Warembo wanaoshiriki shindano la miss kanda ya kaskazini kutoka katika mikoa ya Arusha,Manyara,Tanga na Kilimanjaro wakiwa nje ya hotel ya Clous view sehemu ambayo wanafanyia mazoezi kwa ajili ya shindano hilo linalofanyika july 6 katika viwanja vya ukumbi wa Triple A fm.


Na Woinde Shizza,Arusha

Jamii imetakiwa kuwapa ushirikiano wa kutosha wasichana wanaoshiriki mashindano ya urembo kwani mashindano hayo ni kazi kama vile kazi zingine.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la kumsaka mrembo wa kanda ya kaskazini (Miss Kanda ya kaskazini ) wakati walipokuwa wakiongea kwa nyakati tofauti na Ripota wa Globu ya Jamii ndani ya hotel ambayo warembo hao wameweka kambi kwa ajii ya shindano hilo linalotarajiwa kufanyika mapema jumamosi Julai 6 katika ukumbi wa Triple A uliopo jijini Arusha
warembo hao wakiwa katika pozi 



Mmoja wa washiriki hao aliyejitambulisha kwa jina la Mariamu Mohmed (18) Mshiriki kutoka mkoa wa Manyara alisema kuwa wazazi wengi hususani ndugu wamekuwa wakichukulia shindano hili kama ni sehemu ya uhuni kitu ambacho sio cha kweli



Alibainisha kuwa shindano hili ni zuri na linatoa ajira kwa vijana wengi na mbali na ajira pia linasaidia vijana wengi ambao ni wasichana kujiajiri wenyewe na wengine kuajiriwa katika sehemu mbalimbali.
Kwa upande wake mshiriki kutoka mkoani Tanga Rukaiya Hassan (20) alisema kuwa kuingia katika urembo sio uhuni wala si umalaya kwani, mtu kuwa na tabia chafu kama hizo ni hulka yake mwenyewe na sio mashindano haya ndio yanasababisha mshiriki au mshindi kuwa muhuni
Aidha pia aliongeza kuwa kwa upande wake anaamini kabisa atashinda katika kinyaganyiro hicho kwani anajiamini na aliwasihi wenzake iwapo itatokea mtu akitolewa nje asibahatike kuingia katika hatua ya tano bora asikate tamaa kwani anaweza pia kushiriki katika mambo mengine ikiwa ni pamoja na uwanamitindo.

Kwa upande wake muaandaaji wa shindano hilo Mkurugenzi wa Mwandago Ivestiment, Faustine Mwandago alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yameshakamilika wanasubiri tu siku ya tukio ifike kwani warembo wamepikwa wakapikia vya kutosha . 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...