MAMA mzazi wa mmiliki wa mtandao wa Saluti5,
Said Mode - Bi Desta Mohamed - amefariki ghafla Jumatatu ya tarehe 31/3/2014
saa 1 za jioni.
Alipata homa kali Jumapili mchana, akapelekwa hospitali
(IMTU) akapata matibabu na kuruhusiwa kurudi nyumbani. Hali yake haikuwa mbaya
wala ya kutia mashaka.
Jumatatu akaamka vizuri na akashinda vizuri hadi
saa 12 za jioni hali ipoanza kubadilika tena. Akafariki akiwa njiani kupelekwa
hospitali. Msiba uko Dar es Salaam, Mbezi Beach Old
Bagamoyo Road kituo cha Zena Kawawa.
Mazishi yatafanyika Jumanne 1/4/2014 saa 10
alasiri kwenye makaburi ya Mbezi Beach (New Bagamoyo Road) mbele kidogo ya Masana Hospital.
INNA
LILLAHI WAINNA ILAYHI RRAAJIUN.
"Inna Lillahi Wainna Ilayhi Rajiun". Mola mpokee mja wako, mughufirie dhambize, mnusuru na adhabuzo zote za dunia na akhera, umpumzishe palipo pema peponi na kesho awe ni miongoni mwa waja wako wema watakaoingia katika yako 'Jannatu N'naaem' . - AMEEN.
ReplyDeleteNa tuwe pole ndugu, jamaa na marafiki wote wa Marehemu Bi Desta Mohamed.
Bwana alitoa.....bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Poleni wafiwa na Mwenyezi Mungu awepe nguvu, faraja na kumbukumbu njema za Mama. Amen
ReplyDelete