Saloon ya kisasa iliopo maeneo ya ya Tegeta Nyaishozi,ina vifaa vyote vya ndani.
mnunuzi hatalipia kodi ya mwaka mzima.
ina A/C,Heater ya maji ya moto,Steamer,Tv pamoja na Washing Chair,etc.

Atakae nunua anapata vifaa vyote vilivyopoto ndani na nje ya Saloon hii ya kisasa pamoja na kodi ya mwaka mzima bure!!

Wahi Sasa!!!

Bei ni Tsh 15M.


kwa mawasiliano 0655 844 266 au 0784 844 266
inavyoonekana ukiwa kwa nje.
kabati la kuhifadhia vifaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. SALON inauzwa 15m, then kodi ya mwa ka mzima ni free, hiyo kodi ni ya nini na umeshanunua , insurance, tax au.......?

    ReplyDelete
  2. Hii saloon hainunuliwi tu, kama vipi ahuke bei vinginevyo litazidi kumdodea.

    ReplyDelete
  3. e bwana we michuzi na hicho kisaloni chako tumekichoka huyo mwenye saloni hawezi tumia akili toka lini mikasi ya kunyolea ikauzwa milion 15 labda kama anauza na nyumba ya saloni lakini sio mikasi baba co mikasi ni sh100,000/= na hapo kuna mikasi mingapi hayo makochi ya kuchonga kwa akina mangi ni elfu hamsini 50,000 camon man we mwenye saloni hebu kuwa sirious bana

    ReplyDelete
  4. Nahisi muuzaji ana mkopo, tangu lini chumba kimoja tena cha kupangisha ukauze milioni 15????? Michu msahuri auze kitu kimoja akimaliza aelewane bei na mwenye nyumba, milioni 15 unapata kiwanja kilichopimwa boko! yeye ataka kutuuzia chumba, balaaaa, No money

    ReplyDelete
  5. 'Mkuu tukitaka kuona cash flow ya saluni na balance sheet yake imekaa vipi tunaweza kupata.

    Sababu 15M ni high investment mkuu, maana lazima nijue cash flow imekaaje.

    ReplyDelete
  6. Ankal inabidi kujifunza namna ya sales, marketing na promotions hizi ni fani za watu! katika kutoa matangazo kama haya inahitaji maelezo yenye kufutia , sasa tufafanulie vizuri hii saloni japo ni barba shop hakuna salon ya wanaume, kama itakuwa ya wanaume basi watakuwa ni dada poa(au shogas) Je hii saluni inauzwa jina na vifaa vyote ndani pamoja na jengo au. Tunahitaji kujua kama inauzwa jumla, na ni sababu gani zinaleta kwa owner kuamua kuiuza? na kama inashindikana kwanini asikodihe mtu aiendeshe na awe anamlipa kwa mwaka au kwa mwezi. Au hiyo sehemu bomoabomoa inakaribia kupita mtu anataka kuchukua chake mapema?
    Tunahitaji majibu kwako wewe na kwa muuzaji.
    Thanks
    Tunashukuru kwa kuondoa urasimu pia katika kutoa mawazo kwani ilikuwa inaanza kuboa kwani process ilikuwa ndefu!

    ReplyDelete
  7. mie nilienda na kukagua, kisha jamaa akasema milioni 19 ndio bei, kwanza dah iko ndani kiasi, rodi ni kauchochoro, hata wateja wenye mandinga yao kufika na kupaki ni ishu, jamaa apunguze bei tuu tena kwa sana, ingekuwa iko pembezeni mwa rodi na kufuata vipimo vya magufuli vya mabarabara, angeuza kwa bei nzuri, laikini vifaa vilivyoko, ukijumlisha, mhh kabda anauza na nyumba yenyewe.

    ReplyDelete
  8. Mangi wa KiboshoMarch 11, 2011

    Michuzi huyu jamaa anatuchanginyi! Anauza au anapangisha? na kama anapangisha kwa bei hiyo hapati mtu! HIYO NI BIASHARA KICHAA

    ReplyDelete
  9. mwenye salon aache utani, asifikiri 15m ni rahisi kuipata namna hiyo! salon yenyewe viwango duni

    ReplyDelete
  10. Is this a recurrent scam?

    ReplyDelete
  11. hahaaaa,mil 15 nshapata kiwanja wazo na Msingi hadi kozi ya tano!wacha masihara bwana..sehemu yenyewe mvua ikinyesha hapapitiki au unabisha..nakaa nyaishozi na naifahamu hiyo saluni.

    ReplyDelete
  12. Da leo nimecheka sana yani chumba cha kunyelea na mikasi kinauzwa m15.halafu muuzaji anavyo isema hiyo m15 ni kama anasema sh 1000,wacha we saloon ya kisasa inauzwa m15.Achamasihara wewe.
    kueni na seriuce na biasha wa bongo wenzangu.mimi mi15 najenga nyumba safi kabisa.Da wabongo bwana kwa masihara.

    ReplyDelete
  13. kasema elfu 15 sio mil 15..si sawa eheee

    ReplyDelete
  14. Huyu mtu anauza au anakodisha? kama anauza suala ya kodi linatoka wapi? Je anauza kiwanja, chumba pamoja na vitu vilivyopo au anauza vitu vilivyopo?. Kama anauza vifaa vilivyopo then mwaka unaofuata unaendelea kulipa kodi, huyu jamaa anapoteza muda wake. 15M siyo suala la mchezo kihivyo.

    ReplyDelete
  15. Kihalali anatakiwa au ze milioni mbili tu hakuna mjadala kwanza huko ni mbaliii halafu haina mvuto wa kivile kawaida sana, haijakaa kiprofesheno tizama hivyo vichupa vya maji ya uhai sijui vimewekwa sabuni na vyenyewe viko kwenye mahesabu mmmh

    hili tangazo lisije tena humu linatuletea usiku!

    ReplyDelete
  16. Duh milioni 15 sio jamaa labda angesema milioni tano maana saloon hazina gharama hivyo labda pango au mkopo nini jamaa wanamtaiti arudishe hela alizokopa?

    ReplyDelete
  17. Hoya hacha hizo jamaa, je ungekuwa unauza na nyumba je ungesema kiasi gani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...