Ankal akiwa na mtangazaji mwandamizi wa Voice of America Bi. Khadija Riyami aliyeongozana naye White House jijini Washington DC leo tayari kuanza kazi ya kuripoti kutokea Ikulu hiyo ya Marekani, akijaza nafasi iliyoachwa wazi na Mh. Juma Nkamia, ambaye sasa ni Mbunge wa Kondoa.

Ankal ameiambia Globu ya Jamii usiku huu kwamba wadau wake wala wasiwe na hofu kwani libeneke litaendelea kama kawa kwani kaacha timu kubwa ya kuendeleza libeneke na wakati huo huo atakuwa akileta mambo moja kwa moja toka sebuleni kwa Obama. VOA wamekuwa wakimzengea sana Ankal ili akafanye kazi kwenye idhaa hiyo ya Kiswahili upande wa habari za mtandaoni.

Ankal akielezea mambo ya libeneke kwenye ukumbi wa mkutano wa White House baada ya waandishi wa White House na wa nchi mbalimbali kumuomba aelezee jinsi tasnia ya habari ilivyo Bongo kwa hivi sasa, hususan swala la kuibuka kwa 'vikombe' karibu kila kona ya nchi. Ankal aliwaambia kwamba ni kweli kumezuka watoa dozi sehemu kadhaa lakini hadi sasa Babu wa Loliondo ndiye anayetamba kuliko wengineo wote. Ankal alipata wakati mgumu sana kuelezea ni namna gani kikombe kimeshika hatamu Bongo.
Ankal akivinjari kwenye viunga vya White House
jijini Washington DC baada ya kutoa mada ya vikombe

Ankal akiwa ofisi za masuala ya nje ya Marekani (State Department) ambako ndiko ziliko ofisi za Bi. Hilarly Clinton. Kazi yake ya kuripoti habari za Ikulu ya Marekani huhusika na ofisi hii pia. Ameiambia Globu ya Jamii kwamba anamshukuru Mungu kwa 'kudakwa' na VOA na hivi sasa anajiandaa kupigana vikumbo na wanahabari wa dunia. Kasema ana uhakika kwamba endapo kama mambo hayatokua mswano ataingia mtaani kubeba boxi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 310 mpaka sasa

  1. April 1st == fools' day !!

    ReplyDelete
  2. michu sikuwezi....kila mwaka kwenye fools day lazima ulete kitu kipya..sawa bwana ha hah a ha ha aha aha

    ReplyDelete
  3. HII IMEKAA KI APRIL FOOLS DAY ZAIDI...!!! poleni woote mliouvaa mkengezz
    mdau canada

    ReplyDelete
  4. Hongera sana uncle yetu, Mungu azidi kukufungulia, ukipata wewe na sie tumepata! tumefurahia sana mafanikia yako!!
    NANA

    ReplyDelete
  5. Kila la kheir, umeweza ngazi ya moja utaiweza na nyengine - Amin.
    Unatuwakilisha kwa hivo tutafata nyayo zako.

    Anko ulikwenda kwa Loliondooooo nini?
    Asante

    ReplyDelete
  6. Hongera kwa kuwapata watu na APRIL FOOL HII!!!... :D hahahaha

    ReplyDelete
  7. KELAND SCHOOLApril 01, 2011

    Wadau leo ni sikukuu ya wajinga isije ikawa Ankal anatudanganya??????

    ReplyDelete
  8. Happy April Fools Day Uncle Michuzi.

    ReplyDelete
  9. ...April Fools day. Dah, umewapata wengi sana leo

    ReplyDelete
  10. Sikujua kuwa Ankal ni mwandishi wa habari wa ku report. Nilikuwa naelewa kuwa yeye ni photo journalist, mwanahabari zaidi katika picha. Hongera zako Mkuu, tutakuwa tunapishana kwenye corridor za White House maana wengine huko ndipo kibarua chetu cha u Jack Bauer. Mwezi Machi naona umepita haraka sana, kumbe leo ni tarehe 1 April?

