1. Epuka Kusambaza ujumbe wa uchochezi ama ushawishi wa kisiasa unaoweza kuleta athari kwa jamii yetu kupitia mitandao
2.
Epuka Kusambaza au kutunga ujumbe unaoleta uchochezi wa kidini unaoweza
kupelekea kuvuruga amani na maelewano kwa jamii kupitia mitandao
3.
Epuka Kusambaza picha ama video za utupu ama zilizokosa maadili kwa
jamii kupitia mitandao mbalimbali ( Whatsapp, Facebook, YouTube,
Instagram n.k)
4. Epuka Kusambaza picha ama video za uchochezi wa kidini ama kisiasa kupitia makundi mbalimbali ama mitandao ya kijamii
5. Epuka Kushiriki kusambaza chochote kati ya vilivyotajwa hapo juu (kutuma kama ulivyopokea ) itakugharimu
6. Epuka Wizi kupitia mitandao mbalimbali na mitandao ya simu utakugharimu
7. Epuka Kumpatia mtu line yako ya simu na kutumika kufanyia wizi ama utapeli itakugharimu
8. Epuka Kushiriki kumchafua mtu,taasisi,kikundi cha watu kwa namna yoyote kupitia mitandao pia itakugharimu
9.
Epuka Kupoteza simu bila kutoa taarifa na kufunga mawasiliano hayo
yanaweza kupelekea kutumika kufanya uhalifu na ukaangukia hatarini
10. Epuka Kutumia mtandao kwa utapeli kupitia 'brand' ama jina la mtu itakugharimu
Hukumu
Ni kifungo cha miaka kadhaa gerezani ama faini ya fedha isiyopungua milioni 5 kulingana na kosa lililofanyika (au vyote!)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...