Na Andrew Chale

MBUNIFU mkongwe wa mitindo na mavazi nchini, Asia Idarous Khamsin, usiku wa leo Desemba 28 anatarajiwa kupamba shoo kali kwa kuonesha mavazi kwenye Usiku wa Real Unique Tanzania’ utakaofanyika ndani ya Regency Hotel, jijini Dar es Salaam huku ukisindikizwa na Skylight Bend.

Akielezea juu ya onesho hilo la ‘Usiku wa Real Unique Tanzania’ , Asia ‘Mama wa Mitindo’ alisema kuwa itakuwa ni ya kipekee katika kufunga mwaka wa 2013 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2014.

“Ni hatua ya kipekee kwa mimi kuweza kuonesha shoo yangu hii leo katika “Usiku wa Real Unique Tanzania” kwani ndio shoo ya funga mwaka, hivyo wadau wa mitiondo na mavazi watapata kufurahia onesho hilo sambamba na burudani kali kutoka kwa bendi maalufu ya Skylight.” Alisema Asia Idarous.

Mbali na kupamba shoo hiyo kwa kuonesha mavazi yake, Asia Idarous pia ndiye mgeni rasmi kwenye usiku huo wa funga mwaka wa Real Unique Tanzania.

Aidha, katika shoo hiyo, kiingilio ni shilingi 25,000. Huku kwa viti maalum, VIP kikiwa sh 50,000.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...