    ReplyDelete
  11. TAARIFA MUHIMU KWA WADAU WA LONDON na UK - KUANZIA LEO JIONI (SAA 12 JIONI) PASTOR KIJIKO WA SEVEN SISTERS ALIYETUNUKIWA NA ROHO SAFI KUFANYA SHUGHULI YA KUTOA TIBA, ATAANZA KUGAWA KIKOMBE (£0.50p only)KWA WATU WENYE MATATIZO NA MARADHI MBALI MBALI. TAFADHALI WASILIANA NAYE: BONGO BAR, 65-67 BROAD LANE, LONDON N15 4DJ.

    HUU NI UWEZO WA MWENYEZI MUNGU TUU.

    ReplyDelete
  12. Siku ya wajinga nadhani umeshawatia changa la macho wajinga big up.

    ReplyDelete
  13. Happy Fool's Day kaka.

    ReplyDelete
  14. wap michuzi haya mambo ya cku ya wajinga cyo,,,we mkal kaka,,,kwan nkamia kashaacha kaz mda mrefu mpaka leo wamekuchukua wewe????????kwel kaka we noma umewashika wajinga

    ReplyDelete
  15. hongera kk mungu akupe wepesi

    ReplyDelete
  16. April fool nyinyi

    pambaf

    ReplyDelete
  17. THE END JUSTIFIES THE MEANS...ANKAL....HONGERA SANA BROH...!!
    jeffmsando@yahoo.com

    ReplyDelete
  18. Ongera kaka

    ReplyDelete
  19. Mimi hujanipata, happy April fools day!

    ReplyDelete
  20. Ya mwaka huu kali lakini naona wengi wameamini!

    ReplyDelete
  21. Hii imekaa kama vile story ya April 1, ujue sisi ni watu wazima kuanza kutuimbisha nyimbo za fools day, ohoooooo!!!

    ReplyDelete
  22. Ha ha ha, hamna kitu mIchuzi, unatuzingua! APRIL FOOLS!

    ReplyDelete
  23. Leo sio siku ya wajinga kweli?nadhani anatania hapa

    ReplyDelete
  24. Is it april fool day or not, any way congraturation

    ReplyDelete
  25. Anko umewapata wajinga kibao
    lol, ckukuu njema

    ReplyDelete
  26. april fools day

    ReplyDelete
  27. i reserve my comment mpaka siku ya wajinga iishe!

    ReplyDelete
  28. April fools day umewakamata

    ReplyDelete
  29. hongera mzee Michux
    mwambie Obama uje nae kwetu aje kutuletea angalau maendeleo

    ila nafikiri hii umeitoa bcz of foolday mmh

    ReplyDelete
  30. kweli au april fools day!!!!

    ReplyDelete
  31. Hii ni kwel ankal au ndio ya mambo ya leo tarehe 1 aprili

    ReplyDelete
  32. Mama Clarencea - TabataApril 01, 2011

    Michuzi!!! Leo ni siku ya wajinga

    ReplyDelete
  33. Ankal, leo siku ya wajinga...humpati mtu!

    ReplyDelete
  34. hv leo si ni cku ya wajinga au????????

    ReplyDelete
  35. Hongera Ankali ila naona utawapat wengi april fools day. ila mie nakuombea one day yes upate nafasi kama hiyo

    ReplyDelete
  36. April fool!

    ReplyDelete
  37. Fools Day!

    ReplyDelete
  38. Happy April Fool Day!

    ReplyDelete
  39. any other day i would believe it, but on april fools day...i don't believe it... let us wait and see

    ReplyDelete
  40. leo si siku ya wajinga jamani......

    ReplyDelete
  41. Ankal, kama huu si utani wa April Fools' Day, [maana naona hiyo posting ni ya 1 April], basi nami naungana na wadau wengine hapa juu kukupa pongezi zangu za dhati na kumuomba Muumba wetu awape wewe na wanafamilia wako kila la heri. J. Mwaipopo.

    ReplyDelete
  42. HAHAHAA...Bro Ankal MIE NAKUPA HONGERA YA KUWEZA KUWASHIKA WENGI,
    Naona hata wewe ukianzisha kikombe utapata mamluki,
    Kweli cku ya wajinga!!!

