BLOGGER chipukizi nchini Dotto Mzava, amefariki Dunia katika ajali ya barabarani Desemba 14, 2015 hapa jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti wa Mtandao wa Bloggers Nchini, (TBN), ambao marehemu alikuwa ni mwanachama wake, Bw. Joackim Mushi amesema Dotto ambaye alikuwa akifanyia kazi Jamii Media (Wamiliki wa mtandao wa Jamii Forum, amefariki kwa ajali ya pikipiki ingawa haikuelezwa ajali hiyo imetokea maeneo gani hasa ya jiji la Dar es Salaam.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina lake Lihimidiwe Amin.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...