguliza maelezo hayo hapo juu ni kutaka kuweka sawa mawazo ya wadau wa soka hasa Tanzania. Kwa muda mrefu tumekuwa tukisuasua kutafuta namna ya kuleta maendeleo katika soka. Hatua kadhaa zilichukuliwa lakini hatukuweza kupiga hatua za kuridhisha kwani tulikuwa na labda na mipango mizuri lakini tukakosa mbinu (strategies) bora za kutekeleza mipango. Ili soka la Tanzania liweze kukua na kuifanya timu ya taifa iwe bora na imara, hatuna budi sisi wadau ambao tuko mstari wa mbele (Wachezaji wa zamani, viongozi, mashabiki nk) tuanze kufikiria jinsi gani ya kuwekeza katika soka la vijana wadogo. hili ndiyo suluhisho la matatizo yetu. ushauri huu umekuwa ukitolewa mara kwa mara na washauri kadhaa wa ndani na wa nje ya nchi akiwemo Maximo alipofika hapa nchi kuanza kazi. Tumekuwa tukiwapa kazi ngumu makocha ya kuweza kutengeneza timu zetu hasa za taifa kwa kuwa inabidi kocha anze kufundisha wachezaji wetu namna ya kucheza mpira katika basic level. Hii ndiyo reflection ya hali halisi iliyopo katika vilabu vyetu, kwa maana unapoona mchezaji ana behaviour mbaya kwenye timu ya taifa basi ujue huko kwenye klabu level ndiyo ameoza kabisa. Vilabu vingi havijui kulea wachezaji na matatizo haya yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na viongozi na wanachama wenyewe. Wachezaji wanavunja maadili ya uchezaji (kama kuvuta bangi, uchelewaji kwenye mazoezi, kutofuata maelekezo ya mwalimi nk) lakini kwa viongozi na wanachama kwao hilo si tatizo, hatimaye walimu husika hushindwa kufanya kazi zao na timu kutofanya vizuri.

    Ni vema basi tujifunze kumwachia mwalimu afanye kazi zake ikiwa ni pamoja na kuwa-discipline wale watovu bila ya kuwaonea aibu au kufikiria uwezo wao. kwa mfano mtoa mada anaposema kuwa Abdi Kassim alifunga goli bora, that does not have any connection with discipline, hata kama ni bora kwa maoni ya mtoa mada lakini si bora kama mchezaji. Tunataka kuona kuwa wale wote wanaopata nafasi ya kuvaa jezi za national team wanafikia na kukidhi viwango vyote muhimu kama wachezaji. Tunataka wachezaji ambaowatakuwa wanauwezo wa kufuata maelekezo ya mwalimu na ku-maintain nidhamu kwa wakati wote 100%.

    Tumuache maximo afanye kazi na sisi wengine tu-msupport kwa kutayarisha vijana wadogo huku mitaani kwetu.

    Ninaamini wachezaji wazuri wa taifa stars bado tunao huku mitaani kwetu na si wale walioko Simba au Yanga.

    ReplyDelete
  11. Mchezaji Rio Ferdinand anavuta bangi lakini hajatolewa kwenye timu ya taifa ya UK au manchester.

    Maximo ukomo wa uwezo wake umefika sasa anatafuta visingizio kama vyama vya siasa vikishindwa uchaguzi vinakuja na visingizio eti kura zilichapishwa china ukimpia mbowe inakwenda kwa JK.

    wakati vyama vyenyewe hazijiuzi vijijini.

    Maximo hata akikaa miaka kumi kwa utaraibu huu timu haitafika popote,kwani muda si mrefu atawafukuza nsajingwa,sued,shaban Nditi kwa kigezo cha umri.

    swali Mapunda na nsajingwa nani mwenye umri mkubwa kuliko boban?

    kama anataka vijana Nsajigwa ana miaka 34 amfukuze lakini ndio kwanza kampa unahodha.

    yaani kocha mgeni ana sauti kuliko sisi wenye nchi yetu?

    Maximo hajielewi ingekuwa nchi za magharibi wangekuwa wamekwisha mtimua ila sisi tuna asili ya uvumilivu na ujinga wa kubabaikia wageni.

    kila dakika anatusimanga kuwa kakuta nchi yetu haina kitu wala haijui mpira,

    tumewahi kuwa na makocha kama victor na tambwe leya wamefanya mambo mengi lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa akitusimanga kama huyu maximo.

    kikosi kilichotengenezwa na Victor au Tambwe leya maximo hana ubavu wa kutengeneza.

    hivi hajui kama club za simba na yanga zilifanya ziara huko brazili miaka ya 70?

    wiki moja tu alipokuja taifa stars ilicheza na burkina fasso tukashinda kwa nguvu ya jk kwenda uwanjani yaani debe la washabiki.ghafla maximo akajipa credit kuwa kazi yake.sasa kama aliweza kufanya miujiza ndani ya wiki vipi ndani ya miaka mitatu kashindwa kuleta kombe hata la challenji?

    kibaya zaidi mwaka jana tumefungwa na somalia kwenye challenge.na mwaka juzi tuliwafunga kwa msaada wa refa kwenye challenji kagoli kamoja.

    kocha mzuri hupimwa kwa mafanikio ya kuleta vikombe.

    challenge tumeandaa Tanzania mwaka jana na timu haikufika hata robo fainali chini ya maximo.

    kipanda aliweka katuni nzuri sana wakati timu inakwenda Ivory coast alisema maximo amesahu mkoba wa visingizio.

    swali kama kina chuji walikuwa na matatizo toka hapa basi asingewachukua ili nafasi yao watumie wengine.

    pia angesema kuwa katika kambi yangu kuna hili na lile lakini alisema kuwa mambo yako safi,anafika ivory coast anakuja na sababu.
    maximo ni mtu ambaye anaongea hili leo na kesho anaongea kitu kingine.hatufai aondoke.

    ReplyDelete
  12. Mdau mbali na kunena kwako ukweli unabaki kwamba TFF ni taasisi huru na ipo juu ya sheria (kwa mujibu wa FIFA) sasa hawatakiwi kuhojiwa sana
    Pia tuelekeze lawama kwa timu zetu hizi zinazoua soka la bongo (Simba na Yanga)timu kama zile hata e mail hazina si tu website. nyingine hata uwanja wa mazoezi haina!
    utategemea eti izalishe wachezaji na kuisaidia nchi? Heri ya Azam FC kwanza ina website (azamfc.co.tz) wanajua wanachofanya. Pili ina timu nzuri ya vijana yenye benchi la ufundi la kueleweka sio kina Simba na Yanga,upuuzi mtupu.
    Marcio Maximo ana matatizo mengi sana nadhani ni tabia za kibrazil kwa sababu tumeona kwa Scolari alivyoigawa Chelsea kwa kupendelea baadhi ya wachezaji wake huku akiwatupia lawama za waziwazi baadhi ya wachezaji wake na matokeo yake tuliyaona.
    Kwa hiyo kwa soka yetu ya Bongo ili isonge mbele kweli kweli tuna kazi ya ziada kwani mafanikio ya soka ni kama system flani hivi ,hivyo ili system hiyo iweze kua bora ni lazima kwanza sub ststems zote ziwe bora kuanzia uongozi wa TFF,mfomo wa uendeshwaji wa vilabu vyetu,na benchi la ufundi la Timu ya Taifa kitu ambacho kwa hali ilivyo hivi sas ni vigumu kama Dar es Salaam kusnow vile, pata picha Tandale,mburahati,tandika,mbagala kote inasnow kunakua hamna vumbi inakuaje!.