    ReplyDelete
  43. April fools day. Umewapata uncle.

    ReplyDelete
  44. Hongera bro. Tunakutakia mema zaidi. Hata hivyo natumai kuwa utaendeleza libeneke na tutaendelea kupata blogspot yetu ya jamii ambayo ndiyo blogspot namaba moja ya kitanzania kila siku. Be blessed.

    ReplyDelete
  45. April Fools day kweli umewapata wengi uncle michuuz

    ReplyDelete
  46. Hongera sana mkuu, ila japo naona hizo pcha lakini habari hii umeitoa siku ya "wajinga" sasa kidogo inautata, hebu kesho tuwekee mkazo ili tukupongeze vizuri.

    ReplyDelete
  47. Picha ya pili inaonekana kama alishawahi kuitoa siku za nyuma jamani. Thikukuu ya wajinga,… thidanganyiki!

    ReplyDelete
  48. i hope its not April fool!!!

    ReplyDelete
  49. Ankal naona umewapata sana watu leo...ha ha ha ha....Najua tutakutana soon pale Break Point. Happy fools day

    ReplyDelete
  50. Ha, ha, ha, LEO NI SIKU YA WAJINGA DUNIANI!

    ReplyDelete
  51. umewapata wengi, siku ya wajinga duniani!!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  52. KAKA LKN HAYA SIO MAMBO YA APRIL FOOL?!MAANA HIZI PICHA NAONA KM ZILE ZA KIPINDI KILE UMEANDAMANA MHE RAIS!

    ReplyDelete
  53. Wajinga ndio waliwao...(April Fool's Day)...

    ReplyDelete
  54. mmmhhh Ankal?
    hii sio fools' day special kwa wadau???

    kama sio, hongera!Mungu akuzidishie!

    ReplyDelete
  55. AHHHHH......WAIT A MINUTE????

    Kwani leo siku gani???? Michuzi aache Bongo, now way. Kwenda zako, mi sihamini leo Aprili moja bwana..this sounds waaay good to be true

    ReplyDelete
  56. AHAHHAHAH APRIL FOOLSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS
    HE GOT YOUUUUUUUUUUUUU!!

    ReplyDelete
  57. ila leo ni siku ya wajinga kumbukeni jamani

    ReplyDelete
  58. Yaani nyote nyie hapo juu mmeingizwa mjini na ankal? leo ni siku ya wajinga, na nyinyi ni wajinga waliwao. taarifa za kuaminika, ankal yupo loliondo kwa babu kaweka hema akisubiri zamu ya kikombe, na sio marekani..wabngo bwana, maneno tu..ina maana angesema leo anatoa kikombe uwanja wa taifa, basi nyie mgeeenda..april 1st, siku ya wajinga na vihiyo..
    hngera ankala kwa kuivuta hii vilivyo..

    ReplyDelete
  59. Ya kweli au sikuku ya ... Maana leo tarehe 01-04

    ReplyDelete
  60. April fooooooooooooooooooooooooooool people

    ReplyDelete
  61. Hongera on the APRIL FOOLS..............ahahhaaaaa

    ReplyDelete
  62. April fools dayyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyyy.Hizi ni picha za zamani wakati Jk alipokuja USA.

    ReplyDelete
  63. Hongera sana Muhidi! Hakika unastahili kufika ulipofika! Hakika!

    ReplyDelete
  64. Ha ha ha ha ha...kaka leo kweli umetupata...HAPPY FOOLS DAY!

    ReplyDelete
  65. mmmhh nina mashaka siku ya wajinga leo hahahhahahahahaa
    uncle kawapata

    ReplyDelete
  66. Leo siku ya wajinga duniani ankal tunaye bongo hapa haendi popote poleni mliokuwa mnamsubiria kwa hamu ughaibuni

    ReplyDelete
  67. Asalaam aleikum, Ankal napenda kuchukua fursa hii kukupa pongezi zangu za dhati kwa kufanikiwa kufika huko maana najua ni kwa juhudi binafsi na kudra za mwenyezi Mungu. Napenda kuungana na wadau wengine kukutakia mafanikio mema zaidi na zaidi, Kwani hata mimi katika nyanja za blog nimekuwa nikipata mwelekeo toka kwako, waweza itembelea Blog yangu ya www.mtandaowawatanzania.blogspot.com.

    ahsante!

