KAMPUNI ya WIA GROUP yakabidhi msaada wa Pikipiki Tatu kwa Serikali ya Mtaa wa Oystebay jijini Dar es Salaam leo, ilikuhakikisha Ulinzi na usalama wa mtaa huo unakua imara zaidi.
Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa Pikipiki tatu kwa Serikali za mtaa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam. Mwapongo amewaomba wadau mbalimbali washirikiane katika kuimarisha ulinzi na usalama wa mtaa wa Oysterbay kwa kutoa michango na ushirikiano kwa viongozi wa mtaa huo ili kuepusha madhara yatakayojitokeza hasa ya wizi katika jamii yao.
 Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo (Kulia)akipongezwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay, Zefrini Lubuva jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kukabidhiwa Pikipiki Tatu na Kampuni ya Wia Group kwaajili ya kuimarisha ulizi na usalama wa mtaa wa Oysterbay.
 Meneja mahusiano wa Kampuni ya Wia Group inayojishughulisha na masuala ya mawasiliano, Abraham Mwapongo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay, Zefrini Lubuva, Ofisa Operesheni wa Wilaya ya Kinondoni, Inspeta Msaidizi Samwel Mkama na  Vijana wa Ulinzi na Usalama wa Mtaa wa Oysterbay wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kampuni ya Wia Group kukaidhi pikipiki tatu kwaajili ya ulinzi na usalama wa mataa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. hongera sana wia group kwa uzalendo by victor

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...