Umoja wa Watanzania ujerumani(UTU) kwa kasi kubwa inaiwakilisha vema Tanzania huko Ughaibuni,kwa kutumia nafasi zote wanazopewa nchi Ujerumani,
ni juzi kati tu Umoja huo ulishiriki katika maonyesho ya "Brüderschaft der völker " mjini Aschaffenburg, ambapo wageni wengi walivutiwa sana na shughuli za Umoja huo za kuitangaza Tanzania, Umoja wa watanzania ujerumani (UTU) unatilia mkazo sana katika kuwashawishi wadau wa
kimataifa wawekeze katika udumua za jamii kama vile Elimu,Afya n.k
Umoja huo umepokea mialiko ya kushiriki maonyesho mengine yakiwemo makubwa kama International African Festival Tubingen 2013 yatakayo anza 8 hadi 11.08.2013
usikose kuwasiliana nao at kamati.utu@googlemail.com
baadhi ya watanzania na marafiki zao ujerumani.
wadau wa UTU wakiwa katika moja ya maonyesho ya Aschaffenburg.
Mdau
baadhi ya bidhaa katika banda la UTU.
mwenyekiti Mfundo, tunaomba picha zinazoonekana vzuri. Mbona mlipiga picha nyingi nzuri tu zilizokuwa zinaonekana vizuri
ReplyDeletemwingine ana bendera ya Kenya! Anawakilisha Kenya nadhani.
ReplyDeleteMimi nimeona mwenye Bendera ya Uganda.
ReplyDeleteSasa sielewi maana watu wakiwa Majuu Wana Afrika ya Mashariki nchi zote 5 Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda HATA ZINGINEZO kama Congo DRC,Malawi, Zambia,Msumbiji,Ethiopia na Somalia ili mradi wanaongea ama wanaelewa kiasi kidogo Lugha ya Kiswahili hujisikia kama ni Sehemu ya Tanzania!
Licha ya hilo, hawa ndugu zetu baadhi yao wa nchi hizo wamekuwa mstari wa mbele kushirikiana na Watanzania kama ndugu sehemu mbali mbali Duniani.
Mungu Ibariki Afrika , Mungu Ibariki Tanzania!
Lakini Rwanda MMMMMMMMMMMMMMM!
ReplyDeleteAliyevaa fylana ya Uganda ni kuwa Rangi za Bendera ya Ujerumani na za Bendera ya Uganda ni sawasawa.
ReplyDeleteRangi NYEKUNDU, NJANO NA NYEUSI.
Hivyo kwa kuwa Uganda ni sehemu ya Afrika ya Mashariki Mdau ameona atumie Bendera hiyo ili kuweka u-Pamoja na Wajeruani ili wajisikie wamoja ktk shughuli!