    ReplyDelete
  13. Shukrani mdau kwa kuanzisha mada na kutushirikisha wadau katika kutafuta ufumbuzi wa pamoja.
    Nakubaliana nawe kwamba Maximo kama kocha amejitahidi. Kadhalika JK amewaongoza vema Watanzania kwa kiasi kikubwa kujitahidi kuiunga mkono timu yao.
    Maoni ya kwamba timu ya taifa inabadilikabadilika mara kwa mara yamekuwa yakisemwa mara kwa mara lakini ukiangalia Maximo amekuwa kwa kiasi kikubwa na festi ileven. Piga ua lazima awaite na kuwapanga wachezaji wafuatao: Shadrack Nsajigwa ‘Fuso’, Henry Joseph Shindika ‘Chakubanga’, Salum Swedi Kusi, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Shaaban Nditi, Abdi Kassi “Babi”, Athuman Iddi “Chuji”, Jerry Tegete, Kigi Makasi na Ivo Mapunda. Kumbuka alipoacha kumwita Meshack Abel alisema amemwacha kwa vile ni majeruhi lakini alimchukua Chuji kwenda Abidjani. Kwa maneno mengine wachezaji ambao anawabadilibadili ni wachezaji wa akiba. Japo siwezi kumsemea nadhani nia yake ni kuona viwango vya wachezaji mbalimbali na kuwapa uzoefu wa mechi za kirafiki za kimataifa ili siku wakihitajika kulitetea taifa wawe tayari wakiwa na uzoefu. Hii inaweza kuwa sababu ya Maximo kuwajaribujaribu wachezaji kwenye mechi za kirafiki kwa mujibu wa kalenda ya Fifa. Vilevile sababu ya kutokuwa na timu ya kudumu ni kuacha nafasi kwa wachezaji watakaofanya juhudi kunyang’anya namba za waliobahatika kuitwa. Mrisho Ngassa amenyang’anya namba ya Nditi. Juma Jabu ameng’ang’ania nafasi ya fulubeki left wa kushoto. Tukumbuke kwamba kikosi kilichoenda Brazil kilitandikwa 4-0 na Senegal. Baada ya mabadiliko ya kuimarisha kikosi Cameroon hawakuweza kutufunga 4-0, tena basi nusu tuwatoe nishai hapo taifa. Rigobert Song alishindwa kuongea vizuri na waandishi wa habari baada ya mechi. Kwa hiyo timu inazidi kuimarika. Changamoto ya kujua kwamba huna namba ya kudumu na tamaa ya kwenda kucheza soka la nje inawahamasisha wachezaji walio timu ya taifa na wengineo kucheza kwa nguvu hivyo kuinua viwango vyao. Ndio kina Mwinyi Kazimoto wametokea hapo. Utaratibu wa kutokuwa na wachezaji ‘nyota’ wa taifa upo duniani kote. Ronaldinho ameshawahi kutemwa timu ya taifa kwa utovu wa nidhamu. Sasa hivi kinachoendelea sio wachezaji 11 au 30 kukomaa wakati wengine wakiwa bado na ugeni na kuchezea timu ya taifa.. Kwa mwenendo huu kunaweza kuwa na wachezaji mia kadhaa wenye uzoefu baada ya muda. Mathalan, akimwita Adam Kingwande kuchezea Taifa Stars haitakuwa mara yake ya kwanza. Ameshacheza huko Mauritius.
    Naunga mkono suala la kulipa suala la nidhamu uzito japo siwezi kuzungumzia matatizo ya kinidhamu ambayo yanadaiwa kutokea katika mazingira mbalimbali (Abidjan, Dakar) kwa sababu sina habari kamili za nini kilichotokea. Lakini wachezaji pekee ambao inadaiwa wametofautiana na Maximo katika masuala ya nidhamu ni Kaseja, Chuji, Boban na Maftah. Wengine wamekuwa wakiachwa kwa sababu kuna wengine wameonyesha viwango vizuri vinavyoendana na mfumo ambao kocha anataka kufundisha. Machuppa alipewa nafasi akaonyesha kitete kisicho cha kawaida licha ya kuwa mkongwe. Abdalla Juma ni mfungaji mzuri lakini Maximo anataka mchezo wa kasi mbele. Kama ulibahatika kumwona katika michuano ya Tusker ungegundua kwamba ameji-Ronaldo de Lima kidogo. Ndio sababu alipenda kuwa na SMG pale mbele. Alipotoka akamchukua Danny Mrwanda. CHAN akamchukua Mussa Mgosi. Wote hawa wana sifa ya kasi. Mwaikimba na Costa wamekuwa hawapangwi mara kwa mara katika klabu zao. Naamini kina Admin Bantu na Bunu watakuja kuchezea tu timu ya taifa. Nikumbushe vilevile kwamba kuna wadau waliwaita Kigi Makasi na Jerry Tegete watalii lakini Maximo kwa kuwa ni kichwa ngumu aliendelea kuwapika vijana wake. Sasa hivi asipompanga Kigi tunalaani. Vilevile kuna wakati anasikia maoni ya wadau. Ngassa si yumo? Na amemrekebisha hachezi na jukwaa tena, anasaidia timu. Abdi Kassim ni mchezaji mzuri sana ila msaada wake katika kumsaidia fulubeki wake sio mkubwa kama anaotoa Kigi Makasi. Vilevile Babi anaonyesha kuchoka mapema kuliko Kigi.
    Nawapa pongezi Stars kwa jitihada zao huko Ivory Coast. Nawapongeza vilevile kwa sababu hawakutoa visingizio. Nahodha Nsajigwa amekiri walikosa umakini dakika ya mwisho. Maximo amesema wameonyesha kwamba kweli walienda kushindana. Walipata pointi nne, walimpiga bao mwenyeji. Kwenye kundi B kuna timu ilipata pointi nne ikasonga mbele. Vilevile walifunga mabao mawili wakati Senegal walisonga mbele kwa kufunga bao moja.
    Kitu ambacho tunakihitaji kweli kweli ni kuwa na klabu zilizotulia. Mafanikio yetu yamekuwa yakipatikana tunapokuwa na misingi mizuri klabuni. Stars ya 1980 iliunda na vijana wa Victor Stanslescu. Kili Stars iliyotwaa chalenji chini ya Mziray iliundwa na wachezaji wengi wa Simba-Popadic. Si kazi ya kocha wa taifa kutengeneza vipaji, ni kazi yake kuvitumia. Ndio sababu timu za mataifa yaliyo mbali kisoka yanaweka kambi ya taifa siku tatu tu.
    Tunaweza kutafuta mafanikio ya muda mfupi au tukatafuta mafanikio endelevu. Kama tunataka mafanikio endelevu inabidi tukubali kwamba hayatokei kwa siku moja.
    Nawapa pongezi wadau kwa kutoa maoni yenye lengo la kujenga.

    ReplyDelete
  14. SERIKALI NA TFF WANANA MAXIMO HAKOSEI KILA ANACHONGEA AU ANACHOFANYA NI SAHIHI,

    KIUKWELI NAYE NI BINADAMU NA ANA MAPUNGUFU TENA MENGI TU.

    SASA HIVI NAAMINI KUNA BAADHI YA WACHEZAJI HAWATAMANI KUCHEZEA STARZ KWA SABABU YA KUEPUKA LAWAMA ZA GOD FATHER MAXIMO.

    UMEFIKA WAKATI WABONGO TUACHE KUEGEMEA UPANDE MMOJA, MAANA HAPO TFF HAWANA LOLOTE LA KUFANYA ZAIDI YA KUSAPOTI CHOCHOTE MAXIMO ASEMACHO.

    NAAMINI KESHO MAXIMO AKIAMUKA AKISEMA NGASA AFAI TFF NDIYO NA VIONGOZI WA SERIKALI NDIYO WATAKUWA WA KWANZA KUSEMA KWELI NGASA HAFAI HATA SISI TUMELIONA HILO.

