Chati ya mapato ya mechi hiyo


Shirikisho la kabummbu nchini TFF leo limekubali kwamba limekula hasara kutokana na kuandaa mechi ya Brazil na Taifa Stars ambapo kiasi cha shilingi 1.6bn/- tu kati ya takriban 4bn/ zilizotarajiwa. Katibu Mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela kasema sasa hivi jijini Dar kwamba Shirikisho hilo linajiandaa na mikakati ya kufunika hasara hiyo pamoja na kuweka mambo sawa.
Hakutaka kwenda kwa undani ni shilingi ngapi walikopa na toka wapi lakini kasema Brazil walilipwa pesa yao kwa muda uafaka na kwamba watoa huduma wote walishalipwa na hakuna mwenye kuidai TFF.
Kasema, hata hivyo, mechi hiyo na Brazil ilikuwa na faida kubwa ya muda mrefu, ikiwa ni pamoja ya wachezaji takriban 6 kufuatwa na mawakala wa timu za ulaya kuwataka. Pia amesema utalii utakuwa sana kwani wengi wanaulizia Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 45 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 13, 2010

    Kaka Michuzi,

    It needed no Genious to figure out, the whole episode was rather mondane,

    I am not saying the Idea to bring Brazil to Tanzania was bad one, but rather the executors were pretty much DUMB FOUNDED, CLUELESS, who followed their emotions rather than REAL DEAL, what I mean by that there was no Nitty/Gritty details of any sort from the TFF, when they went ahead with this exprimentation.

    The first clue came when, when I found that the brazil team would come to Tanzania, from Foreign Media.

    This pretty much undermine the internal media attention, which was needeed even before the TFF starting negotiation with Brazil Football Federation, and why I am saying that, it is because the local media would change the mood of the country, in favour of wanting the Brazil team to come to Tanzania, and that would pretty much change the mood of the nation in favour of the match. But it is unfortunate that was not the case, again for same reason the TFF are dumb Founded. Everything, seems to me was done in Secrecy for WHAT, tunaenda vitani na UGANDA???

    Secondly, the TFF did not have numbers when they planned for the tickets, thats why a lot of fans were left out, you would have noticed that the ground was half empty, again for the same reason TFF are DUMB founded, they pretty much didn't have figures and numbers of their Home base FANS trends of spending.

    Labda kwa kuwakumbushia tu,

    1. Moja ya sehemu muhimu katika kutayarisha friendly match ya such a high magnitude like this, walitakiwa at least wanegotiate adverticements na licence rights na warushaji, pamoja na kuipublish kwa local industries, whether that be tourism department or kiwanda cha Soda, sifikiri hilo limefanyika. Utaitangaza vipi Tanzania kama huna cha kuwaonyesha zaidi ya Jina kwenye on Screen Score Board.

    Mimi ningependelea sana, serikali ikatafuta vijana na kupewa training kwenye timu za Ulaya katika sekta ya kabumbu, katika maswala ya kibiashara, TV rights, Sponsorship, negotiation skills, na uandaaji wowote wa michezo ambao patakuwepo na utumikaji na upatikaji wa fedha.

    na siyo kupewa Clean Bill, na kupewa pesa kwenda kutumia tu, kwa sababu ya kufata nyoyo zao.

    Na effects hii, ni katika sekta nyingi sana za kiserikali, na siyo mpira tu, lazima vijana tuvunje strunglehold waliyoiweka na kuvunja unnecessary bureacracy and start modernizing our institutes with policy making and bring in talented young enterpreneur with business and techninological talents, ni kwa manufaa ya nchi na siyo matumbo na VICHWA MAJI.

    Nani on the chopping Block following this ? na wamejifunza nini zaidi ? watueleze na siyo watupe excuse tumeitangazia nchi na maagent wameongea na wachezaji.

    Yaani hii mechi, imenikumbusha mtu akifumaniwa na mtoto wa jirani, hakuna interviews after the match na wachezaji, promos or nothing.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 13, 2010

    Hawa TFF wanachekesha kweli kwanini hawakutafuta wachumi wakafanya project analysis if it was worth investing such amount...Wanajua wapenda soka ni walalahoi...wanaweka viwango vya mawaziri...hawakujifunza match ya Ivory Coast jinsi uwanja ulijaa? niliishia kuangalia pub lol laki mchezo? wakome. Wachezaji wamepata soko na utalii watu wanaulizia atupe facts with data msione watz wote wehu....POOR TFF

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 13, 2010

    Mr Kamau here from Tanzania...as I have said before...Tanzanians put their emotions before the reality... you see..Its all failure...and you will keep on failing unless u select responsible leaders.....big up for Kenyans.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 13, 2010

    Surprise, surprise...

