Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Aziz Mlima akiongea na wadau wa takwimu wakati wa uzinduzi wa warsha ya kitaifa kuhusu mpango wa Takwimu za Malengo ya Milenia kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi leo jijini Dar es salaam. Warsha hiyo inashirikisha wadau wa ndani na nje ya nchi.
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa akitoa taarifa ya ofisi yake ilivyojipanga katika kusimamia takwimu za taifa wakati wa uzinduzi wa warsha ya kitaifa kuhusu mpango wa Takwimu za Malengo ya Milenia kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi leo jijini Dar es salaam.  Warsha hiyo inashirikisha wadau wa ndani na nje ya nchi.

 Washiriki wa warsha wakifuatilia hotuba ya uzinduzi wa warsha ya kitaifa kuhusu mpango wa Takwimu za Malengo ya Milenia kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi leo jijini Dar es salaam.
Washiriki wa warsha wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa alipokuwa akitoa taarifa ya ofisi yake wakati wa uzinduzi wa warsha ya kitaifa kuhusu mpango wa Takwimu za Malengo ya Milenia leo jijini Dar es salaam.
(picha na Eleuteri Mangi, MAELEZO)

Na May Simba na Eleuteri Mangi, MAELEZO
SERIKALI kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imezindua mpango wa kuboresha matumizi ya takwimu sahihi katika kutekeleza malengo 17 ya dunia kwa maendeleo ya nchi.

Akizungumza na wadau wa takwimu jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa warsha ya kitaifa kuhusu mpango wa Takwimu za Malengo ya Milenia kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Aziz Mlima amesema kuwa matumizi ya takwimu sahihi yataisaidia Serikali kutekeleza sera na mingo ya ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...