    NACHUKUIA SANA KUBURUZWA KIASI HIKI.
    MAZINGIRA ALIYOANDALIWA MAXIMO HATA MAKOCHA WETU WABONGO WANGEFANYA VIZURI ZAIDI YAKE.

    LAKINI NDIYO TENA KASHIKA MPINI...TUTAFANYEJE

    ReplyDelete
  15. Rocky wa London.unasema kuwa maximo anachukua mchezaji wa kikosi cha kwanza kwenye timu ndio anamchagua timu ya taifa sio kweli.

    maximo alikuwa na kipa Ali mustafa-Barthezi kwa muda mrefu wakati huyo kipa ni namba mbili ya kaseja.lakini maximo akawa anamchagua hapo utajua kama maximo hakuna kitu.

    mchezaji kama DIEGO MARADONA.alikutwa na madawa ya kulevya sio mara moja au tatu mara nyingi lakini msaada alioutoa kwa nchi yake hadi sasa haujafikiwa na mchezaji yeyote.

    hakuna aliyekuwa hajui kuwa maradona ni mteja lakini kwa vile kazi nzuri alikuwa akiwafanyia uwanjani hawakuwa na shida naye.

    kapelo habadilishi wachezaji kila mechi kama maximo na pia hawezi kumuacha mchezaji yeyote anawika kama kina HESKY EMILY kamchukua lakini maximo kuna wachezaji wazuri anawakataa tu kwa jealous yake.

    fanyeni utafiti mechi alizocheza boban kazalisha vyumba vingapi?

    Steven Gerrard wa liverpoool kampiga mtu bar na akalazwa jela na hadi sasa ana kesi mahakamani kama ni nidhamu ndani na nje ya uwanja basi Gerrard anatakiwa afukuzwe timu ya taifa ya england kwa kigezo cha maximo cha 100% nidhamu ndani na nje ya uwanja.

    Maximo kumuacha chuji kwenye Chan ni kosa lililotugharimu sana tungeshinda mechi zote mbili.

    kwa vile yeye mshahara wake unaingia na hana anachopoteza na kadri alivyokaa sana kwetu ndio anapata pesa hivyo kila siku lazima alete jipya "naunda kikosi cha vijana wazalendo wenye nidhamu ndani na nje tena wazalendo"
    tumtafutie malaika awafundishe.

    wachezaji waliobaki stars hata kama wana jambo la kumwambia wanaogopa.au kama wana ushauri kinyume na uoni wake wananyamaza tu.kwani dikteta awaambia hawana nidhamu.

    pia kwanini hao TFF wasiwaite wachezaji wakawasikiliza na maximo nae akasema yake kuliko kuwahukumu bila kuwasikiliza huo ni ujinga.

    maximo bora uondoke hatukutaki.
    mdau kisiju.

    ReplyDelete
  16. Nyie makocha wa bongo bwana!!!! Lazima muwelewe hii sio enzi zile, eti mnaandika maelezo mengi oo mie sijui niko ujerumani blabla nyiiiingi, acheni ufilauni nyie vikorosho, Maximo ndio kachangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza soka mpaka sasa tunaogopeka katika ulimwengu wa soka, wivu umewajaa mpaka mmesha anza usanii eti mimi niko ujerumani oo sjui uchumi wa tanzania sio mzuri, ni unafiki na hamna lolote nyie tulieni na vikorosho vyenu, wacha niwaambie kitu ninyi mnaonyooshe wenzenu vidole, you know why? every body in tanzania ni MWANA FALSAFA!!!! SO, NYIE MNAO ANZISHA HIZO TOPIC ZENU ZA NJAA YA LAZIMA, HUKO NI KUWAFISADI WATU WANAO MUUNGA MKONO COCHA NAMBER ONE BRAIN MASTER MAXIMO!!! ANGALIENI HATA AMERICA KUNA RAIS BLACK NYIE NININININI NYIE!!!

    MAXIMO ATAENDELEA KUWACHOMA MOYO BECAUSE IS GOOD GUY FOR TAIFA STARS.

    FUTURE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    KWA HIVI SASA NIKO AUSTRALIA!!

    ReplyDelete
  17. Tukubali kuwa mfumo wa huendeshaji wa vilabu pia umepitwa na wakati kwani kwenye vilabu hususani Yanga na Simba ambazo ndo timu zinazotoa wachezaji wengi wa Taifa zinaendeshwa kienyeji sana hakuna kabisa profesionalsm. Wadau wenzangu tutamkumbuka George Mpondela alipotaka Yanga kuwa kampuni
    miaka ya tisini nahakika tungekuwa mbali sana kwani Yanga ndo ina funs wengi hapa nchini, hapa nadhani umenielewa!! kama Yanga leo hii 2009 ingelikuwa inaendeshwa as a company over the past 12 or 14 years, watu kama sijui mwenyekiti, katibu, mweka hazina, makomando yosso huu mtililiko wote husingelikuwepo!! Channel ya mapato ya yanga kwa mwaka mzima nadhani inaishia kulipa fadhila kwa waliomchagua mwenyakiti na katibu aah siunajua tena bongo tambarare, nyoo kama tunataka Success hata tukimleta kocha toka wapi staz tutakuwa wa kupewa dozi tu. Ni mawazo yangu tu sijui nyie wadau.

    Maximo tunamshukuru alipotufikisha umefika wakati sasa wa kutuachia timu yetu, aodoke, napia TFF tuleteeni coach mwenye CV nzuri na tena wa kigeni sina maana mbaya kwa ma coach wazalendo, ni mtazamo wangu tu.

    ReplyDelete
  18. Wadau waosema Maximo hafai, lazima wakubali yeye ni mwalimu. Tatizo watanzania karibu wote ni Makocha; kinachoshangaza kwa nini walishindwa kuinyanyua Taifa stars hadi ikabidi watafute huyu Maximo? Tunapokosa Uvumilivu wakati wa kutafuta mabadiliko tutaishia kuwa palepale kila siku....mabadiliko yanaambatana na maumivu na inabidi kujitolea.

    Tanzania hatujawa bado na professional players, so hakuna haja ya kulalama ati wachezaji wanbadilishwa ovyo.....Angalia hii timu unayoiona leo kwenye luninga ikishishiriki Michuano ya Africa sio ile aliyoanza nayo Maximo...hii inaonyesha Kocha anapata kazi kubwa kuibua vipaji na hii inatakiwa ili tuweze kuwa na ushindani kwenye wachezaji kiliko mtu ajijue yeye ni Taifa stars tu no matter what....so tumwache Kocha afanye kazi yake na tuache majungu...kama unaona wewe unafaa kuwa kocha basi apply hiyo kazi uanze kufundisha hata club ya mchangani uone kazi inavyokuwa.

    Mchezaji ili aweze kuchezea team ya Taifa lazima awe professional na consistence ili apate number ya kudumu, lakini wachezaji wetu bongo wakiwika sana ni 5years sasa huu si uzushi tu.

    Angalia Team ya CAF, na selection criteria ili ujue Safari tuliyo nayo watanzania.
    Kwa Bahati Mtanzania ni Musa Mgosi na yeye yupo kwenye reserve list.