    Kuna dogo aliongea mambo ya msingi hapa. Ishu yote ilikuwa imejaa uchafu na siasa tu bila kuangalia mbele.

    http://vijanafm.blogspot.com/2010/06/watanzania-na-ujio-wa-brazil.html

    ReplyDelete
  5. Bila kuzungumzia kwa nini na vipi wapepata hasara. Au kujadili ni vipi nchi imefaidika/ itafaidika kutokana na Taifa Stars kucheza na Brazil.

    Napenda kuwapongeza TFF kwa kuwa wawazi kwa umma wa Watanzania kwamba walipata hasara. Hili wengi waliliona mara tu ilipofahamika ni kiasi gani cha pesa Brazil walilipwa kuja kucheza na Taifa Stars.

    Matokeo ya jedwali la hesabu hapo juu inaonyesha ni 47% tu ya tiketi ziliuzwa kulinganisha na makadirio yaliyowekwa awali.

    Hapa TFF wamefeli tena "BIG TIME", sasa nawasihi wawe wawazi tena kwa kuja kutufahamisha ndani ya TFF ni hatua gani zitachukuliwa dhidi ya wahusika walio sababisha hasara hii kubwa.

    Soames Phares,
    Reading, UK.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 13, 2010

    Hii inji kweli ni BURE kabisa! Yaani Sirikali ipo tayari kukopa Billions kuwalipa foreigners - Brazil kuja kucheza na kipira cha gozi kwa dakika 90, lakini si kuwawezesha wazawa ama wananchi wake ili waweze kuiendeleza inji yao?

    Je, ni wasomi wangapi wangeendelezwa hapo kupambana na mikataba mibovu? Ni shule ngapi zingejengwa hapo? Ni wodi ngapi zingejengwa hapo kuwasaidia mama wajawazito wajifungue salama? Hiyo hele isingetosha kweli kupiga dawa Tanzania nzima kuua mazalia ya mbu?

    Halafu eti tuichangie CCM? Maaawee!

    Susi na Chuma indeed!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 13, 2010

    Mbona hajaweka mapato kutoka kwenye matangazo na pesa za masponsor? Hii mechi lazima ilikuwa sponsored tuliona mpaka yule rais wa ngo ya kupambana na malaria, kisha leo tunaletewa mapato ya mlangoni. hawa TFF wao kila siku huwa hawapatagi faida hata mechi moja? Walinegotiate nini kuhusu matangazo na tv rights?

    ReplyDelete
  8. INGEKUWA NI HII NCHI NINAYOISHI HUYO RAIS WA TFF NA WENZAKE WANAJIUZULU LAKINI SIO BONGO, TUNAMSHANGILIA NA MATARUMBETA KABISA !!

    ReplyDelete
  9. Obhwatasyo ImpokocholeJune 13, 2010

    Lazima tubadilike tuwe 'strategic'.

    Tulishashauri hapa kuwa tukiweka nguvu zetu zaidi katika michezo ambayo nina uhakika tunaweza bila kuumiza sana vichwa wala kuwekeza pesa nyingi sana kama RIADHA, tutaitangaza Tz kwa ufanisi zaidi na Wanariadha hao watapata faida ya kuboresha maisha yao kwa haraka bila blabla nyingi.

    Huko Manyara, Arusha, Mara n.k tunao akina 'Husain Bolt' kibao Hata michezo mingine ya mtu mmoja mmoja kama Boxing, Kick boxing, kuruka n.k tunaweza kabisa tena kwa gharama nafuu tu.

    Kuna watu huwa wanajiokoa kwa kuogelea wenyewe toka karibu katikati mwa ziwa Tanganyika & Victoria na Nyasa. Kwa nini msijiulize kuwa hivyo ni vipawa ambavyo vikiendelezwa katika 'Swimming Pools' mtu anaweza kuwatisha akina Michael Phelp n.k

    Haiwezekani eti Ethiopia & Kenya iwe tofauti nasi sana katika riadha. Wake up Tanzania!

