Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Inspekta Jenerali,
Ernest Mangu (katikati), akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya shs. milioni
255 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (wa pili
kushoto), kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kituo cha mawasilianio ya Jeshi la
Polisi. Kulia ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna, Simon
Siro, Mtendaji Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi, Omary
Issa (wa pili kulia) na kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB,
Esther Kitoka.
(Picha na Francis Dande)
(Picha na Francis Dande)
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza katika hafla hiyo.
Na Glory Chacky.
BENKI ya CRDB imekabidhi
msaada wa sh. Milioni 255 kwa Jeshi la polisi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mawasiliano.
Akizungumza jana jijini Dar
es salaam wakati wa makabidhiano hayo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei
amesema kuwa wanatambua kuwa jeshi la polisi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi
linahitaji mfumo bora wa mawasiliano kati yake na raia.
Alisema wameamua kuelekeza
msada huo kwa jeshi la polisi kwa kutambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa
na jeshi hilo ya kuhakusha kwamba kuna usalama na amani kwa raia.
Kimei alisema juhudi za
wanachi katika kujikwamua katika
umaskini hazitafanikiwa kama kutakuwa na
ukosefu wa usalama wa raia na mali zao
kwa ujumla.
Naye mkuu wa Jeshi la polisi
IGP, Ernest Mangu alisema kuwa
wanashukuru kwa msaada huo kwani itasaudia kupunguza matukio ya kiualifu.
“ Kituo hiki kitasaidia kulisogeza jeshi la polisi
karibu zaidi na wananchi na kushirikiana nao katika kutaarifiana juu ya maswala
ya kiualifu pindi yanapojitokeza”alisema Mangu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...