    TUSIPENDE KUINGILIA KAZI ZA KITAALAMU. Muda utafika na atabadilishwa Kosha, ila akiwa anaendelea na kazi yake si vema kumuingilia. Je akifuata ushauri wako halafu team ikiboronga utamlaumu?

    http://www.cafonline.com/competition/african-nations-championship_2009/news/2392-mputu-tops-them-all.html

    FAIR PLAY: DR CONGO

    BEST PLAYER: Trésor Mabi MPUTU (DR Congo)

    BEST SCORER: Given SINGULUMA (Zambia)


    BEST ELEVEN (XI)
    Goal keeper
    Mamadou BA (Senegal)

    Defenders
    Samuel INKOOM (Ghana), Ofusu APPIAH (Ghana), Gladys BOKESE (DR Congo), Harrison AFFUL (Ghana)

    Midfielders
    Jonas SAKUWAHA (Zambia), Kazembe MIHAYO (DR Congo), Bongeli LOFO (DR Congo), Moustapha DIALLO (Senegal)

    Strikers
    Given SINGULUMA (Zambia), Trésor Mabi MPUTU (DR Congo)

    Substitutes
    Samir ABUD (Libya) GK, Ovidy KARURU (Zimbabwe), Mussa MGOSI (Tanzania), Ibrahim AYEW (Ghana), Mamadou Baila TRAORE (Senegal), Charles ASAMPONG TAYLOR (Ghana)

    Criteria for Selection
    1. Performance during all matches and consistency
    2. Attitude towards team mates, opponents and officials
    3. Leadership
    4. Influence
    5. Tactical
    6. Skill and talent
    7. Exemplary
    8. Enthusiastic and motivator
    9. Personality
    10. Number of appearances

    ReplyDelete
  19. DISPLINE, DISPLINE, DISPLINE, DISPLINE.MAXIMA WHEN TALKS ABT DISPLINE, HE MEANS, HOW PLAYERS DRESS UP, BEHAVE, BEING ON TIME,BEING AS A TEAM, DOES A RIGHT THING AT A RIGHT ITM eg PASSING THE BALL ON TIME,AND SCORE WHEN GETS A CHANCE.I HAVE MY FRIEND USED TO WORK IN RESTAURANT IN SPAIN. CARLOS AND OTHER BRAZILIANS PLAYERS USED TO EAT THEIR DINNER THERE. THEY WERE THE MOST DISPLANED PEOPLE THAN ANY BODY CAME THERE. THEY EAT DINNER, TIP, TALK TO WAITERS SLOWLY AND RESPECTFULLY AND LEAVE. NOT NATIONAL TEAM PLAYERS, I HAVE SEEN IT. THEY ARE IN CAMP IN EVENING GOING OUT THE CAMP ON STREED SMOKE WEED. GIVE ME A BREAK! INSTEAD OF BEING IN THEIR ROOMS THINKING ABT GAMES AND PRACTICE YOU SMOKE WEEK ON THE STREET? NO DISPLINE NO STARS, YOU OUT I DON'T CARE HOW TALENTED YOU ARE.MAXIMO DOES GREAT JOB SHAPING THESE MOST UNDISPLINED PLAYER. THEY ARE CREAZY, SOCCER IS THEIR CARIER, IT SHOULD BE PROFFESIONAL TO THEM.
    MAXIMO KEEP IT UP THE GOOD JOB AND PLEASE GET THEM STRAIGHT.

    IT IS WHAT IT IS.

    ReplyDelete
  20. MAXIMO ANA MAZURI YAKE NA ANA UBAYA WAKE. MENGI YAMESHAONGEWA HAPA NA WADAU. ZAIDI, NIMEONA HII HABARI YA KUWA ANGALAU KUNA MCHEZAJI MMOJA KWENYE BEST TEAM YA CHAN.NI VYEMA MKAIONA PIA.

    "DR Congo striker Tresor Mputu Mabi has been named the Best Player of the maiden edition of the African Nations Championship (CHAN), which ended in Cote D’Ivoire on Sunday.

    Mputu, who played a pivotal as his side beat Ghana’s Black Stars 2-0 in the final emerged topped in the scheme conducted by the CAF Technical Study Group (TSG) of the tournament.

    Zambia striker, Given Singuluma was adjudged the topscorer with his five goals scored in his team build-up to the third place.The CHAN is restricted to footballers playing in their domestic leagues.

    FAIR PLAY: DR CONGO

    BEST PLAYER: Trésor Mabi MPUTU (DR Congo)

    BEST SCORER: Given SINGULUMA (Zambia)


    BEST ELEVEN (XI)
    Goal keeper
    Mamadou BA (Senegal)

    Defenders
    Samuel INKOOM (Ghana), Ofusu APPIAH (Ghana), Gladys BOKESE (DR Congo), Harrison AFFUL (Ghana)

    Midfielders
    Jonas SAKUWAHA (Zambia), Kazembe MIHAYO (DR Congo), Bongeli LOFO (DR Congo), Moustapha DIALLO (Senegal)

    Strikers
    Given SINGULUMA (Zambia), Trésor Mabi MPUTU (DR Congo)

    Substitutes
    Samir ABUD (Libya) GK, Ovidy KARURU (Zimbabwe), Mussa MGOSI (Tanzania), Ibrahim AYEW (Ghana), Mamadou Baila TRAORE (Senegal), Charles ASAMPONG TAYLOR (Ghana)

    Criteria for Selection
    1. Performance during all matches and consistency
    2. Attitude towards team mates, opponents and officials
    3. Leadership
    4. Influence
    5. Tactical
    6. Skill and talent
    7. Exemplary
    8. Enthusiastic and motivator
    9. Personality
    10. Number of appearances."


    SOURCE:www.cafonline.com

    ReplyDelete
  21. MDAU ULIEILETA MADA HII UKUMBUKE HAPA SIO KIJIWE CHA WANYWA MATAPTAP.KUWEPO KWAKO UJERUMANI BADO HAKUTUTISHI HUNA POINT ZAIDI YA JAZBA DHIDI YA MAXIMO NA HUJIJUI KAMA HUJUI KITU BADO.UNATAKA MAXIMO AKAMSHTAKIE KWA MZIRAY MCHEZAJI ASIE NA NIDHAMU WEE KWELI UMEROGWA KAMA HUJALEWA AISEE!!!KHAAAA!!MZIRAY TULISHAMJADILI HUMU KUWA NI MNAFIKI NA MWENYE WIVU LABDA KAKUTUMIA WEWE UMPIGE ZENGWE MAXIMO NA HAPA UMEUKWAA MWAMBA KWA KIFUPI HILO SAHAU.KUHUSU WACHEZAJI WALIOENDA BRAZIL NA AMBAO BADO WAMO STARS YUPO NDITI,SALUM,HENRY JOSEPH, SUED,NIZAR,NSAJIGWA,BABI, CANNAVARO NA MAFTAHA.HAO WOOOTE WALIKUWEMO IVORY-COAST SASA HAPO SIJUI WEE ULITAKAJE MDAU???NA MAXIMO SIKUZOTE ANAKWAMBIA UWEPO WAKO STARS SIKUZOTE INABIDI UUPIGANIE USIJIBWETEKE UKADHANI UMEGONGELEWA MISUMARI NEVER!!HIVI WEE TUAMBIE NI YUPI AMBAE ALIENDA BRAZIL HAYUMO STARS LEO NA BADO ANAWIKA KWENYE KLABU YAKE????MTU KAACHWA HADI KWENYE USAJILI KATIKA TIMU YAKE KIWANGO KIMESHUKA LEO UNATAKA MAXIMO AMWITE KISA ALIENDA BRAZIL MY ASS"KUHUSU NIDHAMU BOBAN HILO LIPO WAZI HAJAANZA KUPEWA ADHABU LEO WALA JANA NA SOKA BILA NIDHAMU HALIENDI KAKA SIJUI DADA MANAAKE HUJATAJA JINSIA YAKO.NINA UHAKIKA MAXIMO HAMUONEI WALA KUMPENDELEA MTU WAULIZE WACHEZAJI WA MUDA MREFU STARS WATAKWAMBIA.NA HUYO BOBAN UNAEMSEMA KAMA ANGEKUWEPO STARS TUSINGEFUNGWA JIULIZE KACHEZA MECHI NGAPI STARS KAMA MSHAMBULIAJI NA KATUFUNGIA GOLI NGAPI HADI SASA??KISHA ANZA KUROPOKWA.MECHI WALIOSHINDA STARS HAO MNAOWAITA MASTAA WALIKUWA JUU JUKWAANI NA VIJANA WAKAFANYA KAZI.KIFUPI BONGO HAMNA STAR WACHEZAJI WENGI VIWANGO SAWA.KUHUSU TEGETE MJOMBA NI NYIE NYIE WALEVI MLIOKUWA MKIMKANDIA MAXIMO KWANINI ANAITA WATOTO STARS NA NGASSA PIA LEO MMESAHAU UBONGO WA SISIMIZI NYIE KHAAAA!!!MWISHO STARS SIO MAHALA PA KUVUTIA BANGI,UVUTAJI WENU WA BANGI MTATUHARIBIA VIJANA WETU KATIKA SOKA HAO WOTE WALIOTAJWA ULIZA BACK GROUND YAO KAMA UNAWASOMA TU KWENYE MEDIA NI MAJIKO KAMA SIO MATANURI KWA HIO SIGARA.MAXIMO OYEEEEEEEEEEEEEE.