    ReplyDelete
  10. TFF ina mipango haba kwanini Harare waliweka kiwango kikubwa ni tzs 15000/= lakini kwa kwamtanzania wa kawaida anaweza kulipa elfu 80,000/= na mshahara ndio huo wangeweka kiinglio wastani ili uwanja ujae kwa kiwango ambacho wangpata hela ya kutosha wataalam wa tff kuhusu uchumi wako wapi tz watch out

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 13, 2010

    This was a no brainer.

    Nilishasema ilikuwa ni kupoteza fedha na kama kuna wanaobisha basi zileytwe hesabu, hesabu ndio hizo.

    Watu wengine wakisikia US Blogger kasema basi ni lazima wambishie hata US Blogger nikisema the sky is blue wao watabisha.

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 13, 2010

    Watanzania wenzangu, tusipoamka. Naona Tanzania ikitumbukia shimoni. Mfumo wa siasa usio na vipaumbele. Tuanapenda sifa za kijinga, ie.ukumbi wa bunge mkubwa,mzuri kusini mwa afrika, kiwanja cha mpira kizuri afrika mashariki na kati, majengo ya benki kuu mazuri afrika nzima. Huku watu wanakufa, elimu inaporomoka na wachache wananenepa tu kwa miradi kama hiyo. TUBADILIKE, tuing'oe CCM wenzetu wamefanya hivyo tunaona mabadiliko. Hata waziri mkuu "Pinda" anashangaa, waTZ pamoja na sisi kuharibu bado wanatujagua, waTZ wamelogwa! Tutafute mchawi.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 13, 2010

    Mwenyekiti na Katibu wa TFF lazima wawajibike kujiuzulu. Failure isikubalike

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 13, 2010

    Jamani mbona mnawashambualia TFF kwani nyinyi ni wageni na Tanzania? Hivi ni kitu gani tunaweza sisi kwani? Hivi ni mara ngapi serikali imeshindwa kwenye mambo yake mengi tena more serious how come mmeshitushwa na hili la TFF? Tutaendelea kushindwa mpaka pale tutakapojuwa kupanga na kuchagua.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 13, 2010

    mechi hiyo na Brazil ilikuwa na faida kubwa ya muda mrefu, ikiwa ni pamoja ya wachezaji takriban 6 kufuatwa na mawakala wa timu za ulaya kuwataka

    wow realy? that good news! that will cover our loss then! NOT

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 13, 2010

    Pia amesema utalii utakuwa sana kwani wengi wanaulizia Tanzania

    Huo sio ukweli kamili, kweli wengi wanaulizia tanzania, lakini kwa bei za kila kitu kuwa ghali kuliko majirani zetu, ubovu wa barabara na kutokuwepo na information za kutosha katika mtandao kuhusu tanzania kutazuia wageni kufika huko.

    Tukumbuke kuwa katika ulimwengu huu wa leo kila information ya jambo watu huangalia katika mtandao. mtandao umekuwa na nguvu ya ajabu.

    Suali ambalo tanzania wanashindwa kulieleza ni "why should i come to tanzania?" "why shouldn't i go to south africa or kenya instead?"

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 13, 2010

    kwanini walichelewa kuuza tiketi? wakasubili paka mwisho?.wakuweza kujua tiketi ngapi zimeuza ili wawe na sale kwa viti tupu mwishoni au kuwa na group sale discount!!!!!!. walisema watu kutoka nje walihitaji tiketi, ni mikakati gani walitumia kuuza tiketi nje au walisubili watu wafike bongo?
    msimamzi na meneja mauzo awajibike/ wajiuzuru.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 13, 2010

    Wazo lilikuwa zuri, utekelezaji ulikuwa na matatizo. Ilikuwa mara ya kwanza. Let's learn from the experience and move on. Hatuwezi kuogopa kuwaalika Argentina kucheza na sisi eti kwa vile tulikula hasara kwenye mechi na Brazil. Watu wanalalamikia hasara ya mechi na Brazil kuliko wanavyolalamikia hasara za bandari, reli, ATC nk. Si mtaona kura za watu zitakapoenda kwenye uchaguzi.
    Tukiwa na programu endelevu tukawa na timu imara ya taifa kama Brazil na sisi tutakuwa na uwezo wa kudai donge nono kabla ya kucheza mechi ya kirafiki na mtu. Tukiwa na timu nzuri tutaona picha ya Rais Obama akimpa zawadi ya kinyago mchezaji nyota wetu.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 13, 2010

