Waziri wa mambo ya Ndani ya nchi, Mathias Chikawe  akizungumza na waandishi wa Habari ( hawapo pichani) kuhusiana  na Taasisi za Dini na vikundi mbalimbali  kuepuka kushiriki  katika  vitendo ambavyo vinaashilia kuvuruga amani na utulivu nchini jijini  Dar leo.
Baadhi ya Waandishi habari waliohudhuria katika mkutano wa wizara ya Mambo ya Ndani  jijini Dar es salaam leo.Picha Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.


ASASI za Kiraia  zilizosajiliwa chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,vinavyojihusisha na siasa na kuacha katiba zao vitaanza kufutwa kuanzia Aprili 30 mwaka huu.


Hayo ameyasema  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mathias Chikawe wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea katika Kura ya maoni pamoja na Uchaguzi Mkuu,Chikawe amesema serikali iko imara katika kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani hivyo watu wanaotaka kuharibu amani  kutumia asasi za kiraia na kuacha katiba zao watafutwa.


Chikawe amesema katika kuelekea uchaguzi kumekuwa na  asasi za kiraia  zikijihusisha na siasa kwa kuchangisha fedha kwa ajili kuwashawishi viongozi wa siasa wagombee hiyo ni kwenda kinyume na katiba zao na kutakiwa kufutiwa usajili.


Amesema katika suala la ugaidi ni tatizo la dunia hivyo kinachofanyika ni kuimarisha ulinzi katika maeneo yetu na kupata taarifa kwa watu wanaoingia nchini na watu wanaobainika kutoa kuwa na taarifa wanawarudisha katika nchi zao.


Chikawe amesema vijana wa kitanzania ambao wamekamatwa nchini Kenya kuhusika na ugaidi hawana taarifa, wanachokifanya ni kupata taarifa kutoka Kenya kama kuna watu wengine wapo katika kundi la al-shabab.


Aidha amesema jeshi liko imara hivyo wananchi waishi kwa amani kwani serikali ina imarisha ulinzi kuhakikisha amani inakuwepo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...