    ReplyDelete
  22. WADAU WOTEEE MMEONGEA NA KUTOA POINTS ZENU NA PIA MITAZAMO YENU LAKINI MIMI NAKUJA MASWALI YANGU KUHUSU MAXIMO NA SOKA LA TANZANIA KWA UJUMLA
    1. MAXIMO ALIIKUTA TANZANIA IKO NAFASI YA NGAPI KATIKA VIWANGO VYA FIFA?....
    2. JE AMEIFIKISHA NAFASI YA NGAPI MPAKA LEO HII??...
    NB. jibu la 1 & 2 yatakufanya ujue kama tumepiga hatua au laah katika soka (ubishi hakuna)
    3. JE ANAMEBADILISHA NIDHAMU YA WACHEZAJI WA TANZANIA AU BADO HASA WANAOONJA MAFUNZO YAKE STARS?..
    4.JE ANACHAGUA WACHEZAJI KWA KUANGALIA NIDHAMU YAO WAKIWA KWENYE VILABU VYAO AU TAIFA STARS?...
    NB.jibu la 2&3 yatatoa mwanga wa kuhusu swala la nidhamu ya wachezaji na pia Maximo
    5.ANACHAGUA WACHEZAJI KWA KIWANGO UWANJANI AU KWA KUANGALIA KILABU ANAYOCHEZEA??
    6. ANAPOTEUA HUWA ANAWAONA WWAKICHEZA AU PIA ANATUMIA TAARIFA ZA MAKOCHA WENGINE??
    NB. jibu la 5&6 yatakupa mwelekeo wa uwezo wa Maximo katika kuinua vipaji
    7. JE KATIKA UFUNDISHAJI:TACTICS NA TECHNICS ZAKE ZINAKUBALIKA NA WACHEZAJI??
    8.JE ANASIKILIZA BENCH LA UFUNDI AU YEYE NDIO ALFA NA OMEGA??
    NB. majibu ya 7 & 8 yataonyesha uwezo wake kama kocha au yeye ni meneja
    9. ALITUMIA KIGEZO GANI KUMPA NSAJIGWA UKAPTENI WAKATI ALIKUWA NA KAPTENI IMARA ALIYEKUWA ANAMTUMIA BAADA YA MAXIME??
    10. JE NI KWANINI ALIMPA UKAPTENI NIZAR KWENYE MECHI 2 ZA MWISHO IVORY COST?
    N.B. majibu ya 9 & 10 yatoa mwanga kuhusu uwezo wake wa kutoa motisha na pia kutawala timu na kutoa maamuzi muhim wakati muafaka!!
    NI HAYO TU KAKA MICHUZI
    "hakuna rangi tutaacha ona"
    mdau nora ttamo

    ReplyDelete
  23. THANK YOU ANON WA 9/03,03.38,JAMAA HANA HOJA NI YALEAYALE MAJUNGU YA KINA MZIRAY,UKO UJERUMANI SAWA,PATA WASIFU WANGU,NIMEZALIWA OCEAN ROAD,NIMESOMA MNAZI MMOJA,KINONDONI NA KIDATO CHA SITA TAMBAZA,NIMECHEZA MPIRA BONGO HADI KUFIKIA NGAZI YA TIMU YA VIJANA MKOA WA DAR 1979,KATIKA MASHINANDAO YA KOMBE LA MWENGE YALIOFANYIKA MTWARA.KABLA YA KUTIMKIA MAJUU KUTAFUTA ELIMU NA MAISHA,NAISHI UPTON PARK,GREEN STREET/CLEVERDON ROAD.NIKIWA BACK GARDEN(UWANI)NAUNGALIA UWANJA WA THE HAMMER(WEST HAM).NAUDHURIA KILA NAFASI INAPO NIRUHUSU KUONA MECHI NA NIKIWA BONGO SIKOSI UWANJANI,YAKO YA MSINGI NA PUMBA ULIO ZUNGUMZA,HUU SIO WAKATI WA KUTURUDISHA NYUMA KWA KINA MZIRAY KATIKA TIMU YA TAIFA,SCORARI ALIWAHI KUMPIGA CHINI ROMARIO KWA UTOVU WA NIZAMU NATIMU IKARUDI NA KOMBE LA DUNIA,WAKATI HUO ROMARIO ALIKUWA JUU,TAMBWE LEYA ALIWAHI KUIBADILISHA NUSU YA TIMU YA YANGA 1974,KUINGIZA WACHEZAJI WASIO KUWA NA MAJINA MAKUBWA WAKATI HUO,JUMA SHABANI,SELEMANI SAIDI,JELA MTAGWA,MOHAMEDI UGANDO,MOSHI ALLY,ALLY YUSUPH,JUMA MATOKEO,NA KUCHUKUA WENGINE KUTOKA YANGA KIDS,JUMA PONDAMALI,JAFARIA ABRAHAMANI,MKWECHE,GORDIAN,KASIM MANARA,SULULU,TOSTAO NA WENGINE NA UBINGWA WAKARUDISHA TOKA KWA SIMBA NYAMAGANA.KAMA KUNA WACHEZEJI WANAOJIONA MAFATHER NA WATOVU WANIZAMU HAWANA NAFASI TAIFA STARS,WAKAVUTE BANI ZAO AU WAKAUZE NDIMU.MAXIMO AMEFANYA KAZI KUBWA NA KWA MUDA MFUPI TUMEONA MATOKEO,MABADILKO YA SOKA AYAWEZI KUJA KAMA UYOGA.KAMA UMETUMWA MWAMBIE ALIEKUTUMA KUNA WATANZANI WENGI NA TUNA UWELEWA WA SOKA TOKA ENZI YA YANGA KUMFUNGA SAINT GEORGE YA ETHIOPIA 6-0,NAKUTOLEWA KWA SHILINGI NA ASANTE KOTOKO YA GHANA TUNAJUA WAPI TULIKO TOKA NAWAPI TUNAENDA KATIKA MUDA HUU MUAFAKA KWA MSAADA WA SREKARI POLEPOLE TUTAFIKA.MAJUNGU SIO MAHALA PAKE.