    "Zimbabwe vs. Brazil match grossed US$ 600 000"
    http://www.thezimbabwean.co.uk/index.php?option=com_content&view=article&id=31589:zimbabwe-vs-brazil-match-grossed-us-600-000&catid=46&Itemid=35

    My comments;
    No research,no right to speak or don't take a risk at al!.We could be learned on Zimbabwe's success!.I think there so many positive things comes on Brazil vs TZ game,but,still we would get those benefits though with great financial outcome of the match.It's so pity we lost the game, and we lost money,but hopeful in a long term strategies,it will pay off eventually.
    Apart from that,Will be great if TFF could announce the interest gain through sponsorships.Being transparency would provide a clear report of the match and people's expectations.

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 13, 2010

    TFF must learn from Zimbabwe Success!.

    I calculated,and see how they made!.

    600,000.00 USD = 871,200,000.00 TSH (8.7 billion Tsh)

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 13, 2010

    Kamau alishatoa maoni yake tukamshambulia sana.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 13, 2010

    mdau wa Sun Jun 13, 03:24:00 PM kwani hujui kama sisi ndio tuliowalipa walioweka matangazo na masponsor? hii yote ni kuitangaza tanzania!

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 13, 2010

    Wewe Anonymous wa Sun Jun 13, 07:47:00 PM.

    Hesabu zako ni sahihi kwenye fihure

    600,000.00 USD = 871,200,000.00

    But,hizo ni 0.87 bilioni(milioni 871.2) na SIO bilioni 871(Unakuwa kama hujasoma darasa la nne).Hizo ni pesa ndogo ukilinganisha na 1.67 billion zilizoingizwa na TFF.Mlaumu kwa facts na sio kwa kudanganya umma.HALAFU kusema Zimbabwe wame success ni UONGO kwa kuwa thamani ya pesa ya Zimbabwe iko chini,TFF walishasema wamepata hasara na maana ya hasara ni kupata pesa chini ya kiwango mlichojipangia.Kama TFF hawadaiwi katika gharama za mechi wameshamlipa kila mtu.Punguzeni kelele watz.MKITAKA Kuleta changes basi mgombee ubunge ili vilio vyenu visikike.
    Ndio maana hatuendelei.Kaletwa kocha mpya mara hoo bomu kuliko Maksimo,hivi akija wenger halafu mkiambiwa kuwa bei za vitu vyote zinaongezwa kwa sh 300 ,ikiwa ni gharama za kumlipa Wenger mtalalamika tu ,hakuna jambo zuri linalofanywa watu Tanzania,kila kitu kibaya.
    Nicholas

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 13, 2010

    kuna mengine zaidi ya haya!!
    kule jumba kuu jeupe la kiranja mkuu wanayajua haya

    God intervene

    ReplyDelete
  25. AnonymousJune 13, 2010

    najuta kua mTZ,kumejaa ufisadi na uozo eti nchi yetu imefaidika kiutalii,eti wachezaji wameuliziwa kwenda kucheza ulaya aibu tupu kiingilio mshahara wa mwalimu au muuguzi hivi kweli waliona bora mpira uangaliwe na watu wawili,sasa ndo uone nchi yetu ilivyo na mafisadi wanafikiri kila mtu mwizi kweli mTZwa kawaida atawezaje kuenjoy na familia yake awalipie elfu 80 80 kila mmoja kuangalia what?Brazil?na huyo aliyeamua hivyo bado yuko madalakani kweli hii ni akili,MI NAONA LAZIMA AJIUZURU AU WAJIUZURU WALIOSABABISHA HAYO YOTE,NAHASIRA NA HIYO NCHI SIJUI KAMA NTARUDI TANZANIA KUNATIA VIDONDA VYA TUMBO UJINGA UJINGA TU WA WATU WAPUUZI WACHACHE.

    ReplyDelete
  26. AnonymousJune 13, 2010

    Kupoteza pesa ni kero moja kutaka kutufanya wajinga kwa kutudanganya ni matuzi makubwa.

    eti mechi hiyo na Brazil ilikuwa na faida kubwa ya muda mrefu, ikiwa ni pamoja ya wachezaji takriban 6 kufuatwa na mawakala wa timu za ulaya kuwataka mnadhani tumezaliwa jana na hatujui masuali ya mpira na hatufuatilii haya?

