Kwa mara ya kwanza Watanzania watakuwa na fursa ya kupata mafunzo ya kompyuta katika ngazi ya kimataifa, International Computer Driving Licence (ICDL) certification, yatakayoendeshwa na Kituo cha Kompyuta cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UCC) kwa kushirikiana na Chuo cha Mafunzo na Ufafiti cha MK Centre kilichopo Dar es Salaam kuanzia Mei 6.
ICDL inatambuliwa kimataifa kama sifa ya juu kabisa ya mafunzo ya kompyuta ambayo humuwezesha mhitimu kuthaminiwa katika sehemu yake ya kazi kama mtaalamu mwenye ujuzi na ufanisi unaokidhi viwango muhimu vya matumizi ya kompyuta.
Iwapo kuna anayegependa kupata mafunzo haya ya muda mfupi apige simu zifuatazo kujiandikisha kwani nafasi zilizobaki ni chache: 071770960, 0753369018, 0757222880, 07148554572 au 0754053921. wa maelezo zaidi nenda MK Centre Mbezi Malamba Mawili au andika kwa
Barua pepe: info@mkcentre.org
Fomu zinapatikana chuoni na kwenye tovuti:
www.mkcentre.org
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...