Mazishi ya Kiongozi wa Wapiganaji Prof. Karim Hiji aliyezikwa makaburo ya Njiro jana. Picha hizi ni wakati wa sherehe za kuuaga mwili wa marehemu kwenye viwanja vya General Tyre zilizokusanya maelfu ya watu kutoka Arusha na kwingineko nchini na hata Malawi, Kenya na Rwanda.
Famili ya Marehemu Prof. Hirji. Katikati ni mkewe akiwa na watoto wawili wa kiume na mmoja wa kike na shemeji yake Firoz (nyuma).
Waliokaa kuomboleza kutoka kushoto Mr. Tesha, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Mbunge Seleli na Mr. Michael Shirima, Mwenyekiti wa Precionair.

Baadhi ya waombolezaji waliofurika viawanjani hapo.

Baadhi ya viongozi wa Arusha Wazee Sports Club ambayo marehemu alikuwa mwanachama. Kutoka kushoto Mzee Kasori, Mzee Danford Mpumilwa (mwenyekiti) na Mzee Mike Taylor.

Mwenyekiti mwanzilishi wa Arusha Press Club Danford Mpumilwa akiuaga mwili wa marehemu Prof. Hirji ambaye wakati wa uhai wake alikuwa Mlezi mwanzilishi wa Club hiyo kongwe na
ya kwanza ya waandishi wa Habari mikoani. Picha zote na Ripota wa Globu ya Jamii, Arusha





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Patrick TsereMarch 17, 2010

    Mzee Danford Mpumilwa na wazee wenzio wa Club ya Wazee nawapeni pole sana kutokana na msiba wa mzee Hirji. I am sure wengi wetu tutamiss jokes zake ambazo zilikuwa zinatupatia uhai kila jumapili tunapokuwa tunacheza mpira pale General Tyre au siku nyingine tukiwa pale AICC club kijenge tukitia stori. Poleni sana. Hata hivyo mwenzetu katangulia kama wazee wenzetu wengine waliotangulia kama akina Geho na wengineo. Kifo ni sehemu ya mchakato wa maisha. Kifo siyo laana wala balaa. Tumshukuru Mungu wetu aliye hai. Amen

    ReplyDelete
  2. Poleni sana wafiwa!

    ReplyDelete
  3. Poleni wafiwa. May he rest in eternal peace.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...