    Toka lini scouts wa club yeyote ya nje kutaka kumnunua mchezaji kwa kumuona katika mechi moja tu tena ya kirafiki?

    clubs zote zinatuma scouts wake kuwafuatilia wachezaji kwa muda mrefu kuanzia miezi sita na kwenda mbele kabla ya kukiri kuwa wana interest ya mchezaji fulani, leo hii iweje?

    scouts hupeleka ripoti na recomendation zao kwenye klabu zao na huku ndio kunakofanyika analysis ya mchezaji kwa kuangalia video za mechi zake (sio mechi yake).

    Haiwezekani kabisa kuwa timu yeyote ile ya ulaya ianze kumfuata mchezaji yeyote yule baada ya mechi moja ya kirafiki hususan katika msimu wa world cup. Msitudanganye namna hii.

    ReplyDelete
  27. AnonymousJune 13, 2010

    Sun Jun 13, 09:48:00 PM, jawabu ni kuwa anayajua maana alitowa baraka zake juu ya uamuzi wa kuwaalika na kuwalipa wabrazil. Sio siri kiranja ni mpenzi mkubwa wa futiboli na brazil ni moja katika timu anazozihusudu!!!

    ReplyDelete
  28. AnonymousJune 13, 2010

    Nicholas wewe si umesoma darasa la nne so JUST SHUT UP, wacha kuongea utumbo!

    ReplyDelete
  29. Haikuwa vigumu kwa TFF kuja na mchanganuo unaoonyesha "namna hasara ilivyopatikana."Mantiki nyepesi tu inaweza kutueleza kuwa kinachofanyika hapa ni kuhalalisha ufisadi.Na TFF si wajinga kama baadhi ya watu wanavyofikiria.Wana akili,japo sio ya kutengeneza faida kwa manufaa ya taifa bali manufaa yao binafsi.Pia wana akili ya kutambua "uzuri" wa Watanzania: watalalamika siku 1 kisha watasahau.

    Wakati baadhi ya wenzetu walipokuwa wanatetea uamuzi wa TFF kununua mechi hiyo (kwa madai kuwa itasaidia kuitangaza Tanzania,nk) niliamini kuwa aidha wamesahau tatizo la ufisadi (na Watanzania wengi ni wasahaulifu kwenye ufisadi) au wameamua kupuuza ukweli kuwa mradi huo wa kuileta Brazil ni miongoni mwa mambo mengi tu yanayafanyika kwa minajili ya "maslahi kwa taifa" japo madhumuni halisi ni maslahi binafsi.

    Tenga na TFF yake hawana hofu ya kuwajibishwa,sio tu kwa sababu utamaduni wa kuwajibishana bado ni "msamiati mpya kwa Tanzania" bali pia wanajua "aliyewapa wazo hilo la kununua mechi na kufanikisha ununuzi huo" atawakingia kifua kama anavyowakingia kifua mafisadi wengine (rejea maelezo ya Tenga kwa Daily Nation la Kenya kuhusu nani hasa aliyewezesha mechi hiyo).

    ReplyDelete
  30. AnonymousJune 13, 2010

    ManUTD, Chelsea FC, Arsenal, Liverpool FC, Real Madrid, Inter Milan n.k hawategemei viingilio vy a milangoni, ila pamoja na viingilio vya mlangoni wanategemea pia Mapato toka vituo vya TV,Matangazo ya Biashara, Radio, Jezi n.k

    Swali kuu kwa TFF je mbali na viingilio vya mlangoni mlipata kiasi gani toka vyanzo vingine?

    Kulikuwa na uwezekano mkubwa kupata faida ndogo au ku-balance matumizi na mapato kama TFF ingejitaarisha vyema, hivyo msisite kuialika Real Madrid, ManUTD ila lazima mjitaarishe vizuri.

    Ni mategemeo yangu kuona ziara nyingi za timu maarufu kuja Tanzania, ndio inawezekana.
    Mdau
    Bwawa la Maini

    ReplyDelete
  31. AnonymousJune 14, 2010

    Toka lini kazi ya TFF ikawa kukuza utalii? Huu ni upuuzi, na inaonekana ni wezi wasio na mipango yoyote endelevu. Hayo wanayoyasema ya wachezaji kufuatwa na utalii hatuwezi kuyapima, watuambie kisa cha kuweka viingilio vikubwa na watoe hesabu ya sponsors waliotoa fedha zao na tv rights!!