    ReplyDelete
  24. NAKUPONGEZA SANA MDAU KWA MADA NZURI KWA POINT ZAKO HAKUNA UIBISHI LABDA MTU AMUE TU KUPINGA ILA UKWAELI HUWEZE KUWA NAKIKOSI IMARA CHA TAIFA BILA KUWA NA WACHEZAJI AT LIAST 11 WA UHAKIKA NA WENGINE NDIO HUWA WANAWEZA KUBADILIKA KULINGANA NA SABAUBU MBALIMBALI KWA UPANDE WANGU MIMI NAAMINI MAFANIKIO TULIYOYAPATA SI KWA SABABU YA KUWA NAKOCHA BORA ILA NI KWA SABABU YA KUWA NA MWAMKO KAMA ALIVYOSEMA MJUMBE MFANO MZURI NI WAKATI MAN U WALIPOCHUKUWA UBINGWA 1999 MWAKA ULIOFUATA WALIUZA BAADHI YA WACHEZAJI TEGEMEO KAMA VILE BECK, STARM,YORK NA KUSTAFU KWA KIPA WAO NA MBAMOJA ILIWACHUKUWA TAKRIBANI MIAKA KUMI NDIO TUNAONAMANU WAKO KWENYE FORM SASA IWEJE LEO UBADILI KIKOSI KILA MECHI UWE NA MAFANIKIO?
    NA MBAYA ZAIDI UNABADILI KIKOSI KATIKATI YA MASHINDANO INAANA UTAKUWA UNAFUNDISHA KITU KIMOJA TU KILA KUKUCHA HII HAILETI MAAANA KABISA IKUMBWUKWE HATA KOCHA WETU MZIRAY ALIONGEA SANA KUHUSU HILI LAKINI KWA CHUKI BINAFSIAKAPINGWA SANA ILA UKWELI UPO PALEPALE BADO PARFOMACE YA UCHEZAJI WATIMU YETU YA TAIFA UKO CHINI SANA
    MIMI MDAU FINLAND

    ReplyDelete
  25. Mi naona huyu Maximo afungashe virago ende kwao, hajui hela ya walipa kodi ndo inayomuweka hapa Tz, kama ni ukomo kafika ende zake kwani hata ma-commentator wa mechi ya kwanza walilalamika kua haiwezekani ndani ya dk 45 kocha ufanye mabadiliko kwa wachezaji 2, its unprofesional. Pia ikumbukwe kocha wa Ethiopia aliwahi kusema kwa mtindo tunaocheza (tunaofundishwa) si rahisi kushinda. Kocha mwenzie alishaona mbali zamani.

    Kina Tenga kama kazi inawashinda nanyi mtwambie huyo atimue hana jipya kwa sasa kwani anajua kua hana kitu sasa kaishiwa anabaki kudai watu hawana nidhamu au anataka awale tigo ndo ajue watu wana nidhamu?

    ReplyDelete
  26. kwani mwalimu akikufundisha si anataka ufaulu jamani (walio wengi) na kocha ni hivyo2. Anategemea ufuate maelekezo yake na uwe na nidhamu pia, si mkubwa, si mdogo. Hata kama ni wewe, boss wako ofisini uki-misbehave inakuwaje? tuache MAXIMO afanye kazi jamani. Mie sku hizi napenda kuangalia stars kwasababu kiwango chao kipo kiwango. Kocha mzuri sku zote ni yule anayeweza kubadili mchezaji na bado timu isiyumbe. MAXIMO anaweza hii biashara na wala si kwasababu anaripoti juu tu. MAXIMO angekua anasikiliza waswahili unafkiri tungekua wapi nyie wanafiki? Waswahili mpende watu wanoperform jamani na muwape sifa zinazostaili. MAXIMO amebadili kabisa soka letu utake usitake. Ambao hawamtaki, ni hao wanaleta ushabiki, sisi wengine hapa tunaangalia performance ndio tunamjaji mtu. Unafkiri kwanini mpaka JK anaamua kwenda mwenyewe TPA; ameona watu wapo lkn hakuna cha maana wanachofanya kazi majungu tu na uswahili mwingiii. Msilete uswahili kwenye professional JOBS. Tunataka nchi hii iendelee zaidi na zaidi ktk nyanja zote na sio kukumbatia mambo ya kijinga ambayo hayajengi. Mwacheni MAXIMO a-discipline wachezaje wawe na adabu sio mchezaji anajiona mjuaji hlf analeta NYODO.

    ReplyDelete
  27. kuna watu wameujua mpira wakati waujio wa maximo hawa ndio tunabishana nao hapa.hawajui chochote zaidi kumsifu maximo na kumuona kama Mourinoh wao.
    tusipoteze muda na hawa kama wanamtaka maximo wamlipe wao.
    mdau kisiju.

    ReplyDelete
  28. Wadau mnaotoa hoja za masuala ya nidhamu na bangi kutokuwa muhimu kama mchezaji akiwa na kiwango cha juu mna mifano mizuri. Maradona, Cantona, Rooney, Gerrard, Rio Ferdinand wote ni mifano mizuri ya mifano mibaya. Lakini turudi nyumbani kwanza. Tunaye Maradona kati ya wachezaji wetu? Tunaye mchezaji mmoja anayeweza kushinda mechi peke yake? (Napoli ilitwaa ubingwa na Maradona, ikashuka daraja Maradona alipoondoka).
    Sasa hivi tunajitahidi walau tuweze kutoa wachezaji wawili watatu wapate nafasi ya kucheza soka ya kulipwa katika mataifa yaliyo juu zaidi yetu kisoka. Mchezaji akitoka atakuwa balozi atakayesaidia kuwatoa na wenzie. Tunataka kupata balozi asiye na nidhamu ya kichezaji? Tunataka kupata balozi mvuta bangi?

    ReplyDelete
  29. Katika habari inayohusiana na hii, CAF wametoa ranking zao za CHAN kama ifuatavyo:
    Final ranking
    DR Congo
    Ghana
    Zambia
    Senegal
    Tanzania
    Zimbabwe
    Libya
    Cote d’Ivoire
    Timu nne za juu zilicheza nusu fainali. Katika ambazo hazikucheza nusu fainali Tanzania ndio iko juu. Kweli Maximo hawezi "kutufikisha popote".

    ReplyDelete
  30. Wadau,
    Nimefurahi kuona maoni yenu pia. Kwa wale wanaoona Maximo aondoke, ni maoni yao na mimi wala sikuzungumzia juu ya uwezo mdogo wa Maximo. Na nilionesha wazi kuwa namuunga mkono kwenye mambo ya nidhamu ila namna ya kuipima na ku-manage hizo nidhamu anahitaji ajifunze. Yeye ni binadamu kama sisi tu. Pia, nilitoa changamoto kwa TFF kutimiza wajibu wao kwa kufuatilia maendeleo ya wachezaji kila siku kuanzia mazoezi hadi mechi, uwanjani hadi nje ya uwanja. Akionekana kukosea anaitwa kuonywa, kukatwa posho,kufungiwa baadhi ya mechi na kuelekezwa cha kufanya. Na hii ni kazi ya kamati ya ufundi ya TFF ya akina Kayuni. Nidhamu ni lazima ila anayei-determine ni Maximo na hukumu anatoa yeye. Lakini ana nafasi ya kujifunza namna ya ku-handle wachezaji kwa kuwa yeye anataka vijana na hao vijana hawajakomaa. Hivyo ategemee "vurugu" za hapa na pale. Hivyo ni jukumu lake kuwanyoosha as long as wako tayari kujifunza na wana viwango.Ukichunguza kwa undani hasa hasa - mazingira mazuri ya kisoka ndiyo yanatufanya tuone tumepiga hatua. Kumbukeni enzi za FAT, mambo yaliendeshwa kimitindo. Na serikali haikuunga mkono kabisa. Kumbukeni viongozi FAT waliondolewa na serikali ila FIFA wakatufungia, baadae tukasalimu amri (enzi za Kapuya). Baadae ikaonekana FAT ma-deal mengi na vurugu tu. Mpira ulikuwa chini ya akina Gulamali. Hakukuwa na stability kwenye mpira hivyo kutuzuia kusonga mbele. Sasa ni tofauti. Ukitaka kuamini hili tuwe wakweli. Kama mazingira ya sasa kisoka (i mean stability ya TFF, mabilioni ya wadhamini, support ya serikali na mwamko wetu wadau) yangekuwa enzi zile za akina Kizota, Gaga, Masatu, Dan Mhoja, Fumo, Makerere, Nteze, Ramadhani Leny, Mogellas (Method na Zamoyoni), Lunyamila (akiwa mtoto Stars), Washokera, Novatus, Sekilojo, Mziba,Malota, Hussein Masha, Sikinde, nk hivi vikombe vya challenge si vingekuwa kwao ni Dar? Mdau mmoja kauliza maswali muhimu sana. Wakati anawachagua anazingatia hayo yote? Anaomba ripoti za makocha wengine? Anabadili kikosi wakati gani? Wadau, kukaa kimya ni kutomuunga mkono Maximo. Mkitoa maoni ya kujenga mnamsaidia. Lakini pia si vizuri sana ukapenda upewe comment nzuri tu na zile za kukupa changamoto ya kukufanya uji-rejuvinate huzitaki. Kuna watu wengi na hata viongozi maeneo mbali mbali wenye tabia hii.Haisadii in the long run. Unahitaji kuwasikia wengine wanaonaje na then unapima kuona lipi uchukue lipi uache. Hata hapa kwenye maoni, wala sikutegemea eti wadau woooooote mtaunga mkono 100% hii mada. Huu ndio ukomavu na njia za kujifunza. La sivyo, kila siku utabaki na vile vile unavyovijua tu. Hutaongeza kitu. Hivyo nasi hapa ni nafasi yetu ya ku(ji)elimisha. Core message ya mada ni TFF kutumia nafasi yake kufuatilia wachezaji na kuwasikiliza na kuwa-link na mwalimu. Ile timu ni ya TFF (kwa niaba yetu) na wala si ya Maximo.Suala la eti mtoa mada anataka tujue yuko wapi wala si la msingi hapa. Naamini wadau wote humu tumekomaa na suala la kutumwa na mtu wala haingii akilini. Naomba tujadili namna ya kuhakikisha management ya Timu ya Taifa (na hata vilabu vingine) ina-improve day-after-day. Wasi wasi wangu ni kuwa Watanzania watakata tamaa mapema na kurudi nyuma kwenye kutoa support yao kwa Stars. Tunaona ujaaji wa watu Taifa siku hizi ukilinganisha na 2007? Watanzania wanafuatilia kwa makini maendeleo ya Timu hivyo wote tuwe pamoja na sio kumwachia Maximo pekee. Kama anavyosema Maximo "Tupo Pamoja"!!! Kuna msemo maarufu naurudia "THERE IS ALWAYS A ROOM FOR IMPROVEMENT".

