Mwakilishi wa Emmanuel Televisheni  na Kanisa la The Synagogue Church  Of All Nations Bi. Martha Harvey akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete jumla ya shilingi milioni ishirini na tano 25,000,000/- kwaajili ya wahanga wa ajali ya Meli ya MV Spice Islander  iliyozama katika mkondo wa Nungwi huko Unguja na kusababisha vifo vya watu wengi hivi karibuni. Mchango huo uliokabidhiwa leo ikulu jijini Dar es Salaam umetolewa na Kiongozi wa Kanisa hilo Nabii Themitope Balogun Joshua ambaye anaishi katika MAKao makuu ya Kanisa hilo jijini Lagos Nigeria.
 Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. NAOMBA KUULIZA SI KWA UBAYA , MBONA WATHAMINI WENGINE NILINA WALIKUWA WANATO AMCHANGO WAO KWA YULE KIONGOZI WA ZENCHI INAKUWAJE HAWA WANATO DIRECT KWA RAISI WA BARA ? NAOMBENI JIBU JAMANI.
    MDAU PARIS

    ReplyDelete
  2. Wewe muuliza swali wa kwanza hapo juu. Yaani pamoja na kuishi Paris Ufaransa bado hufahamu kuwa Rais Kikwete ndiye kiongozi wa Tanzania yaana Bara na Visiwani? Ukimpatia Rais kikwete pesa itafika kwa wahusika.

    Mchungaji Dar es salaam

    ReplyDelete
  3. Nimependa staili ya hilo kanisa katika jinsi utunzaji wa pesa, badala kushika minoti kama makaratasi ya kufungia maandazi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...