    ReplyDelete
  32. AnonymousJune 14, 2010

    ajiuzulu...uwanja ulikua so empty as if haishi tanzania na hajui vipato vya wananchi. angaweka hela ya kawaida waingie wengi hela irudi.

    ReplyDelete
  33. AnonymousJune 14, 2010

    Masikini walala hoi walikua hawana hela ya kuingia

    Ticket za mafisadi ziliisha za walala hoi simebaki

    ReplyDelete
  34. AnonymousJune 14, 2010

    NENDENI SHULE KWANZA SIYO MNAKURUPUKA TU KUCHANGIA $600,000.00 HUWEZI
    KUPATA TSHS 8.7BN NI MILIONS TU = 871,000,000 HAIFIKI HATA BILIONI MOJA, HUWEZI KUWEKEZA BILLIONI 3 NA KUPATA FAIDA YA BILLIONI 8 ON EARTH. WANGEWEZA KUPATA FAIDA BAADA YA KURUDISHAMADENI YOTE LAKINI ISINGEFIKA
    TSHS 1,000,000,000.00 MAHESABU RAHISI KABISA $600,000.00 X 1500 = TSHS 900,000,000.00 HAIFIKI HATA BILIONI

    ReplyDelete
  35. Mpalang'ombeJune 14, 2010

    TFF wangeweza kuepuka lawama kama tu wangefanya yafuatayo
    1. Kabla ya kuweka viingilio au kuwaita Brasil wangefanya quick survey ya kujua uwezo wa mashabiki wa soka

    2. Wasingesema kuwa anayelalamikia kiingilio kikubwa akae nyumbani- hii ni arrogance ya hali ya juu na kama mimi ngekuwa nina authority ningemfukuza kazi aliyetoa kauli hii.

    3. Kutumia waandishi wa habari kuwa na wasemaji wao kuwa marketing managers, wakati kuna watu wanasomea degree hiyo miaka mitatu kwa assignment na mitihani migumu

    4. Wangeanza kuuza ticket immediately baada ya kusaini mkataba wa ujio na Brasil, hii ingeweza kuwapa picha halisi ya ticket zilizouzwa aiku mbili kabla ya mechi na kuamua kuujaza uwanja kwa ticket za TZS 10,000 siku moja kabla ya mechi kwa kusema kuna mfadhili atalipia TZS 20,000 kila mtu atakayetoa elfu kumi kuingia uwanja, na siku ya mechi wangeshusha mpaka alfu tano kwa style kama ya Tzs10,000. Nina hakika uwanja ungejaa.

    Wangefanya hayo nina uhakika wangepata 70% ya targetted collection au hata ku-break even inategemea na Serikali/Bank iliawapatia kiasi gani cha kuwalipa brasil.

    ReplyDelete
  36. AnonymousJune 14, 2010

    kama ni kweli utalii utanufaika na pia kama wachezaji sita watalamba ulaji, basi hakijaharibika kitu, chukueni asilimia kumi ya mapato yote yaliyotokana na gemu hiyo mpaka mfidie gharama zenu. KAMA NI KWELI LAKINI.....

    ReplyDelete
  37. AnonymousJune 14, 2010

    Ni kweli faida za kuleta Brazil ni nyingi na za muda mrefu ambazo haziwezi kurudishwa kwa kiingilio cha mara moja, kwa wapenzi wa soka itabaki ktk kumbukumbu zetu maisha yote. Mbona kuna mambo mengi yanafanyika hatuulizi faida au hasara? hata hivyo hesabu zinaonesha fedha zilizotarajiwa ni TZS 3B sio 4B kama ilivyoandikwa hapo juu.