    Geoff Mwambe
    Mannheim, Germany

    ReplyDelete
  31. Wadau wa soka,
    Nashukuru tena kwa maoni yenu. Inanifariji kuona mpo watu wenye misimamo ya kuona tunaendelea mbele. Ni wazi kabsia kuwa tunahitaji sana kuwa wawazi, wakweli na kusimamia yale tunayoyaamini siku zote. Lengo wala siyo kumpiga majungu Maximo ila kama binadamu naye anahitaji ajirekebishe kwa upande wake. Awe mvumilivu na ajue namna ya kuwalea wachezaji. Kama mwalimu anatakiwa awe amesomea Saikolojia (hata waalimu wetu wa shule zote huko nyumbani husomea hilo) ya wachezaji na Management. Kama hajasomea haya basi kuna kasoro kwenye CV yake. However good one can be in terms of footballing skills, kama hajabobea kwenye saikolojia basi ana mapungufu. Ni lazima ajifunze kufanya kazi nasi.

    Lakini zaidi, ni TFF. Wameacha Maximo afanye anachotaka. Hii si sahihi hasa kwa kulea wachezaji ambao yeye mwenyewe ndiye aliyewachagua. On technical grounds, kama kushuka kiwango nk ni wazi ni jukumu la mwalimu pekee. Ingawa nalo kunahitaji yeye ashirikiane na makocha wa vilabu kuhusu maendeleo ya wachezaji anaowahitaji Taifa. Hii ndio soka ya kisasa. Ila suala la nidhamu nk ni la ki-management zaidi. Kuna wachezaji wanafukuzwa kwenye klabu eti kisa kadai mishahara ya miezi minne. Ni haki yake na anaishi maisha ya kubangaiza mtaani wakati kuna viongozi wanajineemesha na mapato. Ukiuliza viongozi wanasema mchezaji hana nidhamu. Wengine kisa ametoa maoni ambayo viongozi hawakuyapenda. Ni muhimu TFF kujua mchezaji halazimiki kuchezea Taifa ila anajitolea. Hivyo ni muhimu kuthamini mchango wake na kwa kuwa wengi ni chini ya 23 (refer Maximo interview in CAFONLINE.COM) years, ni muhimu kuwalea na kuwafanya wajue jukumu lao, nidhamu na mbinu ya kuhifadhi hayo ili mpira wake ukue na aweze hata kupata timu nje. Kuna wakati nilisikia TFF imeandaa semina kwa wachezaji wa Taifa. Semina juu ya mambo ya UKIMWI, NIDHAMU, WAJIBU, nk. Hii ni nzuri lakini ni more eventual than normal monitoring ya mchezaji mmoja mmoja. Na kama kuna tatizo limebainika, chap chap mchezaji anawekwa chini, pigwa shule na kama kuna adhabu za kumpa mnampa and then anajifunza. Kama mchezaji akikosea anatupwa nje ya timu moja kwa moja, je, si wale wote wanaopatikana na makosa mahakamani (hata kosa la matusi) si tungewaua wote? Lakini hatufanyi hivyo, bali wanatozwa faini, wanaonywa, wanafungwa, nk na baadae wanarudi kutumikia Taifa (ingawa jela nako hufanya kazi za Taifa pia). Hii ndio njia mojawapo ya kuweka misingi ya soka la kisasa. Sasa wakati wa FAT, kiongozi anamwambia mchezaji huna nidhamu na huchaguliwi tena timu ya Taifa mimi nikiwa hapa. Na sasa, wakati ambao tunaamini kuna mabadiliko makubwa ya kiuongozi TFF, kocha anafanya hayo hayo ya enzi zile. Sasa tofauti iko wapi?

    Wadau tuendelee kutoa maoni ili kama kuna jema litaonekana na TFF na Maximo (of course na serikali pia) walichukue. La sivyo, wapuuzilie mbali ilimradi tumeshiriki kujenga nchi.

    Geoff Mwambe
    Mannheim, Germany

    ReplyDelete
  32. Wanaonshangaa Mgosi kuchaguliwa kwenye orodha ya wachezaji bora Chan.hao hawaujui mpira.huko nyuma kulichaguliwa timu ya Africa first eleven tulikuwa na Omar Mahadhi na Dilunga.sio mchezaji wa akiba kama mgosi.

    Maximo ondoka tena huyu wakiombwa na mbagala market hata kwa dola mia tatu kwa mwezi atabaki kwani hana pa kwenda.

    kocha wa kimataifa huwa na agent wake na mwanasheria wake hao ndio wanaozungumza kwenye offer yeyote lakini maximo yeye ndio wakili na yeye ndio agent na yeye mwenyewe ndio biashara yenyewe anakwenda kuongea na kina tenga aongezwe mkataba.
    Maximo ondoka.
    mdau kisiju.

    ReplyDelete
  33. DISPLINE, DISPLINE, DISPLINE,GOOD JOB MAXIMO. MAXIMO IS RIGHT, TO PROVE HIM LETS DO DRUG SCREENING THEN MTANIAMBIA WHAT'S UP. HATUTAKI TEAM YA WAVUTA BANGI TUNATAKA PROFFESSIONAL. I WAS SO EXCITED TO SEE STARS DRESSING SUTI. THAT'S PRO. HATUTAKI WAVUTA BANGI. PLEASE DRUG TEST. KEEP IT UP MAXIMO, YOU ARE THE MAN.

