Waziri wa mali asili  na utalii, Lazaro Nyarandu akiwa na waumini mbalimbali baada ya Ibada ya jumapili Jijini Arusha katika Kanisa la KKKT  Dayosisi ya Mjini Kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi .
Waziri wa maliasili na utalii, Lazaro Nyarandu akibadilishana mawazo na Kada wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, James Ole Milya baada ya ibada ya jumapili iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Diyosisi ya mjini kati Arusha ambapo Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutaja rasmi kuwa tarehe 6 mwezi ujao atachukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kuwania urais .

 **************
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazoro Nyalandu ambaye alishatangaza nia ya kukiomba chama Chake cha Mapinduzi (CCM) kumteua kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, anataraji kuchukua fomu ya kutimiza adhma yake hiyo Juni 7 mwaka huu mjini Dodoma.


ametangaza rasmi kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo baada ya kutangaza nia yake majuma kadhaa yaliyopita mkoani Singida.

Nyalandu anaungana na makada wengine wa CCM kuingia katika kinyang’anyiro hicho ambapo anasema mpango na dhamira yake ya kuwania kuteuliwa na chama chake uko palepale huku akijinasibu kuwa dunia itaandika historia pale atakapo ibuka kidedea kwa kupeperusha bendera ya ccm katika kinyang’anyiro hicho.

 “Mpango na dhamira yangu ya kuomba ridhaa ya Chama changu kuniteua kugombea urais mwaka huu upo palepale na dunia itaandika historia pale nitakapo ibuka kidedea na kuipeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa mwaka huu,” alisema Nyalandu.

Waziri Nyalandu ataungana na makada na Mawaziri wakongwe katika siasa za Tanzania katika kuwania nafasi hiyo ndani ya CCM kama akina Edward Lowassa, Steven Wasira, Bernard Membe, Samuel Sitta, na wengineo wengi ambao tayari wameshatangaza nia na dhamira yao ya kuutaka urais.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...