Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akisalimiana na sehemu ya watendaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) pamoja na wakandarasi wanaosimamia miradi ya umeme vijijini inayosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) mara baada ya kuwasili wilayani Handeni mkoani Tanga.

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela (kushoto) wakifuatilia taarifa ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini inayosimamiwa na REA Awamu ya Pili (REA II) iliyokuwa inasomwa na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Tanga Mhandisi Abdulrahman Nyenye (hayupo pichani)
Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Tanga Mhandisi Abdulrahman Nyenye akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo pamoja na watendaji wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Wilaya ya Handeni, Wizara ya Nishati na Madini, TANESCO na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya REA.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigela akielezea mafanikio ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini iliyotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini Awamu ya Pili (REA II).

Na Greyson Mwase, Tanga

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2020 kila mwananchi anapata umeme wa uhakika na kupelekea uchumi wa nchi kukua kwa kasi.

Profesa Muhongo aliyasema hayo mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme vijijini inayosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini Awamu ya Pili (REA II) kutoka kwa watendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Tanga. Profesa Muhongo yupo mkoani Tanga kwa ajili ya kukagua miradi ya umeme vijijini inayotekelezwa na REA pamoja na kuzungumza na wananchi.

Profesa Muhongo alisema kuwa kwa kutambua mchango wa nishati ya umeme katika ukuaji wa viwanda nchini, serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha kuwa kasi ya usambazaji wa umeme vijijini inaongezeka ili ifikapo mwaka 2020 mgawo wa umeme uwe ni historia

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...