    IT IS WHAT IT IS

    ReplyDelete
  34. Mdau nimeharau comment zako baada yakuona eti unasema Mwaikimba, Cosma,Admin,Kipao etc wanawika ktk timu zao!kweli uko Germanyhivi kati ya hao umesikia hata mmoja yuko ktk first eleven ya timu yake?sasa unataka Maximo amuache National team kufata nini?Tatizo wachezaji wengi wa TZ hawana consistency, akiwika miezi 3 basi, soka limeisha,hii ni kwa kuwa hawana malengo!huwezi kufananisha na wakina Rooney na wengine uliowataja.Na hiyo ndio tofauti.Usimlaumu Maximo eti anabadili timu kila siku,kama mchezaji ameshuka kiwango kwa 60% abakie ktk timu anafanya nini?Angalia Salum Swedi, amekosa mechi moja tu tangu maximo kaanza kufundisha,tena kwa kuwa alikuwa na Red Card.Nakuhakikishia only one match (najua hujui hilo). Ngassa tangu aingie ktk timu kakosa mechi 1 tu ya Cape Verde, tena alikuwa majeruhi.Hao ni mfano, uone wachezaji wenye malengo wakati wote viwango viko juu!na Maximo hathubutu kuwaacha.Sio wachezaji wanaochochewa kucheza na cannabis!MAXIMO IS THE MAN. Juzi kocha wa Zambia kauliza popn ya Tz,akaambiwa 40M, akasema "no wonder 15M watakuwa wanajifanya ni makocha,thats african soccer"

    ReplyDelete
  35. march10,2009 11:51 AM.BIG UP SANA MWENYE MACHO ATAONA NA MWENYE MASIKIO KASHASIKIA NIMEPENDA POINTS ZAKO HAZINA TOFAUTI NA ZA MTU MWENYE phD.HUYO BWANA HUKO GERMANY ABEBE TU BOKSI LAKE SOKA HALIJUI ASIVAMIE FANI ZA WATU ETI MWAIKIMBA,KIPAO MY ASS!!NI KWELI SUED AMEKOSA MECHI 1 TU STARS TANGIA AITWE MA MAXIMO.SUED NI MCHEZAJI AMBAE ANA NIDHAMU KUANZIA MUDA,UWAJIBIKAJI NDANI YA PITCH HADI UTORO KAMBINI + PUNCTUALITY.MTIZAME NIZAR KHALFAN,NDITI SHABAN,HENRY JOSEPH.HAO WOTE WANA NIDHAMU YA SOKA NA MALENGO TOFAUTI NA WACHEZAJI WENGI WA KIBONGO AMBAO HAWANA DISPLIN NA DISPLIN SIO KUTOKUVUTA BANGE TU UWAJIBIKAJI NDANI NA NJE YA UWANJA.HARUNA ALISHATUMIWA TICKET NA STARS KUTOKA OMAN ANAKUJA BONGO BADALA YA KWENDA RIPOTI KAMBINI ANAFIKIA MASKANI KULA BANGE SIKU YA TATU NDIO ANAKUJA MAZOEZINI ETI KURIPOTI KWANINI MAXIMO ASIMTIMUE MVUTA BANGE KAMA HUYO???KWANZA KAIFUNGIA MAGOLI MANGAPI HIO TAIFA STARS JAMANI????MANAAKE SITATAKA KISINGIZIO NAFASI ANAYOCHEZA NI CENTRE STRIKER LAZIMA AWE KASHATUFUNGIA GOLI LKN HAJAWAHI KUTUFUNGIA NA HANA DISPLIN NA KINGINE LUGHA NAYO HAIJUI NA WABONGO MNAWAENDEKEZA WACHEZAJI WAHUNI PASI SABABU.POPULATION 40MILLIONS KWELI LAZIMA TUWE NA MAKOCHA WA SOKA KAMA 15MILLIONS AMBAO WANAILILIA NAFASI YA MAXIMO WAKIONGOZWA NA BABA YAO MZIRAY.UKOCHA SIO MAKALIO JAMANI KWAMBA KILA MTU ANAYO ANAYO.

    ReplyDelete
  36. brazil ina watu zaidi ya milioni mia na hamsini unalijua hilo?
    hatufai aondoke zake amekula pesa zetu zinatosha.
    mdau kisiju.

    ReplyDelete
  37. WADAU NAFURAHI KUONA SHAUKU YENU YA KUONA MAENDELEO YA TIMU YA TAIFA.
    KWA MTAZAMO WANGU, MAXIMO AMEREJESHA TUMAINI LILILOKUWA LIMEPOTEA NA KWA KISASI KIKUBWA WATANZANIA WENGI WAMERUDISHA MAPENZI YAO KWA TIMU YA TAIFA. TULIKUWA TUNAPATA VICHAPO VYA AIBU KILA MASHINDANO. TULITUMIA MAKOCHA WOTE WANAOJULIKANA TANZANIA LAKINI BADO HAKUNA MUUJIZA ULIOTOKEA.
    KWELI SWALA LA DISCIPLINE (NIDHAMU) NA WACHEZAJI WANAOTAJWA KUACHWA WANA NIDHAMU MBOVU. NIDHAMU NI MUHIMU KATIKA MPIRA NA INASAIDIA KUFATILIA MAZOEZI NA KUMFANYA MTU KUWA NA UTARATIBU WA KILE ANCHOFANYA. KWA MCHEZA SOKA UNAHITAJI KUWA MBUNIFU ILI KUWEZA KUTUMIA NAFASI ZINAZOPATAIKANA UWANJANI UKISAIDIWA NA MAFUNDISHO YA KOCHA. UKIWA NA BANGI KICHWANI NI NGUMU SANA KUWA NA UMAKINI. SOKA NI KIPAJI LAKINI KIPAJI LAZIMA KICHUNGWE NA KUNG'ARISHWA ILI KIWE BORA. WACHEZAJI TULIO NAO NI WAZURI LAKINI HAWAKUWA NA MWANZO MZURI HIVYO INAKUWA KAZI KAZI KWA KOCHA KUFANYA NAO KAZI KIRAHISI. MTU ANA KIPAJI KIZURI LAKINI AMEKULIA KATIKA MAZINGIRA MAGUMU NA KWA BAHATI AMEFIKA LIGI KUU, HUYU MTU SWALA LA NIDHAMU YA SOKA LITAKUWA GUMU.AMEZOEA FREE-STYLE SASA WEWE UNALETA MIFUMO YA KUCHEZA SOKA NI LAZIMA ITAKUWA NGUMU.. PIA ELIMU NI TATIZO SANA MAANA ELIMU INASAIDIA KUKUFANYA UWEZE KUTAMBUA KUWA UNAHITAJI KUFAHAMU JAMBO, INAWEZA KAUTARATIBU KA KUFATILIA MAMBO, NA SOKA LA KUVUTIA LINA NJIA ZAKE NA STYLE ZAKE HIVYO UMAKINI NI MUHIMU. .
    TUWE WAZALENDO LAKINI TUSIACHE KUWA MAKINI KWA MAmBO AMBAYO NI YA KAWAIDA NA YAKO WAZI.. MAXIMO AMESAIDIA SANA NA MIMI NINGEPENDA APEWE MUDA ZAIDI. PIA SHULE KAMA MAKONGO NA JITEGEMEE ZIPEWE SUPPORT ZAIDI ILI KUKUZA VIPAJI VYENYE NIDHAMU. PIA ATA SERIKALI(WIZARA YA MICHEZO NA ELIMU) KUPITIA TFF WAANZISHE PROGRAMU ZA KUTAMBUA NA KUENDELEZA VIPAJI.. VIPAJI VYETU VINGI VINAPOTEA KWA KUKOSA MIONGOZO THABITI.. SO MAXIMO APEWE UHURU NA TUACHE SIASA MAANA NI LONGO LONGO ZISIZOSAIDIWA NA UFANISI WA MATENDO..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...