Kama umefikia Mkoani Ruvuma hususani wilaya ya Songea Vijijini,basi ni lazima utakuwa umepita  katika Kijiji cha Peramiho ambapo kuna Kanisa hili kubwa la lenye historia ya kipekee.Hili ni Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Benedict Abbey lililopo ndani ya Kijiji cha Peramiho mkoani Ruvuma. Lilijengwa zaidi ya miaka 100 iliyopita lakini ukiliangalia leo ni kama vile limejengwa jana.
Sehemu ya Kumbukumbu ya Mtakatifu Benedict mbele ya Majengo ya kanisa hilo
Sehemu ya Majengo ya Kanisa hilo ambapo pia kuna Hospitali kubwa.
Kiukweli eneo hili la Petamiho linapendeza sana na kuvutia.
Haya ni sehemu ya Makaburi ya watakatifu wa Kanisa hilo la Peramiho waliofariki miama mingi iliyopita,ambapo Baadhi ya waumini wa Kanisa hilo huwa wanafika na kuzuru makaburi hayo.
Jengo la Benki na ilipo Maktaba ya Vitabu
Sehemu ya Majengo yalipo makazi ya Mapadri na Madaktari.
 Barabara ya Kuelekea Seminari Kuu,Peramiho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 15, 2013

    Kanisa KATORIKI ni jipya duniani? Mimi najua kanisa KATOLIKI

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 15, 2013

    Asante mdau kwa kutuweka tukio hili limenikumbusha mbali, mimi nilisoma Shule ya Sekondari ya wasichana ya Peramiho ambayo ilikuwa chini ya wabenedictine na baadhi ya walimu wetu walikuwa Masista. na hilo kanisa ndo tulikuwa tunasali na ilikuwa sehemu ya outing, hahahahahah

    ReplyDelete
  3. We Misupu usipotoshe bana.
    Wakatoliki hawaiti USHARIKA bali wao wanaita PAROKIA ya....

    Usipotoshe bana, kama hujui uliza bana uelekezwe bana!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 15, 2013

    Dah! hayo majengo ni legacy a mkoloni,mkoloni asingekaa hapo pasingekua hivyo. Siku hizi tuna wakoloni weusi..ni nomaa wanaiba bila kujua kesho itakua vipi.Kidumu chama cha Mapindizi!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. green guardJuly 16, 2013

      kidumu...!!!.na udumu ukoloni mweusi

      Delete
  5. AnonymousJuly 16, 2013

    Duu hii imenikubusha mbali miaka ile ya 91 na 92 ambapo vijana wa songea boys waliwatosa ndugu zao tamsala Ila mimi nakumbuka jinsi sosage za ukweli za hapa zilipokuwa zinatengenezwa na mabruda na tofali za kuchoma ni kiboko tuwe tunaweka mara kwa mara vitu vyetu vizuri kwenye display sio tu issue mbaya na mataifa yaliyoendelea ni wajanja katika kuweka vivutio vyao na kuvitangaza zaidi na kuficha mabaya tuige mfano huo

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 16, 2013

    Angejenga mjenzi wa leo angechakachua na kuripua kazi, tujifunze kutenda veme wajibu tunaopewa, itawezekana wabongo???. Siyo kila kitu kizuri afanye mzungu tu.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 16, 2013

    Thank you soooo much misupu nimefurahi kuona Peramiho tena baada ya siku mingi, mtoto wangu wa pili alizaliwa hapo 1990! Natumaini Mheshimiwa Jenister Mhagama Mbunge atafurahi pia.

    ReplyDelete
  8. Mdau wa maguJuly 16, 2013

    Bro Michuzi,
    Umenifurahisha uliponiambia makaburi ya watakatifu. Mtakatifu nani kazikwa hapo kwa mfano niambie? Hamna mtakatifu kazikwa hayo makaburi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 16, 2013

    Ni mazuri na ni ukumbusho wa kitamaduni ila pia tuone jinsi yalivyo imara hadi leo. Tuombe tu mola wasiyachome moto!!!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 16, 2013

    Asante kaka Michuzi yaani leo umenikumbusha mbaliiii saana nilisoma Peramiho girls siku hizo palikuwa panaitwa (Vatican City) yaani tulipikwa ki maadili na kimasomo mpaka leo popote niendapo sina shida ya kuishi na jamii. Namkumbuka sister Martina,Fidelis, Goretha Edisa,Kesha, Mr and Mrs Zenda, Mr and Mrs Jacobo, Mr. msuya n.k God bless you all

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 16, 2013

    imeingia kwenye ramani hiyo

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 16, 2013

    Yuko Mtakatifu mmoja anayetarajiwa kutangazwa anaitwa sister Bernadetha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...