Rais aliyemaliza muda wake wa Rotaly Club tawi la Songea mkoani Ruvuma Michael Sinienga (kushoto) akikabidhi hati na kumbukumbu mbalimbali za ofisi kwa Rais mpya wa club hiyo Albert Kessy (kulia) kabla ya kuzindua mradi wa ukarabati wa choo katika shule ya sekondari Bombambili mkoani Ruvuma jana,  ambapo club hiyo imeanza ukarabati wa choo hicho kwa gharama ya shilingi milioni 4 ili kuwanusuru wanafunzi wa kiume ambao wanatumia choo kimoja kilichoazimwa kwa wanafunzi wa kike.
Rais mpya wa Rotaly Club of Songea mkoani Ruvuma Albert Kessy kulia akichanganya udongo ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mradi wa ukarabati wa choo cha wavulana katika shule ya sekondari Bombambili katika Manispaa ya Songea mkiani Ruvuma ambacho hadi kukamilika itagharimu kiasi cha shilingi milioni 4,kushoto ni Rais wa club hiyo aliyemaliza muda wake Michael Sinienga.
Baadhi ya wanachama wa Rotaly club of Songea mkoani Ruvuma,wakiangalia jana choo cha wavulana katika shule ya sekondari Bombambili kata ya Bombambili katika manispoaa ya Songea ambayo imeharibika na wanafunzi wa kiume 620 wa shule hiyo kujisaidia katika choo kimoja cha wasichana chenye matundu 6,ambapo Rotaly club of Songea iliamua kufanya ukarabati mkubwa wa choo hicho ili kuwanusuru watoto hao.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Bombambili kata ya Bombambili katika manispaa ya Songea wakimsikiliza jana Rais wa Club ya Rotaly tawi la Songea mkoani Ruvuma Albert Kessy(hayupo pichani) kabla ya Rais huyo kuzindua mradi wa ukarabati wa choo cha wavulana shuleni hapo ili kuwanusuru wanafunzi 620 wa kiume wanaolazimika kutumia choo kimoja chenye matundu 6 ambacho kinatumika kwa ajili ya wanafunzi wa kike.
Rais wa Club ya Rotaly tawi la Songea mkoani Ruvuma Alibert Kessy akizungumza jana na wanafunzi na walimu wa shule ya sekondari Bombambili kata ya Bombambili katika manispaa ya Songea kabla ya kuzindua mradi wa ukarabati wa ujenzi wa choo cha wavulana shuleni hapo ili kuwanusuru wanafunzi 620 ambao wanajisaidia choo kimoja ambacho ni cha wanafunzi wa kike kufuatia choo chao kuharibika na mvua miaka miwili iliyopita. Picha na Muhidin Amri

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...