Bwana na Bibi Kanza.
Wapendwa wetu, ilikuwa siku, wiki,
mwezi na hatimaye tarehe 01/05/2013 mmetimiza miaka minne (4) toka mtutoke kwa
ajali ya gari katika hii dunia. Tunafarijika kwa sababu tuna Imani mpo pamoja
nasi Kiroho siku zote.
Hakuna siku ipitayo kwetu bila kuwakumbuka kwa UPENDO,
UKARIMU, USHAURI MWEMA, MSIMAMO BORA NA BUSARA ZENU. Hakika BUSARA ZENU
zimekuwa dira na nuru katika maisha yetu. Tunaendelea kuwaombea na tutaendeleza yale yote mema mliyotuachia.
Daima mnakumbukwa na watoto wenu, Bright Kanza na
Alvin Kanza, Mr & Mrs T. Kweka, Mr & Mrs G. Kanza, wadogo zenu wote,
wajomba, shangazi, ndugu, jamaa na marafiki. Daima tutawakumbuka Milele.
Sisi tuliwapenda sana, lakini Mungu Baba wa
Mbinguni aliwapenda nyinyi zaidi. Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana
Lihimidiwe. Amen!!
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...