codes;
Katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Martin Shigela akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Ndugu Mboni Muhita kabla ya kuanza kwa kikao cha wajumbe wa baraza la Umoja wa Vijana katika Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
Wajumbe wa Baraza la Vijana wakicheza ngoma ya Boso yenye asili ya Kusini Pemba, kabla ya kuanza kikao cha Baraza Kuu la Vijana.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Balozi Seif Idd akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar ambapo Makamu wa Pili wa Rais ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi.
Viongozi Wakuu wa CCM wakiomba Dua mbele ya kaburi la Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Sheikh Abeid Aman Karume kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Vijana la CCM Taifa.
January Makamba akizungumza na Wajumbe wa Baraza laVijana wa CCM kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dk.Emmanuel Nchimbi akitoa salaam kwa wajumbe wa Baraza kuu la Vijana Taifa kabla kuanza kwa kikao cha Baraza Kuu la Vijana wa CCM
Mjumbe wa Kamati Kuu Mohamed Seif Khatibu akiwasalimu wajumbe wa Kikao Cha Baraza Kuu la Vijana la Taifa kwenye ukumbi wa mikutano CCM Zanzibar.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Sadifa Juma Hamisi akisoma risala kabla ya kumkaribisha Balozi Seif Idd kufungua kikao cha Baraza la Umoja wa Vijana.

Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Idd akitoa hotuba ya kufungua kikao cha Baraza Kuu la CCM Vijana leo 1/9/2013 katika ukumbi wa mkutano wa Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndugu Sixtus Mapunda akizungumza kwa mara ya kwanza na wajumbe wa Baraza la Vijana wa CCM .
Meza Kuu ikiwa na Katibu Mkuu mpya aliyechaguliwa Sixtus Mapunda wakati wa kikao cha Baraza la Vijana kilichofanyika Zanzibar.

Wajumbe wa Mkutano wa Baraza kuu la CCM wakiserebuka baada ya kuidhinisha kuwa Sixtus Mapunda ndiye Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo ya CCM.

Nice 'Quotation' hapo kiambazani from Qur'an Kareem.
ReplyDelete"كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ , وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ"
(Kila kiliyoko juu yake kitatoweka. Na atabakia mwenyewe MOLA wako mlezi mwenye utukufu na ukarimu)
MOLA mlaze pema peponi Hayati Abeid Aman Karume - AMEEN. Huku nikiwatakia kila la kheri Umoja Wa Vijana CCM na pongezi za dhati kwa Katibu Mkuu mpya wa Umoja huo.
Mdaua Kwanza,
ReplyDeleteSwadakta!!!
Kwa mwendelezo mwingine kwa Quotation hiyo (Kila kilioyoko juu yake kitatoweka) NI KUWA KILA WENYE NIA MBAYA NA MUUNGANO NA CHAMA PIA WATA TOWEKA !!!