Na Woinde Shizza,Arusha

Hospitali ya wilaya ya Tengeru (Patandi) inakabiriwa na ukosefu wa vitanda ,hali inayopelekea baadhi ya wagonjwa kulala zaidi ya mmoja katika kitanda kimoja.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hii,Wagonjwa hao mara baada ya kupokea msaada wa vyandarua kutoka kwa wafanyakazi wa mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) tawi la Arusha, walisema kuwa wao kama wagonjwa wa hospitali hiyo wamekuwa wakipata tabu sana haswa wakati wakiandikiwa kulazwa,kwani wamekuwa wakibanana sana na wakati mwingine wamekuwa wakikosa kabisa vitanda.

Mmoja wa wagonjwa hao ambaye alijitambulisha kwa jina la Anna Akyoo alisema kuwa wamekuwa wakilala wagonjwa wawili hadi watatu hali ambayo imekuwa ikiwafanya wajisikie vibaya kwani wana banana sana katika vitanda hivyo vichache.
picha ikionyesha wafanyakazi wa NSSF pamoja na Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Tengeru katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi msaada wa vyandarua
wafanyakazi wa NSSF wakiwa wanabadilishana mawazo nje ya hospitali hiyo 
mmoja ya wagonjwa akiwa amekaa kitanda kimoja na watoto wawili wakiwa kila mmoja ana mama yake.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...