Waziri Mkuu wa zamani,Edward Lowassa(Kushot0)akimkabidhi Bahasha yenye Tsh. milioni 13, Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu,Issa Shaaban bin Simba,kwa ajili ya kusaidia shule ya sekondari la Edward Lowassa iliyopo Kigamboni,Dar es Salaam.Kwa mujibu wa Mufti ambaye ni mlezi wa shule hiyo, Shule hiyo inatarajiwa kufunguliwa rasmi mwakani kwa kuanzia na wanafunzi 200 wa kidato cha kwanza, na kwamba fedha hizo zitatumika kukamilisha baadhi ya mambo ya shule hiyo ikiwemo kujenga bweni la watoto 30, choo cha shule, kisima cha maji na shule itajihusisha zaidi kusomesha yatima na watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Kulia ni aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Alfred Tibaigana ambaye pia ni mlezi wa shule hiyo.
Edward Lowassa(kulia)akimsindikiza Mufti wakati akiondoka baada ya hafla ya kumkabidhi fedha hizo,iliyofanyika Ofisini kwake,Mikocheni, Dar es Salaam. 
Wakiagana  baada ya shughuli hiyo.Picha na Mdau Bashir Nkromo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2011

    harooo hiro rimjamaa ringine katikati ya rishekhe na rirowasa sirifahamu muraaaa hebu ritamburishee nadhani ni rimtu maarufu muraa

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 13, 2011

    Go Lowassa!! Our next President!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 13, 2011

    This is nice watanzania mna ushirikiano sawa Mbarikiwe!Allah akuzidisheni!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 14, 2011

    Rais wa ukweli 2015, wabaya wako watakufa kwa kiwewe very soon. A very visionary leader, we need you!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...