    ReplyDelete
  68. kweli uncle umewapata weeengi kwenye sikukuu ya leo ya wajinga.....wamekupa hongera ni wenngi.

    ReplyDelete
  69. hongera kwa kuwaingiza wachache mjini!!!

    APRIL FOOOOOOOOOOOOOOOL!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    CU nxt yr 01.April

    ReplyDelete
  70. Hongera sana. Tunakuomba tu ukifika huko usije ukaanza nawewe kutuandikia vingerza hapa kwenye blog yako kama akina mashaka. Vingerza vyenyewe ni vya kuunganisha na selotepu/gundi.

    lingine tusije tukakusikia baada ya miaka 2 eti ooh nataka nigombee ubunge. Tutaacha kusoma hii blog yako kwani tunajua ww ni kijani na njano, rangi ambazo zimeshachuja. tunahitaji jezzy zingine nazo kwenye ulingo wa siasa tuone zinakuja na lipi.

    ReplyDelete
  71. ankal acha uongo!hata mimi nilitaka kupatikana ila umenikosa

    ReplyDelete
  72. siku wajinga leo

    ReplyDelete
  73. Hongera kaka, sasa umetumbukia kubeba box.lol

    ReplyDelete
  74. Hongera sana ankal Mungu akutangulie katika kazi hiyo, na akupe afya njema. Kikombe ulipataaa????

    ReplyDelete
  75. Anksl isije ikawa April Fools Day ...

    Otherwise nikupe hongera sana naamini katika juhudi na maarifa. Na hivi ndio vimekufikisha hapo ulipo.

    Ila kama ni April Fools Day utawapata wengi ..

    Dommy

    ReplyDelete
  76. Hongera sana ankal lakini kumbuka white house dressing code si ze fulana lol
    all ze best

    ReplyDelete
  77. kaka nimekukamata siku ya wajinga leo..hahahahahahahaha.hizi picha zako za kitambo ulivyoenda..poleni wajinga

    ReplyDelete
  78. uncle i hope hujatufanya fools leo, but kama kweli hongera sana

    ReplyDelete
  79. Wote mliotoa comments kalakabahu. Hivi hamjamgundua leo ni siku ya wajinga, Ankal kawachakachueni eti na nyie mmechakachuka. Kweli MJINI SHULE. Popleni na hongera ankal kwaa kuwapata wajinga wengi kiasi hicho... lol

    ReplyDelete
  80. APRIL MOSI 2011

    ReplyDelete
  81. HONGERA KAKA MICHUZI TUNAKUTAKIA KILA KHERY KATIKA KAZI NA DHAMANA MPYA ULIYO TUNUKIWA NASI TUNAOMBA USILIACHE JAMVI LETU NYUMA ....BIG UP...........MDAU...DOHA

    ReplyDelete
  82. Tarehe 1 leo mwezi wa nne, ni sikikuu ya wajinga. Hongera kwa kuwakamata wengi.

    ReplyDelete
  83. April Fools dayyyyyyyyyyyy got a lot of people. Ukiangalia hizi picha vizuri utagundua zina zaidi ya mwaka. Michuzi hapa anaonekana kijana tofauti na post moja ya mwanzoni mwa wiki hii ambayo inayonyesha ana mvi kichwani

    Mbigiri

    ReplyDelete
  84. leo ni april fool, usiwe unatudanganya ankal, hahaha

    ReplyDelete
  85. Hongera kwa bonge la April fool

    ReplyDelete
  86. Ephata SozigwaApril 01, 2011

    Haya yasije kuwa , mambo ya april fools lakini. Nasubiria kesho nitoe pongezi.

    ReplyDelete
  87. april fool dude

    ReplyDelete
  88. Hongera mkuu!but naona km fix vile coz leo ni siku ya wajinga!!
    frm manto.

    ReplyDelete
  89. Happy fools day!