    ReplyDelete
  38. ANKAL KAMAUJune 14, 2010

    I TOLD YOU TANZANIANS YOU LIKE TO SHOW OFF WE KENYANS ARE NOT THAT STUPID EVEN RWANDA CAN NOT DO THAT, NOW YOU ARE BLAMING EACH OTHER I WANT TO SEE JOHN MASHAKA AND MATINYI COME UP AND DEFEND THEIR POINT, YOU DON`T NEED EDUCATION TO KNOW THAT WAS SCAME, BUT MOST TANZANIANS WILL DO ANY STUPID THING AS LONG AS YOUR PRESIDENT SAY SO. THEY TOLD YOU THE 200,000 TSHS WERE SOLD OUT THE FIRST DAY YOU FOUND OUT IT WAS A BIG LIE, NOW THEY TELL YOU SO MANY COUNTRIES ARE CALLING TO CHECK WITH SOME PLAYERS FROM YOUR COUNTRY THAT IS A LIE WHO IS GONNA ASK FOR PLAYERS FROM TANZANIA? SHAME ON YOU NEXT TIME ASK US KENYANS BEFORE YOU JUMP INTO THE WAGON WHICH YOU DON`T KNOW WHERE IT IS HEADING!! STUPID....!

    ReplyDelete
  39. AnonymousJune 14, 2010

    mmevuna mlichopanda tff

    ReplyDelete
  40. AnonymousJune 14, 2010

    Big Up Ankal Kamau

    ReplyDelete
  41. AnonymousJune 14, 2010

    Maskini baada ya kuwatukana wafanyakazi sasa kura zinatafutwa za walalahoi wapenda mpira kwa ngarama ya nchi, kweli kichwa cha mwenda wazimu. Mimi hoja yangu ni kwamba yawezekana hizi hela zimo humu kwa ajili ya SSM na hili lilikuwa ni changa la macho tu. Mwenye kiongozi tunaye!!!!! Pumbafu kabisa na ngoja muda wake uishe lazima ajibu tuhuma!!

    ReplyDelete
  42. AnonymousJune 14, 2010

    Dawa ya wabongo ni ankal Kamau, mimi namkubali sana Kamau ukweli ndiyo huo, pesa ambayo ingetosha kusambaza umeme vijijini sasa unaipeleka kwenye soka why??????????kilimo hakuna pembe jeo?? kweli sisi ni malofa, Kamau lete article nyingine, mimi nitakutetea,

    wabongo ni wavivu wa kufikiri, asante kamau
    mdau anayetarajia kukata urai wa bongo kuwa raia wa nchi zenye watu smart kama kamau

    ReplyDelete
  43. AnonymousJune 14, 2010

    hapo tff hamjafanya jambo jema kwa taasisi kumwa kama hiyo kufanya hisabati za kitoto ni hatari mnatuumiza sie wote siku nyingine ndugu zangu tuulize wachumi bASI ili msituumize tena.

    ila hawa ndugu zetu wakenya vipi mbona kujifanya wanajua sanaaaa!!
    washikaji wananikera sana. hawa jamaa wameshazoea wiziwizi ndo wanataka kuuleta bongo ila kila kitu wanajiona wanajua sana!!
    akili zao mavi matupu ya wabongo tuachie wenyewe endeleeni na kina odinga wenu hao.
    huku ughaibuni wamejaa wakenya kibao hawana muelekeo wamekuja kihuni tu ila kazi kututangaza vibaya
    katika you tube nyimbo zote za bongo mmezipiga chapa ya kenya hamoni hata aibu. hadi Juma nature eti ni mkenya
    mmerogwa nyie wavivu tu.
    tuachieni wabongoi tupite
    hey kenyans stop damn on walls sie hatujazoea kujisifusifu kiasi hicho!!

    ReplyDelete
  44. AnonymousJune 14, 2010

    ankal kamau sijakupenda kabisa mjivuni mkubwa wewe.

    jamaa umerogwa wewe mpenda kupiga chabo mbona kenya huongelei ya akina kibaki na raila!! tena shindwa kabisa kutuita sie stupid!!!!!

    kama huna kizuri cha kuchangia kaa kimya sio kazi kusifia kenya watu tunajadili mambo yetu ya msingi ndani ya nchi yetu

    acha ujinga wako unataka tuwaulize kenya mna nini cha kutushauri zaidi ya utapeli!!
    shindwa kabisa ningekuona ningekutemea mate huna akili we jamaa

    ReplyDelete
  45. AnonymousJune 14, 2010

    wewe kamau acha ujinga wako!! ya kenya yapeleke kenya hayatuhusu sie ya tanzania ni ya kwetu una hulka za kibaguzi na kibinafsi na wala hauna lengo la kutusaidia hatukutaki au tafuta lugha nzuri ya kutumia hapa ulingoni kwa ankal!!
    mwenendo wako unataka kuharibu east africa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...