    ReplyDelete
  90. april fools day!

    ReplyDelete
  91. Sio mambo ya tarehe 1 April kweli! Manake habari yenyewe imetoka siku ambayo sio!

    ReplyDelete
  92. kaka mbona maoni mengine una minyia?

    ReplyDelete
  93. 1st of april

    ReplyDelete
  94. BIG UP ANKAL!!

    ReplyDelete
  95. Ankal hiyo ni kweli au mambo ya siku ya wajinga...Binafsi naomba iwe kweli ule bata huko ughaibuni.Inshallah

    ReplyDelete
  96. HA-HA-HA-HA HAPPY FOOL!....Mdau USA!~

    ReplyDelete
  97. APRIL FOOLS! Hizi picha nakumbuka kama kipindi kile ulivyoeenda na JK Nyumba Nyeupe( White House)

    ReplyDelete
  98. sikukuu ya wajinga. Naona umewapata wengi kweli

    ReplyDelete
  99. Hah hah Hah! leo uko unaripoti VOA! kesho tarehe 02 April unarudi kupambana na joto na foleni za Dar Es Salaam.

    Kesho tutakuna Rose garden kama kawaida na kuporojoa kungojea jam ipungue kabla ya kurejea makwetu.

    Libeneke kuendelea kutokea Dar na siyo Washington DC. Fools Day I guess.

    ReplyDelete
  100. kaka mbona haieleweki eleweki au imekaa ki 1st april? mwandishi mpiga picha, wanabadilishana na mtangazaji?

    ReplyDelete
  101. UNCLER MICHUZI. KAMA LEO NI SIKU YA WAJINGA VILEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE

    IRENE MZIGURA

    ReplyDelete
  102. Jamani leo ni 1st of April, naona amewapata haswa

    ReplyDelete
  103. Utani Mwingine bana...

    ReplyDelete
  104. NAOMBA ANKOO UJIITEE ANKOO WA MANKOO

    ReplyDelete
  105. Michuzi tunaomab uthibitishe kauli yako usiku huu.

    ReplyDelete
  106. Shabashii! Wapiiiii!!!!!! hiyo nafasi ameipata saa ngapi! Huyo ni Ndanda boy ktk siku ya Foooooooooooooooools!!!! Day.

    ReplyDelete
  107. mzee wa pajazzzzz na titizzzzzz nikumbukwe pia ankal!

    ReplyDelete
  108. ankal hongera lakini mbona umevaa suti tatu kwa siku moja au na wewe ushakuwa super star?
    sawa mimi nakwambia karibu nyumbani

    ReplyDelete
  109. NASHUKURU WADAU WOTE MLIOTOA NA MSIOTOA MAONI. UKWELI NI KWAMBA ANKAL ALITANGAZA HIVYO KAMA KUENDELEZA LIBENEKE LA APRIL FOOL'S DAY. HIVYO HABARI HIYO SI YA KWELI BALI NI YA KUFURAHISHA BARAZA TU. ASANTENI KWA KUENDELEA KUNISAPOTI KATIKA LIBENEKE NAMI NAWAAHIDI WEMBE NI ULE ULE, HAKUNA KULALA

    ReplyDelete
  110. April Fool - Hukmu Ya Kushiriki Kuongopa Kwa Mzaha
    Nasiha Za Minasaba Mbalimbali
    Kufanya utani wa kusema uongo siku ya tarehe 1 Aprili limekuwa ni jambo la kawaida kwa baadhi ya Waislamu, jambo ambalo limeharamishwa katika Shari’ah ya Kiislamu

    عن ابن عمر رضي الله عنهما قال : قال صلى الله عليه وسلم: ((إني لأمزح ولا أقول إلا حقّا)) رواه الطبراني في المعجم الكبير - " وصححه الشيخ الألباني

    Kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhiya Allaahu ‘anhuma) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika mimi sifanyi mzaha wala sisemi ila tu yaliyo ya kweli)) [At-Twabaraaniy katika Al-Mu’ujam Al-Kabiyr na ni Swahiyh kwa mujibu wa Shaykh Al-